MAKUNDI 4 MUHIMU YA MABADILIKO NA MAKUZI YA MTOTO!
Kwa mujibu watafiti wa saikolojia ya watoto kuna makundi manne ya muundo wa kimakuzi na kimaendeleo ya kiakili kwa mtoto
I. MWAKA 0 – 5
1. Mtoto kwenye kundi hili huwa na swali moja tu – NINI? What is this.
2. Hiki ni kipindi cha mtoto ku “register” vitu vya aina mbalimbali. Kumbuka kwamba mtoto ndiyo kwanza ameingia katika dunia hii na kila kitu anachokiona ni kigeni ndiyo maana katika umri huu mtoto anaswali moja tu Hii ni nini? What is this?
1. Mtoto kwenye kundi hili huwa na swali moja tu – NINI? What is this.
2. Hiki ni kipindi cha mtoto ku “register” vitu vya aina mbalimbali. Kumbuka kwamba mtoto ndiyo kwanza ameingia katika dunia hii na kila kitu anachokiona ni kigeni ndiyo maana katika umri huu mtoto anaswali moja tu Hii ni nini? What is this?
3. Wazazi wengina hufanya kosa kwa
kuona kero kumjibu mtoto mara kwa mara anapokuja kuuliza hii ni nini. Wakati
mwingine mtoto anaweza kuja kukuuliza swali hilo hilo kwa kitu kile kile mzazi
anakasirika maana anaona mbona tayari nilimjibu ananisumbua tena kwa hiyo
anamjibu vibaya au hamjibu kabisa.
4. Hiki ni kipindi ambacho mzazi
anatakiwa atumie mtindo wa KUTAWALA katika kumlea mtoto wake. Katika kipindi
hiki mzazi anatakia kutumia nguvu ya kutawala kumtengeneza (“shape”) mtoto
katika njia njema.
5. Mtoto katika kipindi hiki
asikuendeshe na kukutawala badala ya wewe kumtawala. Mfano mtoto analilia
kuchezea simu na ukimpa anaibonda bonda chini au kuitupia kwenye maji na
ukimkataza anaanza kulia basi ili anyamaze inabidi tu umpe hicho anacholilia
hata kama ni cha thamani. Kwa kufanya hivyo unalipeleka (forward) tatizo mbele
kwani atakapoingia kwenye kipindi cha pili utapata shida sana ya kuliondoa hilo
tatizo na litaendelea kukua.
Kuna siku atalilia umtungulie mwezi angani sasa sijui hapo utaazima ngazi wapi umpe kila anacho kililia.
Kuna siku atalilia umtungulie mwezi angani sasa sijui hapo utaazima ngazi wapi umpe kila anacho kililia.
II. MIAKA 6 – 9
1. Mtoto katika kundi hili swali lake kubwa huwa ni “HOW” INAKUWAJE.
1. Mtoto katika kundi hili swali lake kubwa huwa ni “HOW” INAKUWAJE.
2. Hiki ndio kipindi ambacho mtoto
hunyonya nguvu ya mahusiano kutoka kwa mzazi. Katika kipindi kilichopita yaani
miaka 0 -5 hata kama hakutakuwa na mahusiano ya kina sana haijalishi sana kwa
mtoto kwani ile misuri yake ya mahusiano huwa imekomaa kuanzia kipindi hiki.
3. Hiki ndio kipindi muhimu sana kwa
wazazi kuhakikisha kwamba wanaweka ratiba kabisa ya kujenga mahusiano na watoto
wao.
4. Hapa ndipo msingi wa ghorofa la
mahusiano unapochimbiwa. Mzazi akipuuzia kufanya kazi ya kuchimba msingi wa
mahusiano hapa kwa hakika itamgharimu kule mbele ya safari. Utajaribu kujenga
ghorofa kule mbele ya safari lakini litakuwa linadondoka kwasababu utakua
unajenga ghorofa juu ya ardhi ya mahusiano isiyo na msingi.
5. Usipojenga mahusiano mazuri na
yakaribu katika kipindi hiki, kuna baadhi ya tabia mbaya zitajengeka kwa watoto
na kuna wakati utakuwa unataka kuziondoa haitawezekana ndiyo wazazi wengine
wanachanganyikiwa kutokana na mambo yanayofanywa na watoto na kwa wakati huo
inakuwa haiwezekani tena kuwabadilisha.
6. Kutokana na mfumo wa kimaisha,
wazazi wengi wapo na mihangaiko ya (BIZE) kutafuta pesa hawana muda na watoto
wao kwaajili ya kuwambukiza joto la maadili mema. Mzazi hana muda na watoto
anakwenda kazini au biashara asubuhi na anarudi usiku na hata akirudi anakuwa
amechoka anapitiliza kulala au anaendelea na kazi zake hata akiwa nyumbani.
Anapoteza jambo la msingi sana ambalo litakuja kumgharimu mbele ya safari na
kwa bahati mbaya wengi huwa hawana uwezo wa kulipa hizo gharama kwani sio za
pesa wala mali ni gharama za mahusiano.
7. Wazazi wengi wanaliwa na “PEPO”
la maendeleo. Baadhi ya wazazi wanawapeleka shule za kulala “boarding” watoto
wao wadogo walio kwenye kundi hili. Wanafikiri ni maendeleo wanajionea fahari
mtoto anarudi anaongea kingereza. Mimi nakwambia mtoto atarudi anaongea
kingereza lakini atarudi pia na roho za ushoga na usagaji na madudu mengine
kwani utafiti unaonyesa watoto wengi waliwekwa mbali na wazazi wao na kuishi
kwenye mazingira kama hayo hupata nafasi kubwa ya kujifunza mambo kama hayo ambayo
huwachukua muda mrefu sana kuja kuwa toka na wengine huendelea nayo mpaka
wanakuwa watu wazima bila hata mzazi kuweza kugundua kwani hufanya siri sana.
Mimi binafsi nimefanya ushauri “counseling” ya vijana wengi mashoga, wasagaji
na wengi wao husema walijifunzia shule za bording wakiwa katika umri huu.
8. Baadhi ya wafanya kazi wa ndani
pia huchangia kuwafundisha tabia mbaya watoto wadogo katika kundi hili. Kama
mzazi hatakuwa na mahusiano ya karibu na mtoto hataweza kugundua kabisa
kinachoendelea nyuma ya pazia katika maisha ya mtoto.
III. MIAKA 10 – 14
1. Mtoto katika kundi hili swali lake kubwa huwa ni WHY? KWANINI?
1. Mtoto katika kundi hili swali lake kubwa huwa ni WHY? KWANINI?
2. Hiki ni kipindi ambacho misuli ya
kichwa cha mtoto imeanza kukomaa na kuweza kufikiri kwa kina zaidi.
3. Hiki ni kipindi ambacho mzazi
anahitajika kuwa na sababu mkononi.
4. Unapomwambia mtoto usifanye 1, 2,
3 kwa upande wa pili mzazi anatakiwa awe za sababu kwanini anamwambia mtoto
asifanye hivi na hivi. Au ukimwambia mtoto nataka ufanye hivi na hivi hakikisha
unasababu mkononi kwanini unamtaka mtoto afanye hivyo.
5. Ukifanya hivyo mtoto atafanya
jambo kwa moyo ana kiwango cha kukuheshimu na kukupenda kitaongezeka.
6. Ni vema mzazi ukajua kwamba hiki
ni kipindi ambacho mtoto huwa makini sana “very sensitive” kuliko kipindi
kingine na hujisikia kufanya jambo kwa kujiamini akiwa anajua sababu zake.
7. Hiki sio kipindi cha kutumia
nguvu kwamba nimesema kama mzazi fanya hivi na sitaki maswali maswali hiyo
itakuwa ni kubomoa badala ya kujenga hasa kwa siku za usoni katika maisha ya
mtoto.
MIAKA 15 – 17
1. Hiki huwa ni kipindi kigumu sana kwa wazazi walio wengi sana. Kipindi hiki huwa kigumu zaidi kwa mzazi hasa kama hatua hizo hapo juu hukufanya vizuri.
1. Hiki huwa ni kipindi kigumu sana kwa wazazi walio wengi sana. Kipindi hiki huwa kigumu zaidi kwa mzazi hasa kama hatua hizo hapo juu hukufanya vizuri.
2. Baadhi ya wazazi hupuuzia hatua
hizo hapo juu hatua ya 1 hatua 2 na hatua 3. Wanapofika hatua ya 4 wanagundua
kwamba kunakitu hawakufanya wakati mtoto anakua na sasa ndiyo wanakurupuka
kutaka kumrekebisha mtoto na kumfundisha maadili mema tayari umechelewa. Ndio
maana nilisema usipozingatia zile hatua za awali ukifika hatua ya 4 utalipa
gharama.
3. Mtoto katika kundi hili swali
lake kubwa huwa WHAT IS THIS, I WANT TO TRY. Hujiuliza HII NI NINI, NATAKA
KUJARIBU.
4. Hiki ndio kipindi ambacho
chochote ukimwambia mtoto usifanye hivi na hivi katika kipindi hiki, ndio kama
kumtuma kufanya hicho unachomkataza.
5. Mzazi ukikurupuka na kuanza
kumfundisha mtoto katika kundi hili kwamba tendo la ndoa sio zuri kwa watoto
subiri mpaka utakapokuwa mtu mzima. Basi ujue hapo ndio kama umemchochea
kujiuliza zaidi hivi hili tendo la ndoa ni nini? Nataka kujaribu.
6. Hiki ndio kipindi ambacho watoto
hutaka kujaribu kila kitu hata vile ambavyo wameambiwa au wamekuwa wakisikia
kuwa ni hatari.
7. Hapo ndipo watoto hutaka kujaribu
vitu kama sigara, bangi, tendo la ndoa, madawa ya kulevya n.k
NAMALIZIA KWA KUSEMA KILA MZAZI
ACHUKUE JUKUMU LAKE KIKAMILIFU KULEA MTOTO SIO KAZI YA “by theway”
Ndugu msomaji ni jukumu lako kuamua kufanyia kazi haya yote ambayo umeletewa na mwalimu na mchungaji Peter Mitimingi mkurugenzi wa VHM sasa usipofanyia kazi nani wa kumlaumu mwanao akiharibikiwa,bila shaka utajilaumu mwenyewe na utabeba lawama hizo mwenyewe.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni