YESU NI JIBU

Jumanne, 22 Septemba 2015

DAWA YA KUPUNGUZA MAKALI YA UKIMWI TEMBE MOJA KUTOKA DOLA $13.50 HADI $750.

Kampuni moja ya kutengeza madawa imelazimika kujitetea vikali baada ya kupandisha gharama ya dawa ya Ukimwi kwa asilimia 5,000.
Hii inamaanisha kuwa bei ya tembe moja ya dawa inayotumika kupunguza makali ya ukimwi itapanda kutoka dola $13.50 hadi $750.
Kampuni hiyo inayoitwa Turing Pharmaceuticals imelaumiwa na washika dau wa maswala ya Ukimwi kwa kuongeza bei ya dawa hiyo ya Daraprim ambayo imekuwa mstari wa mbele katika kuimarisha uwezo wa mwili wa mgonjwa aliyeathirika kupigana na maambukizi mapya.
Turing Pharmaceuticals ilinunua hati miliki ya dawa hiyo ya Daraprim mwezi uliopita Agosti.
Mkurugenzi mkuu wa kampuni hiyo Martin Shkreli amenukuliwa akisema kuwa faida itakapatikana baada ya mauzo ya dawa hiyo itasaidia kugharamia utafiti wa dawa mpya na zenye ubora zaidi.
Tembe moja ya dawa hiyo ya Daraprim inagharimu dola moja pekee kutengeneza.
Hata hivyo bwana Martin Shkreli anasema kuwa bei hiyo haijumuishi gharama ya kunadi dawa hiyo wala usambazaji wake ilihali gharama imeimarika maradufu katika miaka ya hivi punde.
''Katika siku za hivi punde dawa za kupunguza makali ya saratani zinagharimu dola laki moja (100,000) ilhali gharama yake asili inaweza kugharimu dola nusu milioni.
Daraprim inauzwa kwa bei nafuu zaidi ikilinganishwa na dawa zinazotibu magonjwa sawa.
Shkreli aliiambia runinga ya Bloomberg katika mahojiano ya kibinafsi.
Shkreli alimsuta mwandishi mmoja wa habari kupitia mtandao wa Kijamii akimuita kuwa ''mjinga'' kwa kutaka kujua kwanini kampuni yake ilikuwa inaongeza maradufu bei ya dawa hiyo muhimu katika vita dhidi ya Ukimwi haswa katika mataifa maskini duniani.
 Daktari Wendy Armstrong kutoka muungano wa wauguzi nchini Marekani HIV Medicine Association amekashifu sababu zilizotolewa kwaajili ya nyongeza hiyo kubwa ya bei ya dawa hiyo.
Muaniaji tikiti cha urais wa chama cha Democratic Hillary Clinton ameonya kuwa serikali yake itachukua hatua kali dhidi ya makampuni yanayofaidi kutokana na msiba wa watu kwa kupandisha bei ya madawa maalum.
Source BBC.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni