Kwa
mujibu wa wakfu wake, Tutu alikuwa akiugua maambukizi yaliyokuwa yamemkumba kwa
mara kadhaa.
Mshindi
huyo wa tuzo ya amani ya nobel mwenye umri wa miaka 83, amekuwa na matatizo ya
kiafya katika miezi ya hivi karibuni.
Hivi
majuzi alilazwa hospitalini kutokana na maambukizi yaliyosababishwa na saratani
ya tezi dume aliyokuwa akiugua.
Askofu
tutu alistaafu rasmi mwaka wa 2011, lakini bado angali anasafiri kwa shughuli
mbali mbali.
Taarifa
iliyotolewa na wakfu wake ilisema kuwa Askofu huyo mstaafu amewashukuru
wafanyakazi wa hospitali ya Cape Town kwa kumhudumia vyema.
Aidha
alitoa shukrani kwa raia wa nchi hiyo kwa kumkumbuka kwa maombi yao na risala
za heri njema.
chanzo BBC
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni