Wanawake washindwa kuzuia na kuficha hisia zao kwa mapadre na kuamua kuweka bayana kuwa ni vyema nao wakapata kibali cha kuoa.
Haya yametokea bada ya wanawake zaidi ya 26 kutaka kuwa na mahusiano na mapadri kitu ambacho hakijawaki kuwepo sasa wao wameona kuwa ni vyema wapewe ruhusa ya kuoa.
Papa Francis kiongozi wa kanisa
katoliki.
Kundi moja la wanawake walio na
hisia za kimapenzi na mapadre wa kikatoliki wamemuandikia barua kiongozi wa
kanisa katoliki duniani Papa Francis ya kumtaka kubadilisha sheria za kanisa
hilo zinazowazuia viongozi hao wa dini kuoa.
Wanawake hao 26 kutoka Italy na
maeneo mengine wanasema kwamba wamekuwa wakishiriki ama wanataka kushiriki
katika uhusiano wa kimapenzi na mapadre na kwamba wametoa ombi hilo kwa niaba
ya wanawake wengine ambao wako katika hali kama hiyo.
Barua hiyo inazungumzia kuhusu
uchungu wa kushindwa kuishi maisha yao kikamilifu mbali na kutaka kukutana na
papa Francis.
Papa Francis amekuwa akiunga mkono
utamaduni wa useja,lakini mwaka 2010 aliandika akisema kuwa huenda msimamo wake
ukabadilika.
Papa francis amekuwa akimtembelea
mjane wa aliyekuwa kasisi Jeronimo Podesta ambaye alijiuzulu katika utumishi
wake na kuoa, zaidi ya miaka 40 iliopita.
sasa nawe msomaji unasemaje kuhusu ssakata hilo unaweza ukatoa maoni yako.
habari chanzo BBC.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni