Waziri wa usalama wa ndani Joseph Nkaisery
Waziri wa usalama nchini Kenya
Joseph Nkaissery amewaomba radhi wanafunzi wa shule ya msingi waliofyatuliwa
gesi ya kutoa machozi wakati walipokuwa wakiandamana kupinga unyakuzi wa
kipande cha ardhi ambacho kilikuwa uwanja wao wa kuchezea.
Bwana Nkaissery amempa mnyakuzi wa
ardhi hio siku moja kuondoa sehemu ya ukuta iliobaki baada ya wanafunzi
kuuangusha na kisha kuondoka katika eneo hilo.
Nkaisery ameongeza kwamba serikali
itaweka uzio katika ardhi hio na kuiwacha kuwa uwanja wa kuchezea wa wanafunzi
hao.
Wakati huohuo, amewaonya
wanaharakati dhidi ya kukiuka sheria kila wakati wanapojiandaa kufanya
maandamano badala ya kuchukua sheria mikononi mwao.
Wanafunzi waliofyatuliwa gesi ya
kutoa machozi kwa kuandamana kupinga unyakuzi wa uwanja wao
Mnamo Jumatatu, wanafunzi watano na
polisi mmoja walijeruhiwa katika vurugzu zilizotokea baada ya wanafunzi
kuandamana kupinga unyakuzi wa ardhi yao kutoka kwa mtu aliyekuwa na mipango ya
kufanya ujenzi.
Wakenya wamekosoa polisi kwa kutumia
nguvu kupita kiasi dhidi ya wanafunzi , hali ambayo imesababisha afisa ammoja
mkuu kusimamishwa kazi kwa mda.
Shirika la kutetea masilahi ya
watoto, la Save The Children, pia limelaani kitendo cha polisi dhidi ya
wanafunzi hao ambao walikuwa wanaandamana kwa amani kutetea uwanja wao uliokuwa
umenyakuliwa.
Source BBC
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni