YESU NI JIBU

Ijumaa, 27 Machi 2015

MAENDELEO YA TEKNOLOGIA IMEONGEZEKA SANA DUNIANI MTU AWEKEWA MOYO WA MTU MWINGINE NA KUENDELEA KUISHI:



Cambridgeshire

Madaktari wa upasuaji huko Cambridgeshire wamefanya upandikizaji wa kwanza wa moyo barani Ulaya kwa kutumia moyo mwengine uliosimama kufanya kazi.
Myoyo hiyo hupatikana kutoka kwa watu waliokufa lakini ambao myoyo yao bado inafanya kazi.
Katika upasuaji huo,moyo huo ulitoka kwa mtu ambaye mapafu yake na moyo wake ulikuwa haufanyi kazi.
Hospitali ya Papworth inasema kuwa mbinu hiyo huenda ikaongeza idadi ya myoyo inayopatikana kwa asilimia 25.
Mgonjwa aliyewekwa moyo mpya kwa jina Huseyin Ulucan, mwenye umri wa miaka 60, kutoka London,alikabiliwa na shinikizo la moyo mwaka 2008.
Alisema:kabla ya upasuaji,sikuweza kutembea na nilichoka sana,kwa hakika siku na maisha mazuri.
Upandikizaji wa moyo
Lakini anasema kuwa amefurahishwa na kuimarika kwa afya yake tangu upandikizaji huo.
Kwa sasa najisikia mwenye nguvu kila siku,na nimetembea hadi haospitalini asubuhi hii bila tatizo.
Kumekuwa na visa 171 vya upandikizaji wa myoyo katika kipindi cha miaka 12 iliopita nchini Uingereza.
Lakini mahitaji yanashinda myoyo iliopo ,hivyobasi wagonjwa wengine hungoja kwa miaka mitatu kupata kiungo kinachowafaa.
Wengi ya wagonjwa hao hufariki kabla ya kiungo kupatikana.
Wewe unamaoni gani?kuhusu hili,
chanzo BBC,

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni