YESU NI JIBU

Jumanne, 25 Agosti 2015

AMA KWELI MUNGU ALIONEKANA KWA NAMNA YA KIPEKEE KATIKA MKUTANO WA SIKU TATU MKOANI ARUSHA AMBAPO WENGI WALIFUNGULIWA NA KUMPOKEA BWANA YESU KAMA BWANA NA MWOKOZI WA MAISHA YAO.

Ni kwanini mpaka sasa wanadamu wanaendelea kuteseka na na kubaki utumwani.
unaweza ukajiuliza katika maisha yako juu ya suala la kuwa utumwani kiuchumi,ufukara, kiafya na hata katika dhambi
hapa askofu mkuu wa wapo mission international askofu Sylvester Gamanywa alifafanua kwa kina juu ya suala la kukombolewa ambapo amesema vyama vya siasa na dini hajaweza kuleta msaada wowote kwa wanadamu.
Askofu Gamanywa amefafanua kwa umakini juu ya aina mbili za roho ambazo zipo ulimwenguni nazo ni roho zilizo kufa na roho zilizo hai ndani ya kristo.
Aidha ameongeza kuwa kuwa watu wote wanaokwenda kwa waganga wa kienyeji na wachawi wamekufa ingali bado wanatembea.

Askofu mkuu wa WAPO Mission International askofu Gamanywa akimtambulisha mke wake Alhappyness ndani ya kanisa la EAGT Sinai Unga limited Arusha.

Mara baada ya kutoka ibadani askofu gamanywa akimshukuru mke wa askofu Leonard Mwizarubi.

Askofu Mwibarubi kushoto akiongozana na askofu Gamanywa mara baada ya kutoka ofisini kwake maeneo ya kanisani.
Katika viwanja vya sheikh Abedi Amni Karume askofu Gamanywa na askofu mwizarubi.

Askofu Gamanywa akiwaongoza watu waliotoa maisha yao kwa Yesu katika sala .

Watu waliosalimisha maisha yao kwa Yesu.





Ndani ya kanisa kusifu na kumwabudu Mungu kila mmoja anafurahia huku wazee wa kanisa na washirika nao wakifuatilia kwa maini ibada. 


Mara baada ya kusifu na kuabudu zoezi la shukrani ndani ya kanisa la EAGT ambapo askofu Mwizarubi na familia yake walimshukuru Mungu kwa binti yao kufunga ndoa na kuolewa kwa heshima.


Zoezi la kuwapongeza waliotoa maisha yao kwa bwana Yesu Kuwa Bwana na Mwokozi wa maisha yao.




kilichofuata kabala ya askofu Gamanywa kupata nafasi ya kfundisha neno la MUNGU ndani ya kanisa ni zoezi la kutangaza uchumba mambo yalikuwa hivyo kama unavyoona katika picha ni hatari kama ndiyo harusi tayari kumbe ni uchumba tu

Moja kwa moja uwanjani hapo ni mwimbaji wa nyimbo za injili Belgano Bukuku akiimba wimbo wake wenye ujumbe ni Mzuri Bwana Yesu.
Alhappyness Gamanywa kulia akiwa na Edina Malissa wakati wa kusifu Mungu katika mkutano wa injili ndani ya viwanja vya sheikh Abedi Amani Karume.






Timu ya kusifu na kuabudu inayoongozwa na Abednego ikiongoza zoaezi na kumsifu MUNGU.
Hata hivyo askofu Gamanywa kawasihi watanzania kuwa makini na kuanza kumiliki na kuachana na njia za udanganyifu ambazo adui shetani anatumia kuwarubuni na kuwapoteza matokeo yake wanakuwa wakiwa masikini kutokana na maradhi,yanayosababishwa na kutokumtii Mungu wa kweli.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni