YESU NI JIBU

Alhamisi, 10 Machi 2016

JENNIFER MGENDI KUNGURUMA TAMASHA LA PASAKA.

MWIMBAJI na Msanii mahiri wa Filamu Tanzania, Jennifer Mgendi  amelipania Tamasha la Pasaka linalotarajia kuanza Machi 26-28 katika mikoa ya Geita, Mwanza na Kahama.

Kwa mujibu wa Mgendi hivi sasa analisubiri kwa amu tamasha hilo ambalo lina malengo ya kusifu na kuabudu kupitia nyimbo mbalimbali za Injili sambamba na viongozi wa dini mbalimbali.

Mgendi alisema analisubiri kwa hamu Tamasha la Pasaka ambalo litafanyika mikoa ya Kanda ya Ziwa ambako hivi sasa waimbaji wengine pia wanaendelea na mazoezi kuelekea tamasha hilo.Mgendi alitumia fursa hiyo kuwaomba mashabiki wake wa mikoa hiyo hasa wa nyimbo za Injili na Filamu  kujitokeza kwa wingi kwenye tamasha hilo ili kupokea baraka za bwana kupitia uimbaji.

Aidha Mgendi alisema katika tamasha hilo aakuwa na albamu nyingine mpya inayokwenda kwa jina lka Nyuma ya Mlima  ambako alisisitiza kuwaomba mashabiki wa muziki wa Injili kujitokeza kuipata albamu hiyo.
Anazitaja nyimbo zilizoko kwenye albamu hiyo ni pamoja na Nyuma ya Mlima, Naomba Uzima, Bwana ni Ebenezer, Nawashukuru adui na Nitafika lini Remix.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni