Viongozi
wa dini na madhehebu yote
nchini wameombwa kuhakikisha
wanajitahidi kuhubiri amani
kwa watanzania wote, ili kulinda
amani iliyopo sasa
isipote, jambo ambalo litasaidia
matendo kama ya
ukatili na umasikini
kutokomezwa kama sio kwisha kabisa.
Hayo yamesemwa
na Mwasisi na mwanzilishi wa
kituo cha nyumba
ya maombi (HPC) Apostle Patrick
Kayimbi Emmanuel maarufu
kama Apostle P.K.E , alipokuwa
akihubiri kwenye kongamano
maalum la kuombea
amani ya Tanzania
linalofanyika kituoni hapo
Tabata- ugombolwa, ambapo amesema kuwa
watanzania hawapaswi kufunga
mikono yao juu
ya maombi ya
amani na badala
yake amesema wanapaswa
kuzidi kumuomba Mungu
kwani mara zote
shetani hapendi amani walionayo Watanzania ama wanadamu kwa
ujumla.
“Sheteni asitudanganye
kusema tuna amani, Hapana shetani
anaandaa vurugu na
kutenganisha dini moja na
dini nyingine,acha nikwambie
hakuna vita kubwa na
mbaya kama vita
ya dini na
ukabila,vita ya dini
ikianza tunaona makanisa
kuchomwa na vita
ya kabila pia ikianza
tutaona watu wakitenganishwa ndio
maana Mungu anataka
kanisa pamoja na
watanzania wote bila
kuangalia itikadi wala dhehebu kwa
pamoja tuunganishwe kwa
pamoja tumwite YESU
juu ya Tanzania” Alisema Apostle
P.K.E huku akishangiliwa.washiriki wa kongamano hilo.
Aidha Apostle
P.K.E aliwataka watanzania
kutegemea amani ya
kutosha nchini kutokana
na kongamano hilo
kudhamiria kuleta
amani nchini,
huku akiwasihi wananchi
wote kumrudia Mungu
na kumtafuta kwaajili
ya amani. Na huku
akiwahakikishia watanzania
kuwa ifikapo jumatatu
ya februari 24
Bunge maalum la
katiba litakuwa shwari
na halitakuwa na
misuguano ya wajumbe ,wabunge kama ilivyokuwa
hapo awali siku
chache zilizopita.
Pamoja na
hayo Apostle P.K.E
alisema kuwa kongamano
hilo pia limelenga
kuombea kampeni mbalimbali
za uchaguzi zinazoendela ,pamoja na
uchaguzi mkuu utakofanyika mwakani
nchini.
Hivyo, kutokana
na shughuli aliwataka wanasiasa kutumia ndimi zao vyema
wakati wa kuwepo kwa amaani maana ulimi ni
kiungo kidogo ila madhara yake ni
makubwa sana, kituo cha nyumba
ya maombezi imeona
ni vizuri kuombea chaguzi mbalimbali nchini.
Hali kadhalika Apostle
P.K.E alisema kuwa
kituo cha nyumba
ya maombezi kipo
tayari kuombea wale
wote wanaohitaji uongozi
endapo tu wakikiri
kuacha kwenda kwa
waganga wa kienyeji.
“We
unayetaka udiwani, unayetaka
ubunge, unayetaka kuchaguliwa
tupo tayari kukuombea
ukisema nitaacha uganga
nataka nikwambie kwa maombi haya
tunayoenda kufanya uchawi
hautatumika Tanzania uganga wala
sadaka ya damu”Alisisitiza
Apostle P.K.E
Na kwa
upande wa mhubiri
kutoka nchini Zambia
Apostle Peter Mwanga
alisema kuwa ni
vyema kila mtu
asimame katika nafasi
yake na kujiuliza ni
kitu gani amefanya
kwa taifa ambacho
kitafanya watu wamkumbuke.
Pamoja na hayo ni
lazima kila mtu
awe na hofu
ya Mungu na
kujiulize umefanya nini kwa majirani
zako na maisha
yako binafsi na kama
hujafanya lolote , ndani ya
nyumba ya bwana
lazima ufanye kitu ili
ukumbukwe na Mungu.
Naye diwani
wa kata ya Segerea
Azuri
Mwambagi aliyeshiriki pia katika
kongamano hilo alisema
kuwa miongoni
mwa mambo yanayopelekea
amani kulegalega ni
pamoja na suala
la umasikini na
kusema kuwa kwa
hali ya kawaida
ni bora mtu
achoke mwili kuliko
mtu kukata tama
Hali
hiyo ni hatari sana
kwa amani,Lakini pia bwana Mwambagi
amepongeza kituo hicho
kwa kuanda kongamano
hilo la kuombea
amani ya nchi.
Itakumbukwa kwamba
kongamano hilo lilianza
tangu februari 16
na linatarajiwa kuhitimishwa
Machi 2 , huku likijumuisha
jopo la watumishi
wa Mungu kutoka
takribani nchi tano
ambazo ni Namibia, Zambia, Canada, Dr Congo,
pamoja na Kenya.
Maoni 2 :
Mungu ibariki Tanzania
Mungu ibariki Tanzania
Chapisha Maoni