YESU NI JIBU

Ijumaa, 24 Oktoba 2014

HOFU,WASIWASI MASWALI JUU YA MCHEZAJI PETER BIAKSANGZUALA KUFARIKI DUNIA BAADA KUUMIA VIBAYA AKISHANGILIA BAO ALILOFUNGA:

Ligi ya Mizoram ikimuombolea mchezaji Peter Biaksangzuala 
 Unaweza kuwa na maswali mengi ,mshangao zaidi kuwaza sana kuwa inakuwaje,na ni kitu gani kinasababisha mchezaji kufa akiwa uwanjani ama akishangilia bao ambalo amefunga au lilofungwa na mwenzake.
Hivi karibu habari za kimichezo ambayo imetawala vyombo vya habari mbalimbali duniani ya mchezaji wa soka nchini India Peter Biaksangzuala kufariki baada kukimbizwa hospitalini kwa matibabu baasa ya kuanguka vibaya uwanjani akishangilia bao lake.
Kiukweli tunajifunza mengi kutokana na kifo cha mchezaji huyo kwani kuna mbinu za adui ya kuangamiza maisha ya wanadamu hasa wale maarufu kwani ukibahatika kupata kitabu kilichoandikwa na Emmanuel Agyarko kilichotafsiriwa na mchungaji Godwin Gunewe ukurasa wa kumi na tatu utajua kinachoendelea.
Mnamo mwaka 2003 kwa mujibu wa kitabu hicho mchezaji maarufu ambaye alijulikana kwa jina la Marc-Vivian Foe kutoka nchi ya Cameroon alifariki dunia uwanjani akiwa Ufaransa.
Kuna baadhi ya watu maarufu kujiunga na imani nyingine ili kupata nguvu na uwezo wa kuwa maarufu na wengine wanashindwa kutimiza masharti ambayo wamewekeana.
Ndugu msomaji ni shauku ya mwandishi na msimamizi wa blog hii kuwa makini sana na kusoma neno la Mungu(BIBLIA) ambayo ndiyo dira kamili katika maisha ya kiroho,na pia kuwasihi wacheza mpira na mashabiki wao kutafakari kwa makini.
Jitahidi kutafuta vitabu ambavyo vitakusaidia kujifunza yale yanayompendeza Mungu.
sasa endelea kupata kisa kilichotokea katika tibu Bethlehem Vengthlang FC.
 Mchezaji wa soka nchini India, Peter Biaksangzuala amefariki kutokana na majeraha aliyoyapata baada ya kuanguka vibaya uwanjani akisherehekea bao lake.
Mchezaji huyo alikuwa na umri wa miaka 23 na alijeruhi uti wake wa mgongo baada ya kupiga pindu uwanjani akisherehekea bao lake la kusawazisha kwa timu yake Bethlehem Vengthlang FC dhidi ya Chanmari West FC.
Biaksangzuala alikimbizwa hospitalini na kufanyiwa upasuaji lakini baadaye alifariki.
Taarifa kutoka kwa ligi hiyo kupitia kwa mtandao wa Facebook, ilisema : ''imekuwa siku yenye huzuni mkubwa kwa ligi ya Mizoram na kifo cha mchezaji wetu kimetushtua sana pamoja na wachezaji wenzake, wachezaji wa soka na mashabiki wa Mizoram. ''
"Peter alikuwa mchezaji mzuri na milizni mzuri sana, na pia alikuwa mchapa kazi.''
 Toa maoni  yako.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni