YESU NI JIBU

Ijumaa, 10 Oktoba 2014

MAOMBI YA UKOMBOZI NA UREJESHO-3

MGUSO WA PILI (SECOND TOUCH)

TOKA KATIKA KABURI LA DHAMBI,TABIRI JUU YA MAISHA YAKO UPATE KUSTAWISHWA
Neno la  Mungu linasema “Mkono wa Bwana ulikuwa juu yangu, naye akanichukua nje katika roho ya Bwana akaniweka chini katikati ya bonde nalo limejaa mifupa akanipitisha karibu nayo pande zote  na tazama  palikuwa na mifupa mingi katika ule uwanda! Nayo tazama ilikuwa mikavu sana.  Akaniambia mwanadamu, je! Mifupa hii yaweza kuishi? Nami nikajibu, Ee Bwana MUNGU wajua wewe.  Akaniambia tena, toa unabii juu ya mifupa hii uiambie  enyi mifupa mikavu  lisikieni neno la Bwana.  Bwana MUNGU aiambia mifupa hii maneno haya  tazama, nitatia pumzi ndani yenu nanyi mtaishi. Nami nitatia mishipa juu yenu nami nitaleta nyama iwe juu yenu na kuwafunika ngozi  na kutia pumzi ndani yenu nanyi mtaishi  nanyi mtajua ya kuwa mimi ndimi Bwana. Basi nikatoa unabii kama nilivyoamriwa hata nilipokuwa nikitoa unabii, palikuwa na mshindo mkuu na tazama tetemeko la nchi na ile mifupa ikasogeleana mfupa kwa mfupa mwenziwe. Nikatazama  kumbe! Kulikuwa na mishipa juu yake nyama ikatokea juu yake ngozi ikaifunika juu yake lakini haikuwamo pumzi ndani yake. Ndipo akaniambia tabiri, utabirie upepo, mwanadamu, ukauambie upepo, Bwana MUNGU asema hivi  njoo kutoka pande za pepo nne Ee pumzi, ukawapuzie hawa waliouawa wapate kuishi. Basi nikatabiri kama alivyoniamuru  pumzi ikawaingia  wakaishi  wakasimama kwa miguu yao  jeshi kubwa mno. Kisha akaniambia  mwanadamu, mifupa hii ni nyumba yote ya Israeli tazama wao husema, mifupa yetu imekauka matumaini yetu yametupotea  tumekatiliwa mbali kabisa. Basi tabiri uwaambie, Bwana MUNGU asema hivi tazama nitafunua makaburi yenu na kuwapandisha kutoka katika makaburi yenu enyi watu wangu nami nitawaingizeni katika nchi ya Israeli. Nanyi mtajua ya kuwa mimi ndimi Bwana, nitakapoyafunua makaburi yenu, na kuwatoa ninyi katika makaburi yenu enyi watu wangu. Nami nitatia roho yangu ndani yenu, nanyi mtaishi nami nitawawekeni katika nchi yenu nanyi mtajua ya kuwa mimi Bwana nimesema hayo na kuyatimiza asema Bwana” Ezekieli 37:1-14
MGUSO WA KWANZA.
Kama ambavyo neno la utangulizi linaonesha tafsiri mbili za kifo ambapo yaweza kuwa ni kifo cha kiroho ambacho mauti hupata mtu kwa jinsi ya roho japo kimwili anakuwa mzima na akiendelea vizuri na maisha yake ya kila siku. Mauti hii humpata mtu atendaye dhambi maana mshahara wa dhambi ni mauti sawa sawa na neno hili, “Kwa maana mshahara wa dhambi ni mauti bali karama ya Mungu ni uzima wa milele katika Kristo Yesu Bwana wetu.” Warumi 6:23
Yesu Kristo yeye ni mkombozi aliye hai na amekuja apate kumkomboa mwana wa Adamu toka katika mauti ya kiroho na kimwili na apate kuwa hai tena, maana yake  ni kuwa tukimwamini yeye kuwa ni BWANA  na mkombozi wa maisha yetu basi yeye anatuweka huru mbali na mateso na dhambi.
Lakini sasa mkiisha kuwekwa huru na kuwa mbali na dhambi na kufanywa watumwa wa Mungu mnayo faida yenu ndiyo kutakaswa na mwisho wake ni uzima wa milele.” Warumi 6:22.
Hivyo unapaswa kuokoka kwanza ndipo huruhusu Mungu akuguse kwa mguso wa pili na kukufungua katika vifungo vyote vinavyokuzunguka.
MGUSO WA PILI.
Mguso wa pili unaonesha dhahiri ya kuwa  hatuwezi kuendelea mbele huku tukiwafungua wale waliofungwa vifungo vya giza , magonjwa,madeni,dhiki na mateso kama wasipokuwabali mguso wa  kwanza wa ukombozi yaani kuokoka.
Hivyo kuokoka ni lazima maana ndilo tendo pekee la kiimani lenye kuleta nguvu ya Kimungu na ondoleo la dhambi kwa mwanadamu.
Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa mwanawe pekee ili kila mtu amwaminiye asipotee bali awe na uzima wa milele.” Yohana 3:16
Na neno linazidi kuthibitisha ya kuwa , “Bali mtu asiye haki Mungu amwambia una nini wewe kuitangaza sheria yangu na kuliweka agano langu kinywani mwako? Maana wewe umechukia maonyo na kuyatupa maneno yangu nyuma yako.Ulipomwona mwivi ulikuwaradhi naye, ukashirikiana na wazinzi. Umekiachia kinywa chako kinene mabaya na ulimi wako watunga hila.Umekaa na kumsengenya ndugu yako na mwana wa mama yako umemsingizia.Ndivyo ulivyofanya nami nikanyamaza ukadhani ya kuwa mimi ni kama wewe. Walakini nitakukemea nitayapanga hayo mbele ya macho yako.Yafahamuni hayo ninyi mnaomsahau Mungu nisije nikawararueni asipatikane mwenye kuwaponya. Atoaye dhabihu za kushukuru ndiye anayenitukuza. Naye autengenezaye mwenendo wake, nitamwonyesha wokovu wa Mungu.” Zaburi 50:16-23
Katika  Yesu tunaamini ya kuwa ndiye sadaka ya ukombozi kupitia damu yake iliyomwagika pale msalabani hivyo katika yeye tunapata uzima wa milele maana, “Na hilo alilinena ili kumjaribu kwa maana alijua mwenyewe atakalotenda.” Yohana 6:6
Lazima mtu ukubali kwanza kuzaliwa mara ya pili ndipo upate faida za ufalme wa Mungu katika Adamu wa kwanza tunakufa lakini  katika Adamu wa pili tunahuishwa upya.
Kuhuishwa ni kurejeshewa uzima na uhai maana Mungu atakulinda na kukuongoza sanjari na kukutenga na wale waovu,  Nikusanyieni wacha Mungu wangu Waliofanya agano nami kwa dhabihu.“Zaburi 50:5
Lakini dhambi ni uozo wa kimaadili unaopingana na kweli ya Mungu ndani mwa mwanadamu maana Adamu wa kwanza alipotenda dhambi , iliingia kwa wanadamu wote. Lakini neema ya Mungu na kipawa chake cha ukombozi kimefunuliwa kwetu kwa njia ya Yesu Kristo, ndio maana ni lazima mtu akubali mwenyewe kuokoka ndipo uponyaji unafuata, japo wengi wanataka kuombewa na kufunguliwa wakati dhambi zimejaa mioyoni mwao hapa panahitaji mtazamo sahihi kuhusu dhambi.
“Waovu hukimbia wasipofuatiwa na mtu, bali wenye haki ni wajasiri kama simba” Mithali 28:1
Lakini BWANA anasema, “Akusamehe maovu yako yote, akuponya magonjwa yako yote, aukomboa uhai wako na kaburi, akutia taji ya fadhili na rehema, Aushibisha mema uzee wako ujana wako ukarejezwa kama tai” Zaburi 103:3-5
Anaongeza kuwa,  Maana yeye aliye juu aliyetukuka, akaaye milele ambaye jina lake ni Mtakatifu asema hivi nakaa mimi mahali palipoinuka palipo patakatifu tena pamoja na yeye aliye na roho iliyotubu na kunyenyekea ili kuzifufua roho za wanyenyekevu na kuifufua mioyo yao waliotubu.” Isaya 57:15
Hivyo ni wazi kuwa toba inasababisha ufufuo wa kiroho na kimwili maana BWANA anaziangalia njia za kila mtu ili apate kumlipa sawa na njia zake, “Nimeziona njia zake nami nitamponya nitamwongoza pia, nitamrudishia faraja zake yeye na hao wanaomlilia.” Isaya 57:18
Mifupa mikavu lazima ipate kuishi. Lazima kutoka katika kaburi la dhambi,uzinzi na zinaa maana katika siku za leo hata wana ndoa wanashindwa kupeana haki zao za msingi hivyo kuwafanya wawe na  tamaa na kuangalia makahaba nah ii inasababishwa na kuruhusu hali ya dhambi iingie mioyoni mwao, “Kwa sababu wote wamefanya dhambi, na kupungukiwa na utukufu wa Mungu;” Warumi 3:23
Ni wazi kuwa peke yetu hatuwezi lazima tuhitaji msaada wa Mungu ili tujazwe nguvu za kuangusha kila ngome na kila fikra ziinukazo juu ya kinyume na matakwa ya Mungu.
Katika mguso huu wa pili lazima tutabiri  juu ya wote waliouwawa kiuchumi,kiroho na kimwili maana watarejeshewa tena kwa kufungua sanda zao zote za magonjwa,dhiki madeni,uchungu moyoni, utasa na ugumba visitawale  katika maisha ya wateule na hapa  tunapata nguvu ya ufufuo na uzima katika  Yesu Kristo.
Lakini, ikiwa Roho yake yeye aliyemfufua Yesu katika wafu anakaa ndani yenu, yeye aliyemfufua Kristo Yesu katika wafu ataihuisha na miili yenu iliyo katika hali ya kufa, kwa Roho wake anayekaa ndani yenu.” Warumi 8:11
Roho wa BWANA  Mungu yu juu yangu ili kuwagusa na kuwafungua wote waliofishwa na magonjwa katika miili yao wapokee uzima tele.
Na wale wenye dhiki katika maisha yao BWANA atayafunua sasa makaburi yote kwani hiki  ni kipindi cha baraka na ustawi.
Umepoteza matumaini  BWANA anasema usiogope maana, .....wao husema mifupa yetu imekauka matumaini yetu yametupotea tumekatiliwa mbali kabisa. Basi tabiri uwaambie Bwana MUNGU asema hivi tazama nitafunua makaburi yenu na kuwapandisha kutoka katika makaburi yenu enyi watu wangu nami nitawaingizeni katika nchi ya Israeli.  Nanyi mtajua ya kuwa mimi ndimi Bwana nitakapoyafunua makaburi yenu na kuwatoa ninyi katika makaburi yenu enyi watu wangu. Nami nitatia roho yangu ndani yenu nanyi mtaishi nami nitawawekeni katika nchi yenu nanyi mtajua ya kuwa mimi Bwana, nimesema hayo na kuyatimiza asema Bwana.” Ezekieli 37:11-14
Mguso wa pili ni nafasi nyingine ambayo BWANA ataitumia ili kufufua makaburi ya kichawi yaliyofunga mabinti wasiolewe na yaliyofunga ndoa za watakatifu zisiinuke tenana hakutakuwa na kufa wala kuzaa mapooza, “Watu wa mjini wakamwambia Elisha angalia twakusihi mahali pa mji huu ni pazuri, kama bwana wangu aonavyo lakini maji yake hayafai na nchi huzaa mapooza. Akasema nileteeni chombo kipya mtie chumvi ndani yake. Wakamletea.  Akatoka akaenda mpaka chemchemi ya maji akatupa ile chumvi humo ndani akasema Bwana asema hivi Nimeyaponya maji haya hakutatoka huko tena kufa wala kuzaa mapooza. Hivyo yale maji yakapona hata leo sawasawa na neno la Elisha alilolinena.” 2Wafalme 2:19-22
Miradi ya kuiuchumi na kazi za mikono zinafufuliwa maana, “Mlivyouzunguka mlima huu vyatosha geukeni upande wa kaskazini.” Kumbukumbu la Torati 2:3
Anawatia  moyo ya kuwa ,  Kwa sababu mkombozi wao ana nguvu; Atawatetea juu yako.”  Mithali 23:11
Naomba sasa kwa ajili yako uisikie sauti ya mwokozi Yesu iinuke kwenye vilio vyako vya maombolezo na minyonyoro iliyokufunga ifunguke sasa.“Naye Mungu wa amani atamseta Shetani chini ya miguu yenu upesi. Neema ya Bwana wetu Yesu Kristo na iwe pamoja nanyi. [Amina.]” Warumi 16:20
Usiogope wala kukata tamaa, “Umtwike Bwana mzigo wako naye atakutegemeza, hatamwacha mwenye haki aondoshwe milele”.Zaburi 55:22
Kwakuwa, “Dhabihu za Mungu ni roho iliyovunjika; Moyo uliovunjika na kupondeka, Ee Mungu, hutaudharau” .Zaburi 51:17
Na BWANA atatoa kilicho chema, “Naam, Bwana atatoa kilicho chema, na nchi yetu itatoa mazao yake” .Zaburi 85:12
Lakini Mungu anataka tukubali kwa mioyo yetu wenyewe, “ Kama mkikubali na kutii mtakula mema ya nchi bali kama mkikataa na kuasi mtaangamizwa kwa upanga maana kinywa cha Bwana kimenena haya” Isaya 1:19-20
Mapinduzi lazima yafanyike sasa katika ulimwengu wa roho upate baraka za rohoni na mwilini upate kuishwa tena kiroho, “Na uzuri wa Bwana, Mungu wetu, uwe juu yetu, Na kazi ya mikono yetu utufanyie thabiti naam kazi ya mikono yetu uithibitishe” Zaburi 90:17

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni