YESU NI JIBU

Jumatatu, 17 Februari 2014

UNGANA NA ASKOFU SYLVESTER GAMANYWA KATIKA OPARESHENI MILIKISHA KWA MUJIBU WA BIBLIA.



Falsafa ya umikilishaji kwa mujibu wa Biblia

Baada ya kupitia kwa ufupi falsafa ya kumilikisha kwa mujibu wa Biblia, leo napenda kukujuza kuhusu mkakati ulioandaliwa na utekelezaji wa kampeni ya OPERESHENI MILIKISHA. Mkakati huo ni kuundwa kwa Mtandao wa Vikundi vya Maadili na Uchumi Tanzania (UVIMAUTA). Mtandao huu utaendeshwa kwa kuzingatia sera iliyotungwa kwa madhumuni hayo, ndio nataka kukushirikisha baadhi ya mambo muhimu yaliyomo katika sera hiyo:

Utangulizi

Suala zima la umikilishaji halikuanzia hewani, bali ni mchakato ulioanza na mpango mkakati wa miaka 20 wa MAADILI KWA KIZAZI KIPYA  ambao ulizinduliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania tangu mwaka 2010. Mpango huu ulisheheni mikaakti mikuu mitatu ambayo ni 1. Ujersho wa maadili ya kibibilia, 2. Unoaji wa vipaji vya uongozi wa kizazi kipya, na 3. Kumilikisha uchumi endelevu kwa kizazi kipya.

Huu ukiwa ni mwaka wa 3 tangu kuzinduliwa kwa mpango huu, mikakati miwili imefanyiwa kazi kikamilifu. Mkakati wa Urejesho wa maadili ulifanyiwa kazi kupitia OPERESHENI TAKASIKA, Mkakati wa uonaji vipaji vya uongozi umezalisha mchakato wa kuanzishwa kwa CHUO KIKUU CHA UONGOZI WA KIMAADILI (MOLUT) na CHUO CHA VIPAJI(TIT) vyote vikisimamia na wanataaluma waliobobea katika taaluma ya elimu.

Mwaka hu ndio tunashughulikia kikamilifu mkakati wa tatu wa kumilisha uchumi ambapo tumeanzisha kampeni maalum ya OPERESHENI MILIKISHA. Wakati huo huo tumepata wazo jipya (ufunuo maalum) la kuunda mtandao wa vikundi vya maadili na uchumi Tanzania (UVIMAUTA) ambao ndio utahusika kumilikisha uchumi kwa kizazi chenye maadili Tanzania.

Katika kutekeleza mkakati wa kuunda mtandao huu, imetungwa sera maalum ambayo imezinduliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe.Dkt Jakaya Mrisho Kikwete ikiwa ni mwendelezo wa mpango mama aliouzindua mwaka 2010 wa MAADILI KWA KIZAZI KIPYA. Katika makala ya leo tunaipitia sera kwa ufupi ili kupata picha kamili ya mtandao wenyewe. Mambo tunayokwenda kuyapitia ni Maono, dhima na lengo kuu;; kisha habari za haki na wajibu wa uanachama pamoja na maeelezo mengine muhimu.

Maono, dhima na lengo kuu

Maono ya Mtandao wa Vikundi vya Maadili na Uchumi Tanzania (MVIMAUTA) ni;  “Kufikia mwaka 2028, vijana wa Tanzania wawe wanamiliki uchumi endelevu  ambao msingi wake ni  ardhi  inayomilikiwa na watanzania wenyewe”.

Dhima kuu ni; “Kuhamasisha na kuwawezesha vijana kumiliki uchumi kupitia vyanzo vikuu ambavyo ni; ardhi, madini, mifugo, maji, na kilimo”.

Lengo kuu ni; “Kumkwamua kijana kutoka katika hali ya umasikini hadi awe na makazi yake mwenyewe, ardhi kwa ajili ya kilimo, na shughuli halali za kumuingizia kipato”.

