YESU NI JIBU
Ijumaa, 21 Agosti 2015
ASKOFU GAMANYWA ANGURUMA KATIKA VIWANJA VYA SHEIKH ABEDI AMANI KARUME JIJINI ARUSHA KATIKA MKUTANO WA INJILI.
Kamanda Liberatus Sababas.
Watanzania wameaswa kuwa makini sana katika wakati huu wa kuelekea uchaguzi mkuu maana mara nyingi uchaguzi ndiyo chanzo cha mfarakano na ukosefu wa amani katika baadhi ya mataifa ambayo uchaguzi ulifanyika na kusababisha machafuko.
Kauli hiyo imetolewa na kamanda wa jeshi la polisi mkoa wa Arusaha Reberatus Sababas wakati wa ufunguzi wa mkutano wa injili wa siku tatu ambao unafanyika katika viwanja vya Sheikh Abedi Amani Karume jijini Arusha.
Aidha Kamanda Sababas Amesema kuwa chaguzi ndiyo chanzo cha wananchi kuwa wakimbizi na kupoteza haki zao za msingi kutokana na uchaguzi kutokuwa wa haki na uhuru.
Ameongeza kuwa watanzania wakiwa wanamcha Mungu hatakuwepo mtu ambaye atamtendea mwenzake jambo baya hasa pale ambapo watakuwa wamejazwa na roho mtakatifu katika maisha yao.
Hata hivyo amewasihi watanzania kulinda amani ambayo ni tuni ta Taifa la Tanzania na kusema kila mmoja popote atakapo kwenda awe balozi wa Amani.
Kamanda Sababas akihutubia katika viwanja vya Sheikh Abed Amani Karume.
Askofu Mwizarube wa kanisa la EAGT unga limited akisisitiza jambo katika mkutano wa injili.
Kamanda Sababas Akiwa na Askofu Gamanywa.
Kamanda Sababas akiwa na Askofu Mwizarube.
Askofu Gamanywa akisisitiza jambo mara baada ya kamanda Sababas kumaliza kuhutubia mkutano.
Zoezi la maombi linaanza mara baada ya kamanda kuwasihi maaskofu na wachungaji pamoja na waumini wao kuombea amani wakati wa uchaguzi.
Askofu Gamanywa akishikana mikono na kamanda Sababas.
Kamanda Sababas Akiwa na askofu Gamanywa katikati na kulia askofu Mwizarube.
Kulia ni mke wa askofu Gamanywa Alhappness Gamanywa akiwa na askofu Mwizarbi na mke wake.
Imechapishwa na
Amaninafuraha
kwa
23:14
Tuma Hii kwa Barua pepe
Blogu Hii!
Shiriki kwenye Twitter
Shiriki kwenye Facebook
Shiriki kwenye Pinterest
Lebo:
Arusha
,
Ask Mwizarubi
,
Askofu Gwajima
,
kamanda Sababas
,
mkutano wa ijili
,
Neno
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni