YESU NI JIBU

Jumatano, 25 Februari 2015

HALI INAZIDI KUWA TETE HUKO NCHINI SYRIA WAKRISTO WAENDELEA KUTEKWA NYARA ZAIDI YA 350.

Kuna hofu kuwa raia wakristo kutoka Syria wametekwa nyara na wanamgambo wa Islamic State.
Duru kutoka kwa jamii hiyo sasa inathibitisha kwamba zaidi ya raia 200 walitekwa nyara Jumanne baada ya vijiji kadhaa kushambuliwa kaskazini mwa Syria.

Wengi wa waliotekwa nyara ni wanawake na wazee.Wakati huo huo, mapigano yangali yakiendelea katika maeneo yaliyoko karibu na mji wa Hassaka.
Kuna taarifa zinazosema kuwa makanisa yameteketezwa moto na kundi la IS katika vita hivyo vikali kati ya wanamgambo hao na makabila ya Wakurdi wanaoungwa mkono na wakristo wenye silaha.

Taswira kamili ya mkasa uliowakumba wakristo hawa wa Syria ndiyo mwanzo unaanza kujitokeza.


 Wakristo kutoka Syria wameanza kutoroka wanakoishi.
Lakini kikundi cha wapiganaji wa kikristo kimetoa madai kuwa idadi hiyo ni kubwa hata zaidi ya hiyo.Hata hivyo kimedokeza kuwa zaidi ya watu 350 wametekwa,huku hayo yakiarifiwa waumii wengine wa kikristo wameanza kukimbia vijiji vyao wakihofia kushambuliwa na wanamgambo wa Islamic State.

Na bado vita vinaendelea huku waislamu hao wakikabiliana na waasi wa kikurdi pamoja na washirika wao wa kiksristo katika mji wa Hassaka.
Source BBC,mshirikishe na mwenzako,unaweza pia kutoa maoni yako.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni