Maaskofu na wachungaji wameitaka serikali ichukue hatua madhubuti kutokomeza wimbi la uchomaji wa makanisa sambamba na uharibifu wa mali kwani hali hiyo inaweza kusababisha amani kupotea katika taifa hili la Tanzania
Kauli hiyo imetolewa na umoja wa makanisa ya kipentekoste kupitia kwa katibu wake jijini Daar es salaam ambao wamekutanika kutafuta ufumbuzi wa tatizo la uchomaji wa makanisa
Akizungumza na waandishi wa habari waliofika katika kikao hicho askofu DAvid Mwasota ambaye ndiye katibi alisema kuwa kikao hicho kilikuwa na lengo la kutathimini uharibibu wa majengo na mali zingine za kanisa na jinsi ya kumaliza tatizo hili ambalo linaonekana kama ni endelevu
Baadhi ya wachungaji pamoja na mbunge wa kigamboni mhe. Faustine Ndungulile wakitembelea makanisa ambayo yameharibiwa na watu wanaosadikiwa kuwa ni waislamu
Mheshimiwa Ndugulile akizungumza na maaskofu na wachungaji kuendelea kuwa na uvumilivu kwa tatizo lililojitokeza
Mwenyekiti waumoja wa makanisa ua kipentekoste mkoa wa Dar es salaam askofu Bruno Mwakibolwa akimwelezea mbunge jambo mhe. Ndugulile
hivyo divyo hali ilivyokuwa
Askofu John Zakaria jimbo la Kinondoni na askofu Bruno Mwakibolwa wa jimbo la Temeke wakimsikiliza mbunge wa Kigamboni kwa makinisa Mhe.Faustine ndugulile.
Katibu wa PCT askofu David Mwasota akielezea hali ilivyojitokeza juu ya suala la uchomaji wa makanisa
waandishi wakichukua habari baada ya kikao cha maaskofu na wachungaji waliofika kutathmini hasara na jinsi ya kutafutia ufumbuzi tatizo hilo
Hizi ni baadhi ya CD ambazo ni vielelezo ambazo viongozi hao walisema kuwa wamepeleka kwa viongozi wa serikali jinsi walivyokuwa wajipanga kuangamiza ama kuaharibu makanisa.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni