Hata hivyo watumishi wa Mungu wanafundisha na kufanya maombi
na maombezi kwa wale ambao wanakubali kumpokea Bwana Yesu kama Bwana na mwokozi
wa maisha yao.
Ama kweli hapo ujione jinsi alivyojidunga.
Katika mkoa wa Singida mwanachuo ambaye anasoma katika chuo cha uhasibu TIA mkoani
hapo aliamua kutaka kukatiza maisha yake kwa kile kinachodaiwa kuwa ni wivu wa
kimapenzi hata hivyo amenusurika kufa baada ya jaribio la kutaka kujiua
kwa kujikichoma kisu kushindikana.
Kiukweli ukichunguza kwa makini utaona kuwa nyuma yake
adui ameamua kutumia roho ya kujiua kwa lengo la kukatiza maisha ya binti Moza
kwa sababu ya kumfumania mpenzi wake Je ? ni kweli kwamba mwanadamu anaweza
kujidunga kisu ili kujiondoa duniani kwa sababu ya mpenzi na hata sio mume wala
ni vyema kutafakari kwa makini maana adui yeye kazi yake ni kuangamiza na kuua
yeye haoni uchungu wala hana huruma kwa mwanadamu.
Mwanachuo huyo ambaye amefahamika kwa jina moja la Moza ambaye ni mwanafunzi wa mwaka wa kwanza amefikia uamuzi huo baada ya mwanachuo huyo kumfumania mpenzi wake wa kiume akiwa na mwanamke mwingine.
picha kwa hisani ya Peruzibongo blog
TOA MAONI NA USHAURI WA KUWASAIDIA NA KUWAJENGA WANACHUO WASIWE KAMA HUYU,
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni