YESU NI JIBU

Ijumaa, 19 Oktoba 2012

KIKAO CHA MAASKOFU NA WACHUNGAJIWA UMOJA WA MAKANISA YA KIPENDEKOSTE MKOA WA DSM WALIPOKUSANYIKA KWENYE KIKAO

Maaskofu na wachungaji wameitaka serikali ichukue hatua madhubuti kutokomeza wimbi la uchomaji wa makanisa sambamba na uharibifu wa mali kwani hali hiyo inaweza kusababisha amani kupotea katika taifa hili la Tanzania
Kauli hiyo imetolewa na umoja wa makanisa ya kipentekoste kupitia kwa katibu wake jijini Daar es salaam ambao wamekutanika kutafuta ufumbuzi wa tatizo la uchomaji wa makanisa

Akizungumza na waandishi wa habari waliofika katika kikao hicho askofu DAvid Mwasota ambaye ndiye katibi alisema kuwa kikao hicho kilikuwa na lengo la kutathimini uharibibu wa majengo na mali zingine za kanisa na jinsi ya kumaliza tatizo hili ambalo linaonekana kama ni endelevu


  Askofu Bruno Mwakibolwa ambaye ndiye mwenyekiti wa makanisa ya kipentekoste mkoa wa Dar es saala akimsikiliza kwa makini mchungaji ambaye kanisa lake liliharibiwa.

 Baadhi ya wachungaji pamoja na mbunge wa kigamboni mhe. Faustine Ndungulile wakitembelea makanisa ambayo yameharibiwa na watu wanaosadikiwa kuwa ni waislamu

 Mheshimiwa Ndugulile akizungumza na maaskofu na wachungaji kuendelea kuwa na uvumilivu kwa tatizo lililojitokeza
 Mwenyekiti waumoja wa makanisa ua kipentekoste mkoa wa Dar es salaam askofu Bruno Mwakibolwa akimwelezea mbunge jambo mhe. Ndugulile



hivyo divyo hali ilivyokuwa

Askofu John Zakaria