YESU NI JIBU

Jumatano, 14 Januari 2015

KANISA LA TAG SAHARA SPIRITUAL CENTE WAWAKUMBUKWA WANAFUNZI WENYE ULEMAVU WA AKILI:


Taasisi mbalimbali za kiserikali na binafsi sanjari na mashirika ya dini na watu binafsi wametakiwa kujitokeza na kuwasaidia watu wenye mahitaji maalum kwa lengo la kuwakwamua na kujisikia kama watu wengine katika maisha yao.
Askofu Geofrey Masawe kulia mwenye koti jeusi akimkabidhi TV ya nchi 21 na deki mwalimu mkuu wa shule ya umoja Bwana 
Abeli Ali Dimbwa na katikati ni mzee kiongozi Mzee Harrison Myombe.
Kauli hiyo imetolewa na Askofu wa jimbo la mashariki kaskazini  ambaye pia ni mchungaji kiongozi wa kanisa la TAG Mabibo Sahara askofu Geofrey Massawe wakati akikabidhi TV ya nchi 21 na deki yake kwa mkuu wa shule ya umoja iliyopo kata ya Mabibo manispaa ya kinondoni  ambayo ina kitengo cha watoto wenye ulemavu wa akili jijini Dar es salaam kwa lengo la kuwasaidia watoto hao kujifunza.
Aidha Askofu Massawe alisema kuwa kama kanisa wameona uhitaji wa watoto hao wa shule hiyo ya umoja walipotembelea shule hiyo na kujionea na kusikia pia mahitaji yao na kuona kuwa ni vyema kuwasaidia kwa baadhi ya vifaa ambavyo vitawasaidia kujifunza maana watoto hao wanahitaji kujifunza kwa kuona wakati mwingine.
Hata hivyo amewataka taasisi na mashirikika ya dini na yasio ya kiserikali kujitokeza kuwasaidia watoto hao maana wanahitaji kusaidiwa ili nao waweze kupata elimu ambayo itawasaidia kujitambua na kuweza kuishi ndani ya jamiii.



Mzee kiongozi Harrison Myombe mwenye miwani akizungumza na mkuu wa shule ya umoja BWana Abel Dimbwa huku kulia askofu Masawe akisikiliza kwa makini pamoja na watu wengine.
Akizungumza na blog hili ofisini kwake mchungaji Oliver Massawe ambaye ni mchungaji msaidizi wa kanisa hilo la TAG Mabibo Sahara alisema kuwa inapendeza sana kama watu waote wenye uwezo bila kujali dini,itikadi wala rangi kujitokeza kuwasaidia watoto wenye ulemavu wa akili wanaosoma katika shule ya msingi umoja ili nao wajisikie kama watoto wengine.
Tatizo la watoto wenye ulemavu wa akili sio la wazazi wa watoto  hao pekee hapana ni tatizo la jamii nzima hivyo nawasihi viongozi wa dini ,viongozio wa serikali na vyama vya siasa pamoja na asasi mbalimbali kujitokeza kuwasaidia shule hiyo ili watoto hawa wapate vifaa ambavyo vitawawezesha kuishi ndani ya jamii,alisema mchungaji Oliva Massawe.
 Aliongeza kuwa ni  jukumu la kanisa kuwasaidia kimwili watu wenye ulemavu wa aina mbalimbali,mbali na kuwasaidia kiroho inabidi kujitokeza na kuhakikisha kusaidia kupunguza mapungufu ambayo yanaonekana katika baadhi ya shule za watoto wenye ulemavu.
Kwa upande wake Mwalimu Mkuu wa shule hiyo ya msingi Umoja mwalimu Abeli Ali Dimbwa amesema kuwa shule hiyo inamapungufu mengi ambapo ameendelea kuto wito kwa wadau mbalimbali kujitokeza kusaidia shule hiyo ili watoto wenye ulemavu wa akili wanaosoma hapo kupata vifaa muhimu ambayo itawasaidia kujifunza.

 
 
 Wanafunzi wenye ulemavu wa akili wakipokea zawadi ya tv ambayo itawasaidia katika masomo yao.
Ni vyema ifahamike kuwa jukumu la kuwasaidia watoto wenye ulemavu wa aina mbalimbali na wanaoishi katika mazingira hatarishi ni jukumu la kila mwanajamii kuhakikisha kuwa wanasaidiwa ili nao wafikie malengo yao katika jamiii .

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni