Mabomu mawili yamelipuka yakilenga makanisa
mawili yaliyokuwa yamejaa watu kwenye mji wa Lahore chini Pakistan wakati watu
walipokuwa wakihudhuria misa ya jumapili.
Polisi wanasema kuwa takriban watu 6 wameuawa
na wengine kadhaa kujeruhiwa.
Mashambulizi hayo yanaoyoaminika kuwa ya
kujitoa mhanga yalifanyika eneo lenye waumini wengi wa kikristo la Youhanabad
Sehemu ya kundi la Taliban linalofahamika
kama Jamatul Ahra limesema kuwa ndilo lililoendesha shambulizi hilo.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni