2 samweli 33
Unaona Sauli
anamwambia Daudi kuwa huwezi hata kidogo
kupambana na Goliathi mfilisti na wewe unaweza ukakaa na marafiki zako
ambao wana elimu kubwa kuliko wewe na
roho ya unyonge inakukatisha tamaa kuwa huwezi kukaa wala kuzungumza na watu
hao maana huna elimu kama yao.
Roho ya
unyonge inamwonesha mtu historia ya maisha yake na ya familia yake,kuwa huwezi
maana familia yako ni maskini sana huwezi na kukaa ama kuishi na watu wengine
wenye uwezo ni vigumu.
Roho hiyo inafanya
historia ya maisha yako ikutangulie na kuona kwamba hauwezi kama ulishafanya
kosa ama dhambi ndani ya kusanyiko na hata kama hakuna mtu aliyekuona ama
kushuhudia roho hiyo inakukwamisha na kukufanya ushindwe hata kumtumikia Mungu.
Waamuzi 6:11-15
Roho ya
unyonge ilimshika hata Gideoni na kuona kuwa hawezi maana familia yake ni maskini
sana kuliko familia nyingine.
Ni roho ya
kukatisha sana tamaa na kukufanya kushindwa,kufanya kile ambacho kitakusaidia hivyo
nivyema kusimama na kukemea na kuacha
kabisa maana imekuwa ikiwakwamisha wengi.
Biblia
inasema kuwa kweli yenu iwe kweli,ndiyo na iwe ndiyo na hapana iwe hapana usiangalie roho ya unyonge
maana itakukatisha tamaa na kukukwamisha,maana kuna baadhi ya watu hata
wamekufa bila kufanya kazi ya Mungu na badala yake wamekufa wakiwa na mambo ya
kimungu bila kutumia hata kidogo.
Hata wengine
wameshindwa kufanya biashara kutokana na kuwa na roho hiyo,ila kila jambo ambalo unataka kufanya
ni vyema kumshirikisha Mungu na hapo unaendelea na kazi yako maana
ukimshirikisha Mungu yeye anaongeza mara dufu.
Na hata
Mungu amezungumza na Yeremia na akakataa na kudai kuwa yeye ni mtoto hawezi
kumtumikia Mungu.
Hakuna
mwanadamu ambaye amekamilika ,mwandamu ni mwanadamu tu ila anakamilishwa na
Mungu kupitia jina na damu ya Yesu hivyo ni vyema kusimama na kukataa Roho ya
unyonge ambaye imekuwa ikiwatesa watu wengi hata washirika .
Je wewe unamaoni gani ama nawe unakandamizwa na roho ya unyonge ambayo inaambatana na woga.
Itaendelea......
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni