Baada ya kuhitimisha “Operesheni Milikisha” ambayo imevuma
mwaka 2014 ikiendesha elimu ya ujasiriamali kwa maelfu ya vijana wa MVIMAUTA
ambayo ilizunduliwa mwezi 15/2/2014; jumapili iliyopita (4/1/2015) kwenye ibada
maalum ya kuweka wakfu mwaka mpya, tuliamua kuitangaza rasmi operesheni mpya
inayoitwa MAVUNO ambayo utambulisho wake ni kama ifuatavyo:
Utangulizi
Utendaji wa huduma za WAPO MISSION INTERNATIONAL ambaye ndiye mmiliki wa vyombo
vya habari vya WAPOMEDIA, likiwemo gazeti Msemakweli, huzingatia mpango mkakati
wake wa MAADILI KWA KIZAZI KIPYA ambao una mikakati mkubwa mitatu:
Utangulizi
1.
Urejesho wa maadili kwa kwa vijana
2.
Kuinua vipaji vya uongozi
3.
Kumilikisha uchumi endelevu kwa
kizazi kipya
Katika kutekeleza mikakati hii, kila
mwaka unakuwa na kampeni maalum inayolenga mikakati hii, kulingana na
vipaumbele husika. Kampeni hizi hupewa majina maalum ili kuhamasisha na
kuelimisha na kushirikisha walengwa katika utekeleza wa mikakati yenyewe.
Mwaka juzi (2013 tulikuwa na OPERESHENI
TAKASIKA ikilenga mikakati ya urejesho wa maadili kwa vijana. Mwaka jana (2014)
kipaumbele kilikuwa utekelezaji wa mkakati wa kumilisha uchumi ambao kampeni
yake ilijulikana kama OPERESHENU MILIKISHA.
Japokuwa OPERESHENI MILIKISHA
imehitimishwa mwaka 2014, bado Mkakati wenyewe wa “Kumilikisha uchumi”
unaendelea sawasawa na “Urejesho wa maadili” nao bado unaendelea.
Kwanini Kampeni ya mwaka huu
imepewa jina la OPERESHENI MAVUNO?
Jina la kampeni hii kuitwa mavuno ni
kwa sababu ya vipaumbele vyake ambavyo lengo kuu ni kuanza kupata matunda ya
mipango mingi iliyokwisha kuandaliwa katika miaka takribani mitatu iliyopita.
Ninaposema matunda nina maana ya kuanza kuona kwa macho matokeo ya mipango
iliyobuniwa wakati uliopita.
Ufafanuzi mzuri ni miradi ya vijana
ya kumilikishwa uchumi ambayo mwaka jana walikuwa wakiandaliwa kimafunzo, sasa
mwaka huu wanaingizwa katika utendaji wenyewe ili waone uhalisia wa mikakati ya
kumiliki uchumi
Wakati wa kuweka wakfu operesheni
mavuno nilitumia mfano wa kibiblia ambapo Isaka alipanda mbegu na kuvuna mavuno
mengi sana katika mwaka ule ule, japokuwa ilikuwa ni wakati wa njaa katika nchi
ile.
Katika mwaka huu, tumetoa kipaumbele
cha kuwepo kwa mradi ambao utatoa mazao ambayo yanatawahamasisha vijana
kuondokana na kukata tamaa kimaisha kwa sababu ya “ukosefu wa ajira”
Lakini mbali na mavuno ya kiuchumi,
pia tunakwenda kutoa kipaumbele kwa mavuno ya kiroho. Mavuno ya kiroho ni
msamiati wa Yesu Kristo mwenyewe aliposema, “Mavuno ni mengi, bali watendakazi
ni wachache.”! Yesu hakumaanisha kuvuna mahindi, bali “wenyedhambi kurejesha
mahusiano ya kiimani na Mungu wa kweli baada ya kutawanyika kama kondoo wasio
na mchungaji.
Kwa maelezo haya unaweza kuona
kwamba, zoezi la “mavuno ya kiroho” ni utekelezaji endelevu wa “urejesho wa
maadili ya kibiblia kwa jamii” ukienda sanjari na “kumilikisha uchumi” kwa
walengwa.
Programu mpya za Operesheni Mavuno
Kampeni ya Mwaka huu inakuja na
program mpya ambazo zitanatarajiwa kuanza rasmi mwezi Februari kwenye huduma za
kila Jumapili kwenye kituo cha BCIC Mbezi beach ambazo ni kama ifuatavyo:
1.
Ibada za
Kiingereza kwa jamii ya kimataifa
Kufuatia ongezeko la wageni kutoka
mataifa ya nje ndani ya miji mikuu likiwemo jiji la Dar es Salaam, tayari
hitaji maalum ya huduma za kiroho limekuwa kubwa kuliko miaka ya nyuma. Kuna
ongezeko kubwa la wafanyabiashara na wataalamu mbali mbali, ikiwa ni pamoja na
wanafunzi wa mataifa ya nje wanaokuja kusoma kwenye vyuo vikuu hapa nchini.
Katika kukidhi mahitaji ya kiroho
kwa jamii ya kimataifa, Februari tunafungua ibada maalum kwa ajili yao, ambazo
zitaendeshwa kwa lugha ya Kingereza.
2.
Chuo cha
Biblia cha Jumapili
Uzoefu wa huduma za kiinjili
umetufundisha kwamba, kumekuwepo tatizo sugu la watu wengi wanaookolewa huishia
kuwa mbegu zilizoanguka “njiani” au kwenye “miamba” kama Yesu alivyosimulia
katika maandiko.
Chanzo kikubwa cha tatizo hili sugu
la udumavu wa kiroho ni utekelezaji dhaifu wa agizo kuu la Yesu Kristo
aliposema: “Basi
enendeni mkawafanye mataifa yote kuwa wanafunzi, mkiwabatiza kwa jina la Baba,
na Mwana, na Roho Mtakatifu; na kuwafundisha kuyashika yote niliyowaamuru
ninyi; na tazama, mimi nipo pamoja nanyi siku zote hadi ukamilifu wa dahari.”
(MT 28:19-20)
UKifuatilia kwa makini kile Yesu
alichomaanisha katika agizo hili ni kwamba alitaka “jamii ya Wasioamini”
kutengenezwa kutoka kutokuamini/upagani na kufanyika wanafunzi wa Yesu kweli
kweli. Aidha, Yesu alionesha kuwepo kwa mfumo wa kufundisha/kuelekeza jinsi ya
kutekeleza katika maisha, amri na maagizo ambayo Yesu aliwaamuru wanafunzi wake
kuyaishi.
Kisha Yesu anatoa ahadi kwamba yeye
mwenyewe atahakikisha udhihiriko wa utendaji wa nguvu za Roho Mtakatifu za
kuleta mageuzi ya kitabia, kufukuza majeshi ya pepo wachafu yenye kusababisha
magonjwa na ufukara uliokithiri. Lakini ukifuatilia katika uhalisia wa kiinjili
utashuhudia udhaifu kama ifuatavyo:
- Upungufu wa Injili kamili yenye mamlaka ya kuwafanya wasioamini kutubu na kugeuka kutoka kwenye mapokeo ya mila, desturi za kipagani;
- Hofu ya kuihubiri na kuifundisha kweli kwa visingizio vya wafuasi kuhama madhehebu ya dini, na kupungua kwa matoleo ya sadaka kwenye makusanyiko
- Mfumo dhaifu wa kuwafanya kuwa wafuasi wa mapokeo ya madhehebu ya kidini, yasiyo Neno hai lenye nguvu za Mungu za kubadilisha tabia na mienendo ya wafuasi
Katika kutaka kushughulikia tatizo
hili tumeazimia Kuanzishwa kwa chuo cha
Biblia cha Jumapili chenye mitaala iliyobeba kile ambacho Yesu aliagiza
“kufundisha kuyashika yote aliyowaamuru”!
Itaendelea
toleo lijalo.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni