YESU NI JIBU

Jumamosi, 21 Februari 2015

IFAHAMU BIBLIA YAKO 21 FEB JIFUNZE ILI NENO LA MUNGU LIKAE KWA WINGI MOYONI MWAKO MAANA NI TAA YA MIGUU YAKO:



1.Rafiki ni nani ?
answer:ni mtu ambaye unaweza kumwamini ,kujiweka wazi kwake.
              ni mtu anayeweza kuchangia kufaulu na ustawi wako katika maisha.
2.Mfalme yupi ambaye amezikwa katika makaburi ambayo amejichimbia katika mji wa Daudi na alikufa katika mwaka wa ngapi wa utawala wake.
Answer: Ni mfalme Asa aambaye alikufa katika mwaka wa 41 wa kumiliki kwake
               2nyakati 16:13-14
3.Neno kuabudu lina maana gani?
Answer:Ni tendo linalogusa akili,hisia,nafsi na utu wa mtu na mwili pia kwa kusujudu,kuanguka kifudifudi,au uso kwa uso
mwanzo 17:3 Tendo hilo hufanywa pasipo ushawishi wa kitu ,wala si nje ya moyo wa kumtambua Mungu kuwa wa thamani  kuliko kitu chochote anayestahili kupewa ibada ya pekee na kupelekea kujitoa kwake bila unafki wala ubinafsi .
4.Karama Tisa za Roho Mtakatifu zimegawanyika katika mafungu matatu nazo ni zipi
      1.Karama za ufunuo
·       Neno la maarifa
·       Neno la hekima
·       kupambanua Roho
2.Karama za uwezo
·       imani
·       karama za kuponya
·       matendo ya miujiza
3.Karama za usemi
·       Unabii
·       Aina za lugha
·       Tafsiri za lugha
5.Daudi na Jonathani walikuwa marafiki ni kitu (siri)gani kilichosababisha urafiki wao udumu toa sababu  sababu nne ama siri nne.
1.    mwambatano ulianzia katika roho zao.
2.    upendo wa kweli kati yao(1sam 18:1)
3.    utayari wa kila mmojaa wao kuwa mwaminifu katika patano la urafiki wao(1sam18:3)
4.    upendo wenye msukumo wa kutoa na kujitoa kwa hiari kila mtu kwa mwenzie(1sam18:4)


Hakuna maoni :

Chapisha Maoni