Kuna hofu kuwa raia wakristo kutoka
Syria wametekwa nyara na wanamgambo wa Islamic State.
Duru kutoka kwa jamii hiyo sasa
inathibitisha kwamba zaidi ya raia 200 walitekwa nyara Jumanne baada ya vijiji
kadhaa kushambuliwa kaskazini mwa Syria.
Wengi wa waliotekwa nyara ni
wanawake na wazee.Wakati huo huo, mapigano yangali
yakiendelea katika maeneo yaliyoko karibu na mji wa Hassaka.
Kuna taarifa zinazosema kuwa
makanisa yameteketezwa moto na kundi la IS katika vita hivyo vikali kati ya
wanamgambo hao na makabila ya Wakurdi wanaoungwa mkono na wakristo wenye
silaha.
Taswira kamili ya mkasa uliowakumba
wakristo hawa wa Syria ndiyo mwanzo unaanza kujitokeza.
Lakini kikundi cha wapiganaji wa
kikristo kimetoa madai kuwa idadi hiyo ni kubwa hata zaidi ya hiyo.Hata hivyo kimedokeza kuwa zaidi ya watu 350 wametekwa,huku hayo yakiarifiwa waumii
wengine wa kikristo wameanza kukimbia vijiji vyao wakihofia kushambuliwa na
wanamgambo wa Islamic State.
Na bado vita vinaendelea huku
waislamu hao wakikabiliana na waasi wa kikurdi pamoja na washirika wao wa
kiksristo katika mji wa Hassaka.
Source BBC,mshirikishe na mwenzako,unaweza pia kutoa maoni yako.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni