YESU NI JIBU

Ijumaa, 14 Agosti 2015

KANISA LA EAGT MLIMA WA FARAJA LAJIPANGA KUPELEKA INJILI VIJIJINI .


Mchungaji kiongozi wa kanisa la EAGT mlima wa Faraja lililopo yombo kisiwani Dar es salaam,mchungaji AIDAN MABUGA,amesema kuwa kanisa hilo ,limeandaa mikakati ya kupeleka injili vijijini.
Alisema hayo siku ya jumapili wakati wa ibada ya kuhitimisha maombi ya mfungo wa siku 40, ambapo katika maombi hayo waliombea mambo mbalimbali ya kanisa pamoja na uchaguzi mkuu wa raisi, wabunge na madiwani utakaofanyika octoba 25 mwaka huu.
Mchungaji Mabuga alieleza kuwa amekuwa na mzigo wa kuhubiri injili tangu alipopata wito wa kumtumikia Mungu miaka kadhaa iliyopita.
Aidha akinukuu maandiko (matendo 20:24) alisema kuwa si vyema kuhubiri tu mjini wakati kuna vijiji ambavyo wanauhitaji mkubwa wa neno la Mungu.
Tayari Mch Mabuga ameshaanza kupeleka injili mijini na vijijini, mwaka juzi ambapo alihubiri mkutano mkubwa katika mji wa Bujumbura nchini Burundi na mamia ya watu walimpokea Yesu kama Bwana na mwokozi wa maisha yao.
Hata hivyo aliongeza kuwa mwaka jana alihubiri katika maeneo ya Bukoba vijijini na Dar es salaam,na mwaka huu mwezi ujao atakuwa na ziara ya kupeleka injilimaeneo ya  vijiji vya Morogoro.
“Tuna mshukuru Mungu ametujalia gari la kubeba waimbaji wachache na vyombo vya mziki, pamoja na hayo bado tuna uhitaji mkubwa wa kupata gari kubwa la kubeba vyombo vya kuhubiria pamoja na vyombo vikubwa vya injili ili kufika maeneo mbalimbali.Tunakuwa tukishilikiana na madhehebu mbalimbali katika mwili wa kristo.” alisema mchungaji Mabuga.

mchungaji AIDAN MABUGA
mchungaji AIDAN MABUGA akisisitiza jambo madhabahuni akiwa na mke wake madhabahuni.



Mchungaji Mabuga akiongoza maombi ya kuhitimisha mfungo wa siku 40 katika kanisa la EAGT yombo Kisiwani.





 Waimbaji wa kanisa la mlima wa Faraja Yombo Kisiwani kwa fundi umeme wakimsifu Mungu wakati wa kuhitimisha mfungo wa siku 40.





Baadhi ya watu wakishuhudia miujiza ambayo walitendewa na Mungu katika maisha yao. 







 Ni wakati wa maombi ya kuombea mipango mbalimbali ya kanisa pamoja na kuombea taifa la tanzania wakati wa kuelekea uchaguzi mkuu wa octoba 2015 uwe wa amani na salama.


 wakati wa maombezi ambapo mchungaji Mabuga akiwaombea waumini na wenye shida mbalimbali.




Baada ya mfungo sasa ni kusherehekea. 
Aliwasihi wadau wa injili kushirkiana naye katika kuchangia ili kufikia malengo hayo kwa njia ya benki na kwa namba za simu.
 EQUIT BANK A/C NO: 3001211248922
JINA : EAGT MLIMA WA FARAJA.
TAWI LA QUALITY CENTRE
M-PESA : 0755 656749
TIGO- PESA : 0713 272368
Mawasiliano:- +255 755 656749
                        +255 713 272368
          E- mail aidan.mabuga@yahoo.com

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni