YESU NI JIBU

Alhamisi, 17 Septemba 2015

MAPINDUZI YA KIJESHI YAFANYIKA HUKO BURKINA FASSO

Yametokea mapinduzi nchini  Burkina Fasso, Afrika Magharibi ambako jeshi limevunja serikali ya mpito ya nchi hiyo na kutwaa madaraka.
 Kwa mujibu wa afisa mmoja wa jeshi aliyezungumza kwenye runinga ya nchi hiyo, Rais wa mpito Bwana MICHEL KAAFANDO amepokonywa madaraka bila kutoa maelezo zaidi.
Hatua hiyo imekuja baada ya Bwana KAFANDO na Waziri Mkuu wake Bwana ISAAC  ZIDA na baadhi ya mawaziri kukamatwa wakati kikao cha baraza la mawaziri na wanajeshi watiifu wa wa zamani, Bwana BLAISE COMPAORE aliyejiuzulu mwaka jana kufuatia maandamano dhidi yake.

Kukamatwa kwao kumelaaniwa vikali ndani na nje, huku jumuiya ya kimataifa kupitia Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa,  Bwana BAN KI-MOON,  ukitaka waachiliwe mara moja na Marekani imelaani jaribio lolote la kutwaa madaraka kinyume na katiba au kuondoa tofauti za siasa kwa kutumia jeshi.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni