Siku ya jumapili iliyoisha katika uwanja wa mpira wa Uhuru
zamani kama uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam, kulifanyika tamasha kubwa la
uimbaji lenye lengo la kuzungumza kupitia uimbaji na atakayekuwa Rais mtarajiwa
wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Tamasha hilo liliandaliwa
na kwaya ya Efatha kutoka Uhuru Moravian Kariakoo na kuhudhuriwa na watu
mbalimbali pia kwaya hiyo ilitumia wasaa wa tamasha hilo kufanya live Recording yao
Baadhi ya kwaya
zilizohudhuria tamasha hilo ni pamoja na Neema Gospel ya AIC Chang'ombe,
Uinjilisti Kijitonyama, Eden Tabata Moravian, Uinjilisti Sayuni Kinondoni,
Tumaini Shangilieni St James Arusha. Ambapo licha ya mahudhurio kutokuwa
makubwa sana kama ilivyokuwa ikitazamiwa lakini watu waliofika waliweza
kuburudika na lengo la tamasha hilo kufikiwa na vyombo vilivyotumika kutoleta
shida kama matamasha mengi yanayofanyika uwanja wa taifa.
Baadhi ya watumishi amabo wamehudhuria katika Tamasha hilo.
Source;www.gospelkitaa.co.tz
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni