Waziri Membe ameyasema hayo wakati akitoa hotuba ya kufunga Kongamano la Kimataifa la Utume la Kanisa la Waadventista Wasabato lililofanyika katika Uwanja wa Taifa, Jijini Dar es Salaam tarehe 07 Februari, 2015.
Mhe. Membe alisema kuwa
Dini na madhehebu yanayo nafasi kubwa katika kujenga jamii yenye maadili na
hofu ya Mungu wakiwemo viongozi na hivyo kupelekea taifa kuwa na amani, upendo
na mshikamano.
Alieleza kuwa kama Waziri
wa Mambo ya Nje, amejifunza kuwa diplomasia na hofu ya Mungu vikifanya kazi
pamoja hakuna changamoto yoyote isiyoweza kukabiliwa.
“Dini na Diplomasia vina
husiana pale masuala ya amani, ulinzi na usalama yanapoguswa. Hivyo nawaomba
mshiriki katika kutengeneza viongozi bora katika jamii zetu kwa misingi ya
uadilifu ambao watasimamia amani na kujiepusha na vitendo viovu ikiwemo
rushwa,” alisema Mhe. Membe.
Aidha, alilipongeza
Kanisa hilo kwa kuwa mfano mzuri wa ustahimilivu na uvumilivu wa kidini hapa
nchini. Alieleza kwamba kamwe hajawahi kusikia Kanisa la Waadiventista Wasabato
limeingia katika mgogoro na Serikali, dhehebu au dini nyingine na hilo ni funzo
kubwa kwa Watanzania, kwamba kutofautiana kiitikadi, kidini, kikabila au rangi
si sababu tosha ya kuwagombanisha na kuvuruga amani ya nchi.
“Nalipongeza Kanisa lenu
kwa kuwa mfano mzuri wa uvumilivu wa kidini na imani, mnaendesha mambo yenu kwa
uvumilivu mkubwa na kushirikiana na dini zote na hili linatufundisha kuwa
kutofautiana kwetu sio sababu tosha ya kugombana” alisisitiza Membe.
Pia, Mhe. Membe
alilihakikishia Kanisa hilo dhamira ya Serikali ya kuendelea kushirikiana nalo
kwa ajili ya ustawi wa nchi na kufafanua kuwa Serikali itaendelea kulinda uhuru
wa kuabudu kwa dini zote kama inavyoelezwa kwenye Katiba ya nchi. “Serikali
inao wajibu wa kusaidia dini na madhehebu kufanyakazi kwa uhuru. Bahati
nzuri Katiba inayopendekezwa imezingatia kulinda uhuru huo hivyo tuiunge mkono”
alifafanua Waziri Membe.
Vilevile alilisifu Kanisa
hilo kwa kuanzisha miradi ya huduma zikiwemo Shule15 za Sekondari na Msingi,
Chuo Kikuu na Hospitali mbili ambavyo vinatoa mchango mkubwa kwa Serikali na
Wananchi kwa ujumla.
Waziri
wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe
(Mb.) (wa pili kulia), akiongozana na Rais wa Baraza Kuu la Makanisa ya
Sabato Duniani, Askofu Ted Wilson (wapili kushoto), Waziri wa
Kilimo, Mhe. Stephen Wassira (kushoto), pamoja na Mchungaji Blasius
Luguri, Mwenyeji wa Kongamano la Kimataifa la Utume kuingia katika
Uwanja wa Taifa Jijini Dar es Salaam.
Waziri
Membe akiwahutubia mamia ya Waumini wa Kanisa la Sabatoikiwa ni siku ya
kilele cha Kongamano la Kimataifa la Utume kwa Makanisa ya Sabato.
Wengine katika picha waliokaa ni Rais wa Kanisa hilo duniani, Askofu
Wilson na Mkewe pamoja na Mhe. Wasira wakimsikiliza mmoja wa Viongozi
akitafsiri kwao baadhi ya maneno ya Kiswahili yaliyokuwa kwenye hotuba
ya Mhe. Membe.
Kikundi cha watoto kikitoa burudani katika maadhimisho hayo.
Rais wa Baraza Kuu la Makanisa ya Sabato Duniani, Askofu Wilson akimpongeza Waziri Membe mara baada ya kumaliza kuwahutubia Waumini wa kanisa hilo waliokusanyika Uwanja wa Taifa kwa ajili ya Kongamano la Kimataifa lilililofikia kilele leo.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni