Lakini
baadhi ya viongozi wa dini wameambia mwandishi wa BBC Leonard Mubali kuwa
huenda ni matokeo ya uhasama wa kidini.
Kuchomwa
kwa makanisa hayo kumeongeza hofu kwa viongozi wa makanisa na waumini kuhusu
usalama wao.
Mchungaji
Vedasto Athanasi ni Askofu wa kanisa la Living Water mkoani humo, ambaye kanisa
lake limechomwa kwa mara ya tatu sasa, ni mmoja wa walioingiwa na wasiwasi.
“Kitendo
hakiwezi kukafanyika mara tatu, na hakuna hatua zinazochukuliwa. Naona
ufuatiliaji wa suala hili ni mdogo sana,” amesema.
Mkuu
wa mkoa wa Kagera, John Mongela, ameiambia BBC kuwa mazingira ya matukio hayo
yana utata kiasi kwamba ni vigumu kutambua mara moja kuwa yana malengo gani.
”Kwa
jinsi ambavyo tuliona, hupati shida ya moja kwa moja, ujue kama ni siasa au ni
nini. Kwa sababu haya yanafanyika wakati hakuna watu,” amesema.
”Lolote
lile ambalo litakuja upande wetu, tutalifanyia kazi na kuona kama litatusaidia
katika kutuelekeza.”
Crodward
Edward, mwenyekiti wa muungano wa makanisa ya Kipentekoste mkoani Kagera,
anasema anaridhishwa na hatua za mamlaka za usalama na kuwataka waumini kuwa
watulivu kipindi hiki cha matukio haya.
Je wewe una maoni yako?
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni