YESU NI JIBU

Jumatatu, 15 Septemba 2014

MAOMBI YA UKOMBOZI NA UREJESHO MGUSO WA PILI (THE SECOND TOUCH)



KILA JENEZA LILILOBEBA MAISHA NA USTAWI WA WATU WA MUNGU NDANI MWAKE,LITAWAREJESHEA UHAI TENA.
Neno la Mungu linasema, “Baadaye kidogo alikwenda mpaka mji mmoja uitwao Naini, na wanafunzi wake walifuatana naye pamoja na mkutano mkubwa. Na alipolikaribia lango la mji, hapo palikuwa na maiti anachukuliwa nje ni mwana pekee wa mamaye ambaye ni mjane, na watu wa mjini wengi walikuwa pamoja naye. Bwana alipomwona alimwonea huruma, akamwambia, Usilie. Akakaribia, akaligusa jeneza wale waliokuwa wakilichukua wakasimama. Akasema, kijana nakuambia,  inuka. Yule maiti akainuka akaketi akaanza kusema. Akampa mama yake. Hofu ikawashika wote wakamtukuza Mungu, wakisema, Nabii mkuu ametokea kwetu na Mungu amewaangalia watu wake.  Habari hii yake ikaenea katika Uyahudi wote, na katika nchi zote za kando kando”   Luka 7:11-17
Kwa kila jambo kuna majira yake na wakati kwa kila kusudi chini ya mbingu hivyo kuna wakati wa kuzaliwa na wakati wa kufa, kuna wakati wa kulia na wakati wa kucheka ,kuna wakati kubomoa na wakati wa kujenga tena, kuna wakati wa kushushwa chini vilevile kuna  wakati wa kuinuliwa.
Hivyo napenda utambue juu ya nyakati hizi za kiimani ambazo lazima tuzipitie katika maisha yetu ya kimungu aliye hai  na ndizo zitakazosimama katika maisha yetu daima.
Tambua ya kuwa katika kila kusudi la kimungu kuna mguso wa pili nasi kwa imani  katika  Yesu kristo  tunakwenda kuguswa tena katika mguso wa pili na kila kilichokufa kitafufuka tena, aliyefungwa atafunguliwa tena na biashara iliyondani ya jeneza itatoka tena.

MGUSO  WA KWANZA:
Katika mguso wa kwanza Bwana Yesu Kristo anaingia katika mji uitwao  Naini lakini alipokaribia lango la mji anakutana na watu wenye msiba wa kufiwa na mpendwa wao.
 Pamoja na msiba huo wapo wengine walikuwana msiba magonjwa, madeni na pia uchungu mioyoni mwao.
Msiba huu unatokana na sababu ya kuwa kila walichokuwa wakijaribu kukifanya kinakufa kwa kuzaa mapooza hivyo BWANA alipomwona yule mama aliyefiwa, akamwonea huruma  na akamwambia asilie.
Akakaribia, akaligusa jeneza wale waliokuwa wakilichukua wakasimama.
Huu  ndio mguso wa kwanza ambapo kijana aliyekufa na kubebwa na watu ndani ya jeneza  na wakiwa njiani walikutana na Yesu langoni na akaligusa jeneza.
Swali la kujiuliza Kwanini Yesu aligusa jeneza?, jibu lake ni hili , jeneza ndicho kizuizi cha kwanza kinachomfanya aliye kufa asiguswe moja kwa moja na Yesu Kristo ili apokee muujiza.
Hii ndio maana ya jeneza,Tazama mkono wa Bwana haukupunguka hata usiweze kuokoa wala sikio lake si zito hata lisiweze kusikia lakini maovu yenu yamewafarikisha ninyi na Mungu wenu, na dhambi zenu zimeuficha uso wake msiuone, hata hataki kusikia.” Isaya 59:1-2
Neno hili linatudhihirishia ni nini maana ya jeneza ,ambapo ni dhambi na uovu ambazo humziba  mtu wa Mungu asiguswe na Yesu Kristo.
Wapo watu wengi ambao ni wakristo lakini wamo kwenye majeneza ya ulevi, uzinzi,uongo, dhuluma , fitina na mambo yote yanayofanana na hayo , elewa ya kuwa majeneza  hayo ni mazito na lazima yakutane na Yesu Kristo katika mguso wa kwanza ili ayasimamishe yasiendelee na safari ya kwenda makubirini maana mshahara wa dhambi ni mauti.
Kwa maana mshahara wa dhambi ni mauti, bali karama ya Mungu ni uzima wa milele katika Kristo Yesu Bwana wetu.” Warumi 6:23
Mkristo lazima uache kutenda dhambi maana huwezi kuendelea kufanya dhambi na ukataka kuona baraka za Mungu , fahamu ya kuwa Mungu hadhihakiwi na apandacho mtu ndicho atakachovuna.
Msidanganyike Mungu hadhihakiwi kwa kuwa cho chote apandacho mtu ndicho atakachovuna. Maana yeye apandaye kwa mwili wake katika mwili wake atavuna uharibifu bali yeye apandaye kwa Roho katika Roho atavuna uzima wa milele.” Wagalatia 6:7-8
Hivyo yakupasa usidanganyike ya kuwa unaweza kuwa na maisha ya dhambi ndani mwa kanisa na bado ukapata baraka katika maisha yako, tambua ya kuwa  hakuna atakayemwona Mungu katika maisha yake ya sasa na ya baadaye asipokuwa na huo utakatifu
Tafuteni kwa bidii kuwa na amani na watu wote, na huo utakatifu ambao hapana mtu atakayemwona Bwana asipokuwa nao;” Waebrania 12:14
Hivyo huu ni wakati wako wa kuacha dhambi na kuokoka,“Kwa maana atakaye kupenda maisha na kuona siku njema auzuie ulimi wake usinene mabaya, na midomo yake isiseme hila. Na aache mabaya atende mema  atafute amani, aifuate sana. Kwa kuwa macho ya Bwana huwaelekea wenye haki, na masikio yake husikiliza maombi yao bali uso wa Bwana ni juu ya watenda mabaya.” 1Petro 3:10-12
Hivyo kwa maneno haya ni wazi kuwa katika mguso wa kwanza ndipo tunapookoka na kuanza maisha mapya ya kimaombi. Hivyo zingatia kweli hii ya kuwa afichaye dhambi hatafanikiwa hata kama ana mipango ya mafanikio  bali yule aziungamaye atapata rehema.
Afichaye dhambi zake hatafanikiwa bali yeye aziungamaye na kuziacha atapata rehema.” Mithali 28:13.

Na hapa msomaji wangu endelea kufuatilia sehemu ya  
                        MGUSO WA PILI:
Yesu alipoona ya kuwa waliobeba jeneza lenye mwili wa kijana yule aliyekuwa amekufa wamesimamisha safari yao ndipo alipoligusa jeneza na kusema ,“..... Akasema kijana nakuambia Inuka.Yule maiti akainuka akaketi  akaanza kusema. Akampa mama yake.” Luka 7:14-15
 Katika mguso huu wa pili tunaona muujiza wa kuinuka mara ya pili kutoka katika kifo maana aliyekuwa amekufa amerejeshewa uzima na Yesu Kristo  na ndipo alipoinuka  tena kwani  kilimchofanya kijana awekwe kwenye jeneza ilikuwa ni nguvu ya mauti.
Mauti ni nguvu ya kufisha ambapo Yesu Kristo anasema “Na aliye hai nami nalikuwa nimekufa na tazama ni hai hata milele na milele. Nami ninazo funguo za mauti na za kuzimu” Ufunuo 1:18
Inawezekana katika mguso wa kwanza umeumia lakini fahamu ya kuwa upo mguso wa pili wenye uwezo wa kimungu wa kukufungua na kukuondoa katika bonde la vilio.
Huu ni wakati wa kutoka katika bonde la vilio kwa kuamishwa na Yesu Kristo toka kwenye umasikini na taabu, hivyo ni lazima uamishwe sasa kiroho na kimwili maana “Naye alituokoa katika nguvu za giza akatuhamisha na kutuingiza katika ufalme wa Mwana wa pendo lake;” Wakolosai 1:13
Naye Yesu Kristo alituokoa toka katika nguvu za mauti,magonjwa,madeni,mapepo,uchawi,utasa na mateso mbalimbali na pia alituhamisha kutoka katika jeneza la mauti,magonjwa na madeni na kutuingiza katika ufalme mwana wa pendo lake, baraka na ustawi,uponyaji na uzima na pamoja na kustawishwa kiuchumi na kifedha.
Maana BWANA  atageuza bonde la vilio kuwa bonde la baraka,”Wakipita kati ya bonde la vilio hulifanya kuwa chemchemi naam mvua ya vuli hulivika baraka”Zaburi 84:6
BWANA anageuza  na hata sasa ageuze  maisha yako wewe na watoto wako na alete baraka na ustawi katika maisha yenu.
Kama ambavyo aliweza kugeuza mauti ya kijana ikawa uzima na sasa atageuza ndoa zilizokufa ziinuke tena ,elimu zilizokufa ziinuke tena,kazi zilizokufa ziinuke a na zipate uzima tele.
Pia atageuza magonjwa yote yatoke kwako na upate uzima na mkono wake Kristo ukae thabiti katika maisha yako ya kiroho na kimwili sawasawa ” Ambaye mkono wangu utakuwa thabiti kwake, Na mkono wangu utamtia nguvu.,Adui hatamwonea, Wala mwana wa uovu hatamtesa.Bali nitawaponda watesi wake mbele yake, Nitawapiga wanaomchukia.” Zaburi 89:21-23
Katika mguso wa pili mkono wake Kristo utakugusa na utakuwa thabiti kwako na mkono wake utakuletea nguvu ya kupata utajiri na heshima “Bali utamkumbuka Bwana, Mungu wako, maana ndiye akupaye nguvu za kupata utajiri; ili alifanye imara agano lake alilowapa baba zako, kama hivi leo.” Kumbukumbu 8:18
BWANA anapotupa ukombozi sharti aturejeshee tena uwezo na nguvu ili  tupate kutawala kimwili na adui zako hawatakuonea tena wala mwana wa uovu yaani wachawi na waganga ,wafunga majini na awarusha mikosi hawatakupata tena.
BWANA anasema hawatakutesa na wale waliokutesa wanakwenda kuteswa wao maana Yesu atawaponda watesi wako na kuwapiga wanaokuchukia. Pia mguso huu wa pili utakuletea ustaei wa kazi ya mikono yako, “Na uzuri wa Bwana  Mungu wetu uwe juu yetu na kazi ya mikono yetu utufanyie thabiti naam kazi ya mikono yetu uithibitishe”Zaburi 90:17.
Endelea kufuatilia mfululizo wa ujumbe huu kutoka kwa mtumishi wa Mungu mch.Florian Josephat Katunzi.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni