YESU NI JIBU

Jumamosi, 28 Februari 2015

ENDELEA KUJIFUNZA KILA SIKU BIBLIA YAKO POPOTE ULIPO IFAHAMU BIBLIA YAKO:


1.Kuabudu maana yake ni nini?
Answer:Ni tendo linalogusa akili,hisia,nafsi na utu wa mtu na mwili pia kwa kusujudu,kuanguka kifudifudi,au uso kwa uso.
Mwanzo 17:3
Kuabudu katika Roho na Kweli kunaweza kukafanywa wakati wowote na mahali popote mradi lengo ni kufanyia Mungu Ibada.
2.Kwa nini malkia esta alimwaambia  Mordekai awakusanye wayahudi na wakufunga na kuomba bila kula wala kunywa kwa muda wa siku tatu usiku na mchana kwa ajili yake,naye atafanya hivyo pamoja na wajakazi  wake
Answer:
Kwa lengo la kuingia kwa mfalme ,kinyume cha sheria(maana Hamani amepanga wayahudi wote katika ufalme wa Ahusero waangamizwe na kupanga kuwa hamani atundikwe Esta 3,4)esta 4:16-17.
3.Karama ya kupambanua Roho inatolewa kwa lengo Gani?
 Jawabu:
1.   kutambua chanzo cha miujiza ,ishara na maajabu matendo 8:4-13
2.   Kutambua mawakala wa ibilisi matendo 13:6-12
3.   Kutambua aina ya roho chafu zinazotenda kazi matendo 16:16-18
4.   Kutambua vyanzo vya magonjwa na udhaifu katika miili na nafsi za watu mathayo 12:22-23
5.   Kutambua mafundisho potofu au ya uongo waebrania 1:1-2; 1thethalonike 4:13-17
4.Toa maana sita za rafiki wa kweli kwa mfumo wa kiblia ni nani?
Jawabu:
1. Rafiki ni mtu anayekupenda (yohana15:12)
2.ni mtu aliyetayari kujitoa maisha kwa ajili ya marafiki zake(yohana 15 :13) Yesu pia alionesha hilo kwa kutufia msalabani (rumi 5:8)
3.ni mtu ambaye yupo tayari kukutendea lile jema utakalomwomba akutendee (yohana 15:14)
4. ni mtu anayehusika na kushirikiana nawe(yohana15:15)
maombezi ,mafundisho na makemeo ya urafikiYesu anainua ,kuponya na kuadibisha.
5.ni yule anayejitolea kwa hiari kudumisha urafiki uliopo(yohana 16:16)
kujitoa kwa  moyo wa hiari kulinda kudumisha uhusiano wa kirafiki(yoh 7:17)
6.ni yule ambaye anaendelea  kuchagua kuwa  rafiki wakati wengine wote wanajitenga na kukimbia kwa sababu mbalimba(yoh15:17)

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni