Madaktari wa upasuaji huko
Cambridgeshire wamefanya upandikizaji wa kwanza wa moyo barani Ulaya kwa
kutumia moyo mwengine uliosimama kufanya kazi.
Myoyo hiyo hupatikana kutoka kwa
watu waliokufa lakini ambao myoyo yao bado inafanya kazi.
Katika upasuaji huo,moyo huo ulitoka
kwa mtu ambaye mapafu yake na moyo wake ulikuwa haufanyi kazi.
Hospitali ya Papworth inasema kuwa
mbinu hiyo huenda ikaongeza idadi ya myoyo inayopatikana kwa asilimia 25.
Mgonjwa aliyewekwa moyo mpya kwa
jina Huseyin Ulucan, mwenye umri wa miaka 60, kutoka London,alikabiliwa na
shinikizo la moyo mwaka 2008.
Alisema:kabla ya upasuaji,sikuweza
kutembea na nilichoka sana,kwa hakika siku na maisha mazuri.
Lakini anasema kuwa amefurahishwa na
kuimarika kwa afya yake tangu upandikizaji huo.
Kwa sasa najisikia mwenye nguvu kila
siku,na nimetembea hadi haospitalini asubuhi hii bila tatizo.
Kumekuwa na visa 171 vya
upandikizaji wa myoyo katika kipindi cha miaka 12 iliopita nchini Uingereza.
Lakini mahitaji yanashinda myoyo
iliopo ,hivyobasi wagonjwa wengine hungoja kwa miaka mitatu kupata kiungo
kinachowafaa.
Wengi ya wagonjwa hao hufariki kabla
ya kiungo kupatikana.
Wewe unamaoni gani?kuhusu hili,
chanzo BBC,
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni