YESU NI JIBU

Jumapili, 19 Oktoba 2014

BAADA YA KUKAA KIMYA KWA MDA MREFU KWENYE UIMBAJI ANAKUJA KWA KISHINDO AKIWA NA UJUMBE WA NINA NDOTO YANGU SI MWINGINE MCHUNGAJI MWANSASU:

Mchungaji kiongozi wa huduma ya Hossana Life Mission Mchungaji Efrahim Mwansasu afunguka na kuweka wazi kwanini amekuwa kimya kwa mda mrefu,na sasa arudi kwa kishindo.
 Mchungaji Efrahim Mwansasu akiimba.
Watu hujiuliza na bila kupata majibu na kusema utawezaje kufanya mambo mawili kwa wakati mmoja ,ila wanashindwa kuelewa kanakwamba unapokuwa mchungaji lazima utafundisha na unapofundisha ili mtu akuelewe lazima uwe mbunifu na namna ya kutochosha waumini wako .

Mchungaji Mwansasu ana wito na kazi ya mungu hivyo ni lazima atumie kipaji chake ya kipekee kipaji cha uimbaji na anakitumia ipasavyo awapo madhabauni na baada ya kuona anakipawa cha uchungaji akaona si vyema kuacha kufanya kazi ya Mungu na awapo popote pale aachi kuimba na pia kuwa mchungaji ni vitu ambavyo mtumishi wa Mungu ni wajibu kutumia vitu hivyo kwa wakati mmoja .
 Aidha ieleweke wazi sio kambwa nipo kimya huwa kila muda na siku haipiti bila kuimba,na uimbaji wangu kutoa albamu pia sio  jambo la kuamka na kukurupuka na kukimbili studio ni jambo la kusema na Mungu nifanye nini katika hiki kipaji ulichonipa kwa ajili ya nchi yangu na mkoa wangu hata katika mataifa mengine.
Ni jambo la  kila mwimbaji kukaa na kutafakari unapotoka na unapokwenda na tujiulize kwa nini nyimbo za zamani hazipitwi na wakati za injili  na kizazi hiki nicha kumuomba Mungu sana kwani tumekuwa tukiimba bila kujua nini tunakifanya waimbaji wa injili tumejisahau na kusema ni utandawazi kumbe sivyo watu wamungu tunapaswa kuwa ,hivyo tuwe na upendo na kurudi chini na kumtumikia Mungu tusitafute pesa kwa kupoteza jamii katika maadili ya kumcha mungu ,bali tutafute kwanza ufalme na kumjengea Mungu.

Na safari hii nakuja kivingine huwa nina ndoto yangu ya maisha na ndiyo maana Mungu ananitunza, nyimbo zangu natamani sana Mungu anisaidie kwa kuangali na kuzitafakari ukisikiliza upate ujumbe na ni wakila mmoja wetu hivyo yakupasa kufanyia kazi.

Kipawa  ch uimbaji na uchungaji namshukuru Mungu kwa kutumia roho mtakatifu na kwa kunitumia,
 Mwaka 1998,Albamu yangu ya kwanza ilifahamika kwa jina la Tutatesa milele ikiwa na ujumbe wa kuwainua wacha Mungu na kuwataadharisha wanaopenda dunia waache na kumrudia mungu ikiwa na nyimbo nane .

Mwaka 2001 Albamu ya pili ,Umepoteza namba,inamaanisha mtu unaemtafuta Mume wa mtu au mke wa Mtu aache mara moja

Mwaka 2005 Albamu ya tatu Msigombane,Niliona ni kama kuna wakati tutagombana Viongozi wa dini katika huduma na katika dini ,upendo utatoweka katika madhehebu mbali mbali na viongoza wa dini na yametimia katika Mwaka 2013 Hadi sasa mfano makanisa kuchomwa moto mashehe kugombana amani inatoweka.

Mwaka 2010 Wosia wa baba .ninamaanisha kila unapoongea na  mzazi iwe mzazi wako au aliyekuzidi umri lazima anapokupa wosia usiupuuzie mzazi maadili yake huwa yanatokea.

Na safari hii kweli linatimia ukimuomba mungu Mwaka huu ninazindua Albamu yangu ya tano inakwenda kwa jina la Nina ndoto yangu Mabano I have a dream,namaanisha kila mtu ana ndoto yake duniani na zipo ndoto ndogo, ya kati, na kubwa,lakini wenye ndoto kubwa  wanamambo makubwa,na madogo ni madogo,hivyo mwenye ndoto lazima awe na maadui.
 Kipawa changu cha kuimba ni kutokana na mazingira ninayopita na Mungu hunitumia kwa kupitia uwezo wa Roho mtakatifu na hadi mimi mwenyewe najishangaa vinatoka wapi na mwisho wa siku vinatokea.

Kufanya mambo mawili kwa wakati mmoja ,uimbaji na mchungaji ni utaratibu unajiwekea ratiba yako tena unaweza kufanya zaidi kutokana na wewe mwenyewe unavyojiwekea utaratibu wako wa kazi ,na pia kuimba na kuubiri ni vitu vinavyoenda sambamba.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni