Karani mmoja
anayefanya kazi serikalini, amefungwa jela nchini Marekani kwa kukataa kutoa
vyeti vya ndoa kwa watu wa jinsia moja.
Karani huyo,
Kim Davis, anayefanya kazi kwenye jimbo la Kentucky, amesema hawezi kuruhusu
watu wa jinsia moja kuoana, kwani hilo linakwenda kinyume na imani yake ya
Kikristo.
Jaji
aliyesimamia kesi ya Kim Davis amesema mshtakiwa amekiuka sheria ya Marekani
ambayo sasa inaruhusu watu wa jinsia moja katika majimbo yote kufunga ndoa.
Aidha, jaji
huyo amewataka wasaidizi wa Davis waahidi kwamba watatoa leseni za kufungisha
watu ndoa, hata kama ni wa jinsia moja.
Ikulu ya
Marekani imeunga mkono uamuzi wa mahakama, ikisema hakuna mtu aliye juu ya
sheria.
Sheria ya
kuhalalisha ndoa za watu wa jinsia moja ilipitishwa miezi miwili iliyopita.
chanzo ni DW.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni