Kutana na mkurugenzi wa huduma ya Voice of Hope(VHM) mchungaji Peter Mitimngi kwa ajili ya ufafanuzi wa aina 12 za watu wasumbufu katika jamii na bila shaka nawe msomaji utajitathimini kuwa nawe upo kwenye kundi gani na hapa mchungaji Mitimingi ameandika kwa kufafanua.
Mchungaji
Peter Mitimingi, mkurugenzi wa huduma ya The Voice of Hope
Ministries (VHM).
|
AINA
YA PILI
MKUSANYA TAKATAKA (Mama PekuPeku) GABAGE COLLECTOR
MKUSANYA TAKATAKA (Mama PekuPeku) GABAGE COLLECTOR
1. Mtu huyu hujiweka katikati ya watu wasio sahihi na wenye hali za moyo zilizoharibika.
2.
Mtu huyu ni kama nyoka, mnyama mwenye sumu kali sana ambapo
akikugonga sumu yake huweza kuenea kwa kasi sana katika mwili wa
mwanadamu na kwa haraka.
3.
Mkusanya takataka ni mtu mzushi na muongo anayependa kusambaza uongo
na uzushi. Mambo asiyoyajua yalikotoka wala yanakokwenda.
Zaburi
52:3
Umependa mabaya kuliko mema, Na uongo kuliko kusema kweli.
Umependa mabaya kuliko mema, Na uongo kuliko kusema kweli.
4.
Kipaumbele chake cha kwanza ni kusengenya na kutapanya uongo na
uzushi wenye sumu kali ya kuangamiza na kugombanisha watu.
5.
Mara kwa mara hutumia muda mwingi kuzunguka zunguka kutafutiza
maneno ya uzushi,uongo na umbea na kuchonganisha watu.
Mithali
14:5
Shahidi mwaminifu hatasema uongo; Bali shahidi wa uongo, pumzi zake ni uongo.
Shahidi mwaminifu hatasema uongo; Bali shahidi wa uongo, pumzi zake ni uongo.
6.
Mbeba takataka (mama pekupeku)Hata Pumzi yake akipumua imejaa Uwongo
Mtupu.
7.
Siku zote huyasema madhaifu na mapungufu ya wengine, kamwe hawezi
kuyasema yale yanayo muhusu yeye.
8.
Hupata nguvu ya kuzungumza na kuyasema hayo maneno ya wengine wakati
ambapo mhusika anapokuwa hayupo. Mara mhusika akiingia kwa bahati
mbaya, basi maelezo yake huishia hapo hapo au hubadilisha mada kwa
ghafla na kujichekesha chekesha kwa muhusika aliyekuwa anamsengenya.
9.
Ni kama chura ambaye yupo majini hulia na kupiga kelele nyingi
lakini ukitupia jiwe moja tu, ananyamaza kimya kama vile hakuna
kelele. Ndivyo alivyo huyu mama peku peku.
10.
Hawezi kujisikia raha wala amani kama hajaongea uongo au mambo ya
uzushi. Kuzusha na kuongea maneno ya uongo kwake ndio burudani. Kama
hakuna hayo maneno yupo tayari hata kutembea umbali mrefu kwenda
kukusanya na kutafutiza umbea ili aweze kuusambaza.
Usoma aina ya kwanza kwa umakini sasa sehemu ya pili maana aina ya pili umeifahamu zaidi ya yote usikose aina ya tatu na kwa sasa umejitambua kuwa upo ama haupo kwenye kundi la aina ya kwanza na ya pili endelea kusoma ili kupata maelezo juu ya aina hizo zingine kumi zilizosalia
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni