YESU NI JIBU

Jumanne, 7 Oktoba 2014

UKATILI WA KIJINSIA BADO NI CHANGAMOTO KATIKA JAMII



Licha ya juhudi mbalimbali zinazofanywa na serikali pamoja na taasisi zisizo za kiserikali katika kuhamasisha na kupambana na vitendo vya ukatili wa kijinsia bado vitendo vya kikatili vinaendelea kujitokeza katika jamii kadri siku zinavyoongezeka.
Tunapo zungumzia vitendo vya ukatili wa kijinsia  tunamaanisha kuwa ni pamoja na vipigo kwa wanawake,wanaume kutelekeza watoto na familia zao,ukeketaji,ndoa za utotoni,mimba za utotoni  pamoja na mauaji ya vikongwe.
Yapo  mashirika na taasisi mbalimbali za serikali na zisizo za serikali ambazo zimekuwa mstari wa mbele katika kupambana na ukatili wa kijinsia kwa kutoa elimu kwa jamii kutokana na athari zitokanazo na ukatili wa kijinsia.
Mashirika na taasisi hizo ambazo ni za kiserikali na zisizo za kiserikali  zinazopambana kwa kiasi kikubwa kuhakikisha vitendo vya ukatili wa kijinsia vinapungua hapa nchini ni pamoja na chama cha wahandishi wa habari wanawake Tanzania [TAMWA], Mtandao wa jinsia Tanzania[TGNP], kituo cha msaada wa kisheria kwa  wanawake[WILAC], Kituo cha sheria na haki za binadamu[ LHRC] pamoja na mashirika mengine yanayopinga vitendo vya ukatili wa kijinsia hapa nchini.
Katika kupambana na changamoto mbalimbali zitokanazo na ukatili wa kijisia serikali kupitia jeshi la polisi iliamua kuanzisha  kitengo cha madawati  ya jinsia katika vituo vya polisi hii yote ni katika juhudi ya kuhakikisha kuwa vitendo vya ukatili wa kijinsia vinapungua au kukoma kabisa na kwa kiasi kikubwa madawati hayo ya mechangia kupunguza vitendo vya ukatili wa kjinsia kwa kiasi flani katika jamii yetu.
Hivi karibuni chama cha wandishi wa habari wanawake  Tanzania TAMWA kilizindua ripoti ya utafiti ya mwaka 2012/2013 ulifanyika katika wilaya ishirini za Tanzania Bara na Zanzibar kuhusiana na hali ya ukatili wa kijinsia nchini,hali iliyoonesha kuwa hali ya ukatili wa kijinsia bado ipo kwa kiasi kikubwa katika jamii.
Kwa mujibu wa ripoti hiyo ya utafiti  kuna unyanyasaji mkubwa wa ukatili wa jinsia hapa nchini kwani watoto wamekuwa wakibakwa, ndoa za utotoni kwa watoto wa kike na hata vipigo wanavyopata wanawake kutoka kwa waume zao ikiwa ni pamoja na kutelekezwa kwa watoto na wanawake hapa nchini.
Hali hiyo uwafanya , watoto na wanawake wengi kuathirika kisaikolojia na kutofikia malengo yao waliyokusudia kama vile kuendelea kielimu kutokana na ndoa za utotoni hali inayo ongeza unyanyasaji wawapo katika ndoa zao.
Kutokana na vitendo hivyo vya ukatili kuendelea kuripotiwa  kilasiku na vyombo mbalimbali vya habari hapa nchini hivi karibuni nililazimika kumtamfuta mkurugenzi mtendaji wa chama cha wanahabari wanawake Tanzania,tamwa bi Valerie Msoka  ili ni msikie anasemaje kuhusiana na vipigo wavyopata wanawake kutoka kwa waume zao ambapo alisema kuwa vitendo vya ukatili wa kijinsia vimeongezeka kwa wanawake kavile vipigo na vifo vinavyo tokana na wivu wa mapenzi.
Amesema jamii inapaswa ielimike na kutambua kwamba mapenzi sio kupigana bali mapenzi nikupendana hivyo amewashauri wanandoa kumaliza tofauti zao kwa njia ya amani na sikwavipigo.
“Jamani mapenzi sio kupigana mimi naamini mtu unaye mpenda huwezi kumpiga bali utamlinda kuhakikisha hapati madhara ” msoka anasema.
Aidha msoka amewashauri wazazi na walezi kuacha kuwa chagulia wachumba watoto wao,ikiwa ni pamoja na kuwaozesha watoto wakiwa na umri mdogo na badala yake wawape elimu ya kutosha  itakayowasaidia katika maisha yao na kuwawawezesha kujitambua pindi watakapo olewa.
Amesma watoto wengi wanao olewa na umri mdogo ndio wanao nyanyasika kwa kiasi kikubwa kwa sababu wengi wao hawatambui haki zao, hivyo kunaumuhimu wakuwapatia watoto wakike elimu kwani pia itawawezesha kujiinua kiuchumi na kuleta usawa wa kijinsia katika jamii na kupunguza dharau na kuleta heshima kwenye ndoa zao hii itachangia kwa kiasi kikubwa kupunguza vitendo vya ukatili wa kijinsia dhidi ya wanawake na watototo wa kike nchini.
Pia ameitaka serikali kuangalia upya sheria ya ndoa,sura ya 29 ya sheria za Tanzania pamoja na kwamba baadhi ya vifungu vya sheria hiyo inaelezea juu ya haki ya mke kumiliki mali katika ndoa na masuala ya mgawanyo wa mali endapo talaka itatolewa lakini baadhi ya vifungu vyake nikandamizi hasa pale inaporuhusu  wasichana wadogo kuolewa wakiwa  na umri wa miaka kuminanane na chini ya miamika kumi nanane  kwa ridhaa ya wazazi wake.
Amesema umri wa miaka kumi na nane  ni umri wa kuwa shule sasa sheria zikiruhusu umri huo msichana kuolewa inapelekea kumnyima mtoto wa kike haki yake ya msingi ya kupata elimu.
Hata hivyo ameongeza kuwa halikadhalika kuongezeka kwa maambukizi ya virusi vya ukimwi katika jamii kumeleta changamoto kubwa kwa matumizi ya baadhi ya ya vifungu vya sheria hii hasa vile vinavyo ruhusu ndoa za wasichana wadogo walio chini ya umri wa miaka  18, hivyo amewataka wajumbe wabunge maalumu la katiba kuiyangalia kwa maakini sheria hii ili tunapopata katiba mpya sheria hiyo kandamizi kwa wanawake iweimebadilika.
Watu wengi wamekuwa wakiishi katika ndoa hali ya kuwa wanamanyanyaso makubwa huku wakivumulia kwa sababu mbalimbali pengine kuepuka kuonekana wanaangaika kwa kuwa na huyu mara yule, au pengine mtu aliye nae anakuwa ameshapata nae watoto hivyo hataki kuwasumbua watoto wake au inawezekekana ugumu wa maisha pia unachangia kumfanya mwanamke avumulie kwa kuona ana pakwenda.
 Katika kuhakikisha kuwa vitendo vya unyanyasaji vinapungua  dhidi ya wanawake kituo cha msaada washeria kwa wanawake WLAC kilizindua kitabu cha sheria ya ndoa na talaka jijini Dar Es Salaam ilikumsaidia mwanamke kuijua sheria hiyo ili kumsaidia kutetea haki zake awapo katika ndoa.
Kwamujibu wa kifungu cha 9(1) cha sheria ya ndoa,sura ya 29 ya sheria za Tanzania,ndoa ni muungano wa hiari kati ya mwanamke na mwanaume unaokusudiwa kudumu kwa muda wa maisha yao yote hata hivyo mambo ya msingi yanapaswa kuzingatiwa  ikiwemo hiari,kudumu,jinsi tofauti pamoja na umri ili muungano huo uweze kukamilika kisheria.
Kwa mujibu wa sheria hii ya ndoa ni lazima nilazima watu wanaotaka kufunga ndoa wawe wametimiza miaka 18 au zaidi.Hatahivyo sheria hii inaruhusu mwanamke kuolewa akiwa chini ya umri wa miaka 18.
Kifungu cha 17 kinaeleza kwamba mwanamke ambaye hajatimiza miaka 18 anaweza kuolewa kwa idhini ya baba yake na kama baba amefariki basi mama, na ikiwa wote wamefariki basi idhini hiyo inaweza tolewa na mlezi wake.
Sehemu ya kitabu hicho kilichoandaliwa na WLAC  imesema kuruhusu wasichana kuolewa chini ya umri wa miaka 18 kunamnyima fursa  ya kuendelea  na elimu ikiwa ni pamoja na kuwaweka katika mazingira magumu ya kuhimili majukumu ya ndoa, hivyo kuhatarisha afya yao kwa kutokuwa na elimu ya uzazi.
Kwa kuzingatia mazingira ya sasa ya ukimwi wasichana hawa wadogo wanakuwa katika hatari zaidi ya kuambukizwa virusi vya ukimwi kutokana na uelewa wao mdogo na pia kutokuwa na nafasi  ya kutoa maamuzi juu ya miili yao.
Hivyo basi nivyema kwa wazazi na walezi wakatoa kipaumbele elimu na sio ndoa japo wanadai kuwa ndoa ni heshima lakini kwa mawazo yangu mimi naona ukimpatia elimu mtoto wa kike basi umemjengea maisha yake na heshima katika jamii pia, wakati umefika sasa wakuachana na mila potofu  zinazo mkandamiza mwanamke na kila mmoja kwa nafasi yake atumie uwezo aliyonao kwa kuelimisha na kumsaaidia mwanamke pamoja na jamii kwa ujumla kuhakikisha tunaondokana na mila kandamizi kama ndoa za utotoni,ukeketaji na mauaji ya vikongwe hapa nchini.
Pia ni vyema ukiona mtu anafanyiwa vitendo vya ukatili wakijinsia au wewe mwenyewe unafanyiwa vitendo hivyo basi usisite kutoa taarifa sehemu husika  ikiwemo polisi ili hatua za kisheria ziweze kuchukuliwa kwani kunabaadhi ushindwa kutoa taarifa pale wanapofanyiwa vitendo vya kikatili kwa madai ya kuona aibu hali ianayo rudisha nyuma mapambano dhidi ya vitendo vya kikatili nchini.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni