Kila kona neno la MUNGU linahubiriwa kwa lengo la kuwafungua
wengi walifungwa na nguvu za giza ,uchawi ,ushirikina na wale wote wenye
matatizo mbalimbali wanfunguliwa na nguvu za BWANA YESU.Hata hivyo watu mbalimbali wamefika kumpokea bwana YESU kama Bwana na Mwokozin wa maisha yao ,hayo yote yamefanyika huko Musoma mkoani Mara ambapo kumekuwa na hali mbaya kila kukicha vyombo vya habari vinaripoti mauaji yanayotendeka na kuendelea katika Mkoa huo.Watumishi wa MUNGU wakiongozwa na askofu wa jimbo la Mara askofu Godson Shaula
Makamu Askofu wa jimbo la Mara kaskazini la TAG askofu Godson Shaula akifuatilia neno la MUNGU kwa makini.
Daniels Mapunda Akitoa ushuhuda wake wake kabla hajaokoka katika mkutano wa Kange ambao unaendelea Musoma mjini maeneo ya
machinjioni,anaongelea walivyokuwa wakiwafanya watu misukule,kuwapeleka na kuwatumikisha.
Alisema wachawi wanakuwa na dawa ya kumchukulia mtu ,wakichukua huwa wanakuwa na dawa wanayotumia kichawi kisha Yule anayetakiwa kuwa msukule anatokwa na damu puani mdomoni na puani na kisha anaitwa na kuongozwa kwa kutumia kioo,hatimaye ndugu hudhani kuwa amekufa Kumbe yupo nyumbani kafichwa sehemu,anasema mtu aliyechukuliwa msukule Anatokwa na damu puani,lakini yote
Tisa Mtu wa Mungu halogeki wala maiti yake haiwezi kuchukuliwa na wachawi alisema Daniel akihitimisha ushuhuda wake.
Wachungaji wakifuatilia kwa makini ushuhuuda wa mchungaji Daniel kwa makini.
Wachungaji wa kanisa la Tanzania Assemblies of God Musoma
mjini wakisikiliza neno la MUNGU kwa makini.
Makamu askofu Godson wakiwa na mke wake.
Mhubiri Daniel Mapunda kutoka Tanga katika kanisa
la TAG Musoma mjini maeneo ya
machinjioni,akizungumza na waongofu wapya.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni