YESU NI JIBU

Jumapili, 27 Septemba 2015

ASKOFU RASMI ATANGAZWA NA KIWANGO CHA KURA HUKO DODOMA NA MSIMAMIZI WA UCHAGUZI ASKOFU BATENZI.

 Mshauri mkuu wa kanisa la EAGT mchungaji Anyandile Mwakisyala. 
Na Mwandishi Yonathan Landa
DODOMA.
Hatimaye kitendawili cha Nani kuvaa Viatu vya Askofu Moses Kulola kimeteguliwa leo na Mkutano Mkuu taifa uliotishwa kwa mujibu wa Katiba ya kanisa la Evangelistic Assemblies Of Tanzania hii leo.
Katika Mkutano huo uliokidhi vigezo vya kikatiba umechagua viongozi watakaongoza kanisa hilo kwa muda wa miaka mitano tangu sasa.

 Mmoja wa wachungaji akihesabu kura

Nafasi ya Askofu mkuu iliyokuwa inakaimiwa na Makamu wa Askofu wa Kanisa ndugu Asumwisye Mwaisabila sasa nafasi hiyo amepata mrithi halali wa kupigiwa kura kwa mujibu wa Katiba ambaye ni Mchungaji Brown Mwakipesile aliyeshinda kwa kura 1526 dhidi ya Mchungaji John Mahene alipata kura 726.
Ikumbukwe kuwa Mwakipesile kabla Nafasi hiyo alikuwa ndiye Katibu Mkuu wa Kanisa hilo kwa kipindi kirefu sasa.
Nafasi ya Makamu wa Askofu imeshikiliwa na Mchungaji John Mahene alipata kura 1490 dhidi ya Mpinzani wake Leonard Mwizarubi aliyepata kura 563.


Aidha Nafasi ya Katibu wa Kanisa hilo imechukuliwa na Leonard Mwizarubi kwa ushindi wa kura 1408 dhidi ya Mchungaji Raphael Machimu aliyepata kura 416.

Vilevile nafasi ya mtunza Hazina wa kanisa hilo imekwenda  Kwa Mchungaji Pray-God Mgonja ambaye ameshinda kwa kura 1011 na kumuangusha kwa mbali aliyekuwa anashikilia nafasi hiyo Mchungaji Joshua Wawa kwa kupata kura 566.

Wakati huohuo Mkutano Mkuu kwa pamoja walimpitisha Mshauri Mkuu wa Kanisa hilo ndugu Anyandwile Mwakisyala pasipo kupingwa na mjumbe yeyote kwa kura ya ndiyo kuwa mshauri wao.
Uchaguzi huo uliongozwa na Kamati Maalumu ya PCPT chini ya Mkuu wa kanisa la FPCT Taifa Askofu Batenzi.


 Mshauri mkuu wa kanisa la EAGT mchungaji Anyandile Mwakisyala mwenye kinasa sauti akimpongeza Askofu Leornard Mwizarubi baada ya uchaguzi.


 Picha ya pamoja kati ya viongozi wapya wa kanisa la EAGT na mshauri mkuu.
Wasiliana nasi 0752834514,

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni