YESU NI JIBU

Alhamisi, 26 Februari 2015

VIONGOZI MBALIMBALI WAWEKWA WAKFU TAYARI KWA KUMTUMIKIA MUNGU KATIKA JIMBO LA MASHARIKI KASKAZINI



Kiongozi ni mtu mwadilifu ,mwenye imani,asiyelaumiwa kwa jambo lolote baya sanjari na kuwa na imani ya kuwatumikia jamii inayomzungukwa kwa lengo la kuwaleta maendeleo.
Kauli hiyo imetolewa jijini Dar es salaam na askofu wa jimbo la Mashariki kaskazini askofu Geofrey Massawe katika hafla ya kuwasimika na kuwaweka wakfu viongozi wa sehemu mbalimbali katika jimbo hilo ambapo amesema kuwa sifa ya kiongozi ni kuwatumikia waumini na jamii inayomzunguka.

 Askofu Geofrey Masawe akiwaweka wakfu viongozi mbalimbali katika jimbo la mashariki kaskazini.





 Kutoka kushoto ni katibu wa jimbo la mashariki kaskazini Charles Shilla na katikati niaskofu jimbo hilo Askofu Geofrey Masawe na kulia ni makamu askofu.
 Zoezi la kuwaweka wakfu viongozi
 Katibu akimpa Askofu majina ya viongozi wanaowekwa wakfu walioteuliwa kuongoza katika sehemu mpya na ya Zamani.
Aidha Askofu Massawe amesema kuwa ni vyema kiongozi anapochaguliwa ama kuteuliwa ni vizuri kuwatumikia wananchi na sio kutekeleeza matakwa yake binafsi jambo ambalo limesababisha mianya mbalimbali ya rushwa na kushindwa kuleta maendeleo.
''Ili kutokomeza tatizo la rushwa na kushindwa kutekeleza majukumu ya kila siku kiongozi anatakiwa kuwa jasiri na mwadilifu katika majukumu yake ya kila siku kama kiongozi ambaye ni kioo cha jamii'',alisema askofu Masawe.
Hata hivyo amewataka viongozi na wananchi kwa ujumla kusimamia, kulinda na kutunza amani ambayo imeasisiwa na waasisi wa taifa hili kabla ya uhuru mpaka sasa kwa kusudi la kudumisha amani na usalama ndani ya taifa hasa katika kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi mkuu.
Amani na Utulivu iliopo nchini ni wajibu wa kila mtanzania kuendelea kulinda na kudumisha maana katika kipindi hiki cha uchaguzi na kuwasihi viongozi mbalimbali kuwa makini na kuwa makini na waadilifu.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni