YESU NI JIBU

Jumanne, 3 Machi 2015

WAIMBAJI WA NYIMBO ZA INJILI MNAKWENDA MBINGU YA NANI? UNGANA NA MCHUNGAJI MWANGOMOLA

Biblia inaonya sana, kuhusu kupenda pesa, pesa kama pesa sio mbaya tatizo ni kuipenda, kwenye Biblia kuna maneno haya, fedha ni jawabu la mambo yote. Mhubiri 10:19 Karamu hufanywa kwa ajili ya kicheko na divai huyafurahisha maisha, na fedha kuleta jawabu la maombi yote. Mwisho wa kunukuu. Pamoja na kwamba fedha ni jawabu la mambo yote, kama Biblia isemavyo pia kumbukeni kwamba Yesu ni jibu, pia fedha ipatikane kihalali na moyo wako usiegemee huko hata moyo wako ukashikwa na fedha hata ukamsahau Mungu kama mlivyomsahau, mkizipenda fedha kuliko Mungu na kazy yake. Hebu fikiri, Mchungaji anakutoa huko alikokutoa, anakuleta Kanisani kwa,e ili umtumikie Mungu kwa kuongoza sifa, unaanza hapo Kanisani, kuongosa sifa baadae ukajulikana, anakuja mtu na kukurubuni kwamba utoke huko na kumfuata Mchungaji mwingine ambaye hakukuleta mjini, maana wengi wenu mmetoka huko, mlikotoka sio wa hapa mjini hivyo unamwacha Mchungaji wako aliyekugharamia kisa huyo mwingien kakuuuliza kwani wanakulipa shilingi ngapi? unataja kiasi unachopewa anakwambia mbona unalipwa ujira mdogo, mimi nitakulipa zaidi baadaye unaondoka na kumwacha Mchungaji wako aliyekutoa huko ulikokuwa na nyie Wachungaji wenye fedha muache kurubuni waimbaji, kwa fedha zenu, sio vizuri na mtapata hukumu maana mnaleta, manung’uniko kwa watumishi wenzenu, Mtumishi wa Mungu, Paulo anamwonya sana mwanae Timotheo juu ya ubaya wa kupenda pesa, kupenda pesa ni tatizo enyi waimbaji wa nyimbo za Injili.

Hebu soma hapa 1Tim. 6:10 Maana shina moja la mabaya ya kila namna ni kupenda fedha, ambayo wengine hali wakiitamani hiyo wamefarakana na imani na kujichoma kwa maumivu mengi. Mwisho wa kunukuu. Hapa Biblia inasema shina moja sio mawili bali moja ni kupenda fedha, kuzipenda fedha ndio tatizo, sio fedha zenyewe, maana fedha ni jawabu, tatizo kuzipenda. Maana wanadamu wana matatizo ya kutaka kutupa lawama kwa mtu mwingine utamsikia mtu akisema fedha bwana ni shetani, pesa sio shetani, pesa ni makaratasi yaliyotengenezwa. Shetani ni roho haonekani kwa macho, pesa zinaonekana kwa macho tatizo unalo wewe unayezipenda kufa wewe ndiyo unafungua mlango ili shetani akutumie baada ya kuona moyo wake umeelekea kupenda fedha kuliko Mungu.

Enyi waimbaji wa nyimbo za injili, nawaonya acheni kuzipenda pesa, ziondoeni mioyoni mwenu muwekeni Bwana Yesu, hapa zilipokaa pesa katika moyo wako, mwache akae Bwana Yesu vinginevyo hamtafika mbinguni, kuimba kwenyewe sio kigezo cha kwenda mbinguni, hakuna mtu yeyote atakayeenda mbinguni kwa kuimba, kuhubiri, kutoa pepo, kutoa sadaka, kuwa mzee wa kanisa au kuwa Mchungaji, Mtume, Nabii, Mwalimu, Mwinjilisti bali mtakatifu pekee ndiye atakayekanyaga pale juu kwa Baba aliye Mtakatifu. Si vinginevyo wala umaarufu wenu hautawafanya muingie mbinguni, kwa sababu kama ni umaarufu Bwana Yesu anawashinda, kama ni kujulikana Bwana Yesu anawashinda, tafuteni kuwa watakatifu.

Soma hapa Ebr. 12:14 Tafuteni kwa bidii kuwa na amani na watu wote, na huo utakatifu, ambao hapana mtu atakayemwona Bwana asipokuwa nao. Mwisho wa kunukuu. Hapa vinazungumzwa vitu viwili ambayo mtu akiwa navyo atamwona Bwana, kutafuta amani na huo utakatifu, hatuoni uimbaji wala umaarufu kuwa mtu akiwa na vitu hivyo atamwona Bwana, sasa nyinyi waimbaji wa nyimbo za injili, hamna amani na watu wote kwa sababu, mmechukua fedha za watu ili mkaimbe hamkwenda kuimba pesa mmlamba kuimba hamtaki amani itatoka wapi? Mioyo ya watumishi mbalimbali inavuja damu kwa dhuluma yenu, halafu hamajli kabisa wala hamna woga kabisa nyie kiboko. Hofu ya Mungu hakuna kabisa kuhusu utakatifu jibu mnalo wenyewe lakini mnajua kabisa kwamba hamkidhi vigezo vya utakatifu maana si tunaishi na nyie tunawaona.

Jambo lingine linalowadanganya ni umaarufu mlionao sasa ngoja niwaambie umaarufu unaotakiwa maana hili nalo ni tatizo lingine mkijidai kuwa mnajulikana na sifa kibao. Yer. 9:23 – 24 Bwana asema hivi, mwenye hekima asijisifu kwa sababu ya hekima yake, wala mwenye nguvu asijisifu kwa sababu ya nguvu zake, wala tajiri asijisifu kwa sababu ya utajiri wake bali ajisifuye na ajisifu kwa sababu hii ya kwamba ananifahamu mimi na kumjua ya kuwa mimi ni Bwana nitendaye wema na hukumu na haki katika nchi, maana mimi napendezwa na mambo hayo, asema Bwana. Mwisho wa kunukuu. Kwa hiyo kama waimbaji wanataka kujulikana wajulikane kwa Bwana kwamba wanamfahamu na kwamba na yeye anawajua, je ni kweli Bwana anawajua? Maana yeye anasema anapendezwa na mambo ya haki katika nchi (dunia) kwa hiyo bWana anataka haki katika vipawa vyenu vya uimbaji kitu ambacho ninyi hamna maana mmewadhulumu watu pesa zao, mlipoliipwa hamkwenda kuimba hapo haki hakuna.

Katika kitabu cha Wakorintho Paulo anasema hivi 2Kor. 10:17 – 18. Lakini, yeye ajisifuye na ajisifu katika Bwana maana mtu mwenye kukubaliwa si yeye ajisifuye, bali yeye asifiwaye na Bwana.

Waimbaji wa nyimbo za Injili, jitahidini snaa katika kuishi kwenu  maisha matakatifu ili mkubaliwe na Bwana, si vinginevyo, pia mkijitahidi sana ili mkubaliwe nay eye kama Biblia isemavyo.

Mmepewa kipawa, kitumieni kwa haki vingienvyo mtakwenda na maji, hakuna huruma kwa sababu huruma inajitukuza kwenye hukumu. Yakobo 2:13 Maana hukumu haina huruma kwake yeye asiyeona huruma. Huruma hujitukuza juu ya hukumu. Mwisho wa kunukuu. Lazima muwe watu wa huruma na kutoa huduma zenu popote mtakapoitwa bila ubaguzi wa aina yoyote ile.

Itaendelea usikose sehemu ya pili.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni