Idadi ya watu waliokufa kwenye ghorofa
la makao makuu ya Kanisa la SCOAN (Synagogue Church of All Nations) la Nabii TB
Joshua wamefikia 50.
Jengo hilo la ghorofa tano ambalo ni
makao makuu ya kanisa na nyumba ya kulala wageni liliporomoka Jumamosi
wakati ujenzi ukiendelea.
Hadi kufikia siku ya Jumapili jumla ya watu 41
walikuwa wameripotiwa kufa,lakini maiti nyingine tisa zimeongezeka.
Inaelezwa kwamba,mhubiri huyo wa kimataifa alipewa kibali cha kujenga ghorofa
mbili,lakini mwenyewe akaamua kujenga ghorofa tano.
Uokoaji bado unaendelea na
watu wengine mia moja na ishirini na nne walikuwa wameokolewa wakiwa hai hadi kufikia siku ya jumapili.
Kiongozi wa kanisa la Synagogue Church of All Nations(SCOAN) Nabii TB
Joshua nyuma ni jengo liloporomoka
Baadhi ya majeruhi waliookolewa kwenye kanisa hilo akiwa hajitambui.
Waokoaji wakienddelea na shughuli za uokoaji.
Picha hizi ni kwa idhini ya premiumt times -Micheal Abimboye,
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni