Imeelezwa
kuwa ni vyema watu kusimama na
kumtumikia Mungu na kufuata taratibu na miongozo ya Kimungu ili waweze
kuondokana na mateso ,taabu na shida mbalimbali zinazo wakumba katika maisha ya
kila siku.
Wito huo
umetolewa na mtumishi wa MUNGU mchungaji Paul Kaisi wa huduma ya Liko Tumaini
Kwa Mungu ilipo katika Viwanja vya sifa za Yesu Manzese jijini DSM.
Ametoa wito
huo wakati akifundisha neno la MUNGU na kusema watu wenye matatizo mbalimbali
na kufungwa na dhambi kujitokeza kuhudhuria ibada hiyo kwa lengo la kufunguliwa
na kuacha dhambi.
Aidha
alisema kuwa watu wengi wamefungwa bila kujua na adui hivyo ni muhimu kuhudhuria
ibada hiyo ya kufunguliwa siku ya jumapili hii kuanzia saa tatu kamili na
kuendelea na maombi na maombezi yatafanyika kwa kila atakayehudhuria.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni