YESU NI JIBU

Jumamosi, 28 Machi 2015

LEO NI SIKU NYINGINE AMBAYO TUNAKUTANA KWENYE ENEO LA IFAHAMU BIBLIA YAKO.



1.Ni mtu yupi ambaye Bwana Mungu alitaka kumtumia katika nchi ya Benjamini kuwaonya watu makosa yao na hakuwa tayari kutokana na umri wake na katika biblia inapatikana katika kitabu gani?
Jibu:Ni Yeremia,
Kitabu cha Yeremia 1:1-7
2.Mshauri wa ajabu,Mungu mwenye nguvu,Baba wa milele,mfalme wa Amani;hayo yote ni majina ya nani na kwa ufafanuzi tunapate wapi?
JIBU ni Bwana YESU
Isaya 9:6
3.Katika wanafunzi wa Bwana Yesu (Tenashara) ni yupi ambaye ameamua kumkana kwa sababu ya fedha bwana Yesu.
JIBU;Yuda ambaye pia aliitwa Iskariote
luka 22:3-6,yohana13:2,27,Marko 14:10-11.
4.Ni mfalme yupi ambaye amemwomba Mungu juu ya hekanu kwa kusema ikiwa mbingu zimefungwa hata hakuna mvua ,kwa sababu wanadamu wamekukosea wewe Mungu ,wakiomba kwa kukabili hekaluni Mungu asikie dua zao na na kuwa samehe dhambi yao.
JIBU:mfalme Suleimani
1wafalme 8:35-40;
2 wafalme 7:12-15
5.Kwanini malkia Esta aliwaamuru wayahudi waliokuwepo Shushani kufunga na kuomba kwa siku tatu bila kula mchana na usiku.
JIBU:Kwa lengo la kuingia kwa mfalme kinyume cha sheria maana hamani bin hamedatha  alipanga kuwaangamiza wayahudi wote.
esta 4:15-17,
6.Ni Sababu gani kuu ya wayahudi kuuuwawa na hamadi nani alisababisha kutokea kwa kosa hilo la wayahudi kuuwawa.
JIBU:ni kwa sababau mara baada ya kupandishwa cheo kuwa mkuu wa maakida wote alitaka kuinamiwa na kusujudiwe na kila mtu,alipoona Mordekai hamsujudii aligadhibika sana,
Esta 3:5(-10).


Hakuna maoni :

Chapisha Maoni