Walengwa wakuu wakiwa ni makundi ya: Vijana wanaohitimu katika vyuo vya kati na vyuo vikuu na wanashindwa kupata ajira; Vijana waishio mijini kwa kufanya biashara ndogo ndogo zisizoweza kukidhi mahitaji yao ; Vijana waishio vijijini wenye kutegemea kilimo cha jembe la mkono peke yake; Vijana wajasiriamali walioanzisha miradi midogo ya biashara; Wanandoa na wazazi/walezi kama wadau muhimu katika urithishaji

Haki na wajibu wa kila mwanachama

Kila mwanachama wa MVIMAUTA atakuwa na haki za msingi za kumwezesha kutimiza matarajio yake ndani ya kikundi chake. Hata hivyo kupatikana kwa haki kutazingatia jinsi anavyotimiza wajibu wake katika kikundi. Baadhi ya haki za msingi za mwanachama ni: Kupewa taarifa zote zinazohusu maendeleo ya kikundi na mtandao mzima; Kushika nafasi ya uongozi kupitia mfumo wa ukuaji wa mtandao; Kupata gawio stahiki la faida itokanayo na uzalishaji wa miradi aliyochangia mtaji wake; Kupata mafunzo ya kimaadili na kiuchumi; Kumilikishwa ardhi katika miradi itakayoanza baada ya miradi ya mafunzo,na Kukopeshwa mitaji.

Kwa upande wa wajibu ni kwamba kila mwanachama wa MVIMAUTA atatakiwa kutimiza wajibu wake katika kikundi chake. Kutotimiza wajibu kwa mwanachama kutamfanya mwanachama huyo kutokuwa mwanachama hai na hivyo kukosa haki zilizotajwa hapo juu.

Wajibu wa kila mwanachama, ndani ya kikundi chake na katika mtandao kwa ujumla utakuwa ni kufuata misingi ya dhana kuu ya MVIMAUTA na malengo yake makuu makuu saba (7) ambayo ni kama yafuatayo: Kudumisha umoja wa kikundi na mtandao mzima; Kujenga uhusiano wa karibu wa kufahamiana na kusaidiana; Kutoa michango ya kiibada na kimasaidiano; Kushirikisha wengine maendeleo ya mtandao; Kushiriki mikutano ya kiibada ili kuombeana na kujengana kiroho; Kujitoa kwa hali na mali katika shughuli za uzalishaji mali na Kutumia vipawa na vipaji kwa manufaa ya mtandao

Umuhimu na upekee wa MVIMAUTA

Kiama ilivyo kawaida katika jamii, kila j”ambo jipya” lazima lihojiwe kuhusu umuhimu na upekee wake, ndipo lipate uhalali wa kuita “jambo jipya”! Kwa upande wa UVIMAUTA, nina hakika ni “jambo jipya” kwa jamii ya kitanzania na huenda katika bara zima la Afrika kwa kuzingatia sababu zifuatazo:

1.   Muunganiko wa maadili na uchumi.

Kwa karne nyingi kanisa la leo limetenganisha ”Maadili na uchumi” kama vitu visivyo na uhusiano. Hali hii imesababisha udhaifu badala ya ufanisi. Kulingana na tafiti zilizokwisha kufanyika huko nyumba, taarifa zake zinafanana katika kubainisha kwamba,  ”uchumi bila maadili” huzalisha ufisadi katika jamii. Na kwa jamii ya kitanzania hiki ndicho kinachosababisha malalamiko na lawama dhidi ya wanaodaiwa kuitwa ”mafisadi”! Pili Maadili nayo bila uchumi ni kudumisha ufukara katika jamii

Lakini kanisa la kwanza, la mitume wa kwanza halikutenganisha maadili na uchumi! Utafiti wa kihistoria unaonesha kwamba kanisa la jijini Yerusalemu lilidumu takribani miaka 40, likiwa na maelfu ya waamini zaidi ya 30,000 lakini halikuwa na mtu mmoja maskini wa kipato MVIMAUTA unarejea historia hii ukilenga kudhibiti ufisadi na kuzalisha uadilifu; na kuhamasisha uchumi kwa kufuta ufukarana na fikira tegemezi

2.   Fursa ya ukuzaji wa vipaji vya uongozi

Hivi leo tunashuhudia kinyanganyiro cha kuwania nafasi za uongozi katika uutmishi wa umma. Nafasi zenyewe ni chache, lakini baya zaidi ni kuwa jamii yetu haina ”kiwanda maalum” cha kuzalisha viongizi wenye sifa na vipaji vya uongozi! Kinachowasukuma walio wengine katika kuwania uongozi sio uwezo wa kuongoza bali tamaa ya kujipatia kipato kupitia nafasi za uongozi au kaka ajira ya kawaida.

UVIMAUTA unakuja na fursa pekee ya kukuza vipaji vya uongozi miongoni mwa vijana watakaojiunga na mtandao huu. Kumbuka kwamba, kila kikundii cha watu ishirini kitakuwa na kiongozi wake. Na kila  kikundi kizima kinapoundwa kitapata mafunzo ya uchumi na uongozi.

Katika mafunzo ya uongozi kila mwanakikundi anatafsiriwa kuwa ni ”kiongozi mtarajiwa” wa kikundi kipya atakachokiunda yeye mwenyewe. Hivyo hivyo zoezi linaendelea la ”vikundi kuzaa vikundi” ambapo mafunzo ya uongozi huendelea na fursa mpya za uongozi kupatikana kwa kuundwa vikundi vipya.

Kigezo cha kuwa kiongozi ni uwezo wa kuongoza na si vinginevyo. Uwezo wa kuongozi ni kipaji maalum na ushahidi unathibitishwa pale ambapo kiongozi anazalisha viongozi wengine wapya chini yake na hivyo yeye kupannda daraja la uongozi ili kusimamia viongozi aliowazalisha mwenyewe!

3.   Fursa ya kukuza mitaji kupitia mtandao

Kikwazo kikubwa ambacho kinadaiwa kuendeleza umaskini wa kipato katika jamii, ni ukosefu wa mitaji. Kila mwenye wazo la kufanya mradi wa uzalishaji anajikuta anakabiliwa na changamoto ya ukosefu wa mtaji. Wakati huo huo njia pekee iliyopo ya kupata mtaji ni mikopo kuotka katika taasisi za fedha. Masharti kukopesha ni mkopaji kuwa na dhamana ya nyumba au mali yenye thamani inayozidi kiwango cha mkopo anaoutaka. Wengi hawana dhamana na hivyo kujikuta hawakopesheki.

MVUMAUTA unakuja na jawabu la miaka mingi la ukosefu wa mitaji. Mfumo wa kuunda vikundi unashughulikia changamoto ya ukosefu wa mitaji kwa sababu, watu ishirini wanaweza wenyewe kuchangiana mitaji kwa zamu kwa kila mmoja kupata mtaji mkubwa wa mradi anaotaka kuufanya, na bila masharti ya kutoa dhamana.

Aidha, kikundi kinapojiunga katika mtandao huu, tayari kinaskuwa kimeingia katika jamuiya ambayo kuna vikundi vingine ambavyo vimeanzishwa kwa madhumuni ya uwezeshaji wa vikundi visivyo na mitaji ili mradi vitaingia ubia ambao utahusisha kugawa faida baada ya mauzo.

Huu ni uwezo wa ndani ya vikundi na mtandao wenyewe. Isitoshe, kwa kupitia mtandao huu, kuna fursa ya kuziendea taasisi za fedha na kuziomba mikopo kwa ajili ya miradi ya mtandao na dhamana ikawa ni mtandao wenyewe kwa taratibu ambazo zi lazima kuzielezea kwa hivi sasa. Ila wewe amini kwamba changamoto ya ukosefu ya mitaji kwa wanachama wa mtandao inakuwa imeshughulikiwa kikamilifu!

Hapa fursa ni Mtandao wenyewe kuwa dhamana ya mikopo ya vikundi badala ya wana vikundi kusumbuka kuweka dhamana ya mali zao binafsi.

4.   Fursa ya kuibua na kuendeleza vipaji

Kutokana na ripoti ya maoni ya vijana wasomi wa vyuo vikuu ambayo ndiyo imechangia kuundwa kwa mtandao huu; imebainika kwamba elimu inayotolewa na sekta yetu ya elimu, haina mikakati ya kuibua na kukuza vipaji, bali imejaa nadharia tegemezi. Kwa mantki hii mpaka sasa kuna upungufu wa fursa za kubaini vipaji mbali mbali na kuviendeleza kwa kuviwezesha kimafunzo na mazoezi kwa viwango vya kimataifa

MVIMAUTA utatoa fursa kupitia vikundi vyake kutoa mafunzo na fursa za mazoezi ambayo gharama zake zitatokana na miradi maalum kwa madhumuni hayo. Isitoshe, kuna taasisi ya Bishop Gamanywa Foundation (BGF) imeanzishwa kwa maono ya kufadhili mafunzo na mazoezi ya ukuzaji vipaji. MVIMAUTA untanufakika na taasisi hii katika eneo hili lililotelekezwa!

Itaendelea toleo lijalo

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni