MCHUNGAJI kiongozi
wa kanisa la EAGT City Centre Florian Josephat Katunzi amekabidhi nyumba ya
kisasa aliyoijenga kwa ajili ya Mdhamini Mkuu wa Kanisa hilo Mdhamini na
Mshauri Mkuu wa kanisa la EAGT, ambaye pia ni mmoja wa waanzilishi wa kanisa
hilo, Mch. Anyandwile Mwakisyala, katika
eneo la Nsonyanga Mbarali Mbeya, katika
sherehe iliyoliza na kuchekesha viongozi na wakazi wa mbeya..
Akiongea kwa furaha ya ajabu mbele ya ummati wa
wachungaji wa kanisa hilo, wakiongozwa na Kaimu Askofu Mkuu, Asumwisyene
Mwaisabila, Mdhamini huyo alisema yeye
alizaliwa mwaka 1924, na katika maisha yake hakupata mtoto wa kumzaa, alijitoa
kumtumikia Mungu katika maisha yake yote, lakini alikuwa akiishi machakani, Mch. Katunzi amemuokoa kwa kumjengea nyumba ya kisasa yenye kila
kitu ndani.
“Wengi wanaomba watoto wanafika mpaka Ulaya kutafuata watoto,
lakini hawapati, mimi toka ujana wangu sina mtoto.. hatuna mtoto natamka mbele ya umati huu, na
Unaponisikiliza sauti hii imfikie Mungu.
Natamka nasema huyu Katunzi ndiye mtoto wangu wa kwanza, huyu ni mtoto wangu wa
kwanza kuanzia sasa…. Kwa jambo lililotokea hata angetoka tumboni mwangu
asingelifanya ila angeweza kuja
kuniharibu na tena huenda angeweza
kutamka kuwa mbona huyu kesho atakufa, lakini huyu mtoto alipotoka simjui, kwao
sikujui, mama yake simjui, baba yake simjui, sasa kwa kuwa Mungu amefanya
hivyo, kufuatana na huyu mtoto aambatane na mimi na mimi naambatana naye kwamba
yeye ndiye mtoto wangu mpaka maisha
yangu nitakapokwenda kwa Mungu ni mtoto wangu wa maisha yangu,”alisema na kuongeza:
“Maana alitoka kwa Mungu kujenga jengo hili si
kawaida ni la gharama , ni la mamilioni,
sasa mamilioni haya angekuwa sijui si Mungu wapo wanaoua baba zao wakiona
nyumba hii kama hii anaweza kumuwahisha baba yake, leo huyu hawezi kuniwahisha.
Mama umesikia hawezi kutuwahisha mpaka siku zetu zitakapokwisha namuomba Mungu
amuweke nyuma yetu na ninakokwenda mimi anifuate. Mwanangu hakika ni Mungu sio
wewe.”
Kisha Mdhamini huyo aliongeza: “Naweka mkono juu yako
kukuambatanisha na mimi, bara za Mungu na ulizi ziwe juu yako, Mungu asikuacha
na akuinua na kukuweka mahali pa juu, uwe mkuu katika utumishi huu ufuate nyayo
za Askofu Kulola Mwanzilishi wa kanisa
hili.”
KAIMU ASKOFU MKUU
Naye Kaimu Askofu Mkuu wa kanisa la EAGT, alipopokea
kipaza sauti alisema: “Nyumba hii haikujengwa na Kanisa la EAGT, wala
haikujengwa na Kamati kuu, wala Mfuko Mkuu, Yupo katibu mkuu hapa ni shahidi,
bali ni Mungu wa mbinguni. Ashukuriwe kumuona mzee huyu anakula matunda yake ya
huduma ya kazi yake. Yesu alisema alipokuwa anambatiza Yohana, usiseme tuna
baba yetu ibrahimu, Mungu anaweza akainua mawe wawe watoto wake, kwa hiyo mtu
au watu walioijenga nyumba hii hata mimi kama Askofu sijui ila wewe ……mimi na
mshauri mkuu na Mwakipesile (Brown Mwakipesile
Katibu Mkuu) tumeitwa na kumkabidhi nyumba hii baba huyu ….Mwacheni Mungu aitwe
Mungu aliyefanya maajabu haya, inatosha..”
Kisha alipopewa nafsi ya pili kuongea Kaimu Askofu Mkuu
alisema: “Tunahitaji vijana ndani ya kanisa kama Mchungaji Katunzi wenye kuona
na kuthamini wazee, wenye mzigo na kazi ya Mungu. Mfuateni huyu mchungaji Mungu
ambariki sana.”
KATIBU MKUU
Katibu Mkuu katika maombi yake alisema: “Sisi ni watu wa
Mungu na leo tunasimama mbele ya jengo hilo, jengo ambalo ni tukufu kwa Mungu
na kama ambavyo tumesikia pale kanisani na Mjenzi wa nyumba ni mtumishi wa
Mungu na mama hapa kupata nyumba hii ni
heshima kwa Mungu, heshima kwa kanisa, Baraka kwa familia na Baraka kwa kanisa
pia name nasoma mstari mmoja tu juu ya jambo hili katika Injili ya Yohana 1:1,
Biblia inasema………….. Bila Yesu Mzee wetu asingepata nyumba hii, lakini kwa
sababu amemwamini Yesu Yeye ndiye mwanzo wa nyumba hii na ndiye mwisho wa
nyumba hii name katika jina la Mungu baba na Mungu Mwana na Roho Mtakatifu nakata
utepe huu kama ishara ya kuifungua nyumba hii.”
MCHUNGAJI KATUNZI
Mchungaji Katunzi
alipopewa kipaza sauti alisema: “Wazee wangu, Askofu wetu Mkuu, Katibu wetu
Mkuu na maaskofu wote mliopo, nawasalimu
katika jina la Bwana. Niseme kitu kimoja tu, nilifika hapa mwaka jana mwezi wa sita, nilikuwa nakwenda
Tunduma kwenye huduma nikasema ngoja nikamsalimie mzee kwa mara ya kwanza
nilifika hapa mwaka jana nashukuru Mungu nikapata mzigo wa kiimani kabisa
kwamba tumjengee mzee wetu nyumba nzuri, kama yeye alivyo mzuri, nikamwambia
mzee nitakujengea nyumba, lakini nilisema kwa imani nasikujua itakuwa kumbwa
hivi. Nashukuru Mungu ametufanikisha nyumba ni hii sasa ipo. Ni heshima kwa
Mungu …..”
Mshauri huyo alimuwekea mikono mchungaji Katunzi na
kumbariki akimuomba Mungu amuinue na kunyooshea safari yake ya utumishi, katika
kanisa lake la EAGT. Aibariki familia yake
na kuyanyoosha mapito yake.
Tukio hilo linaakisi
lile la Askofu Mkuu na Mwanzilishi wa EAGT, Dk. Moses Kulola
alilolifanya siku chache kabla ya kutwaliwa alipomuwekea Mchungaji Katunzi
mikono na kumuambia kuwa amemwachia mikoba ya kazi ya uinjilisti aliyokuwa
akiifanya katika uhai wake na akamtaka kufuata nyayo zake.
Askofu Kulola aliandika hata kwenye wosia wake kuwa
Katunzi ndiye msimamizi wa mali zake alizoacha.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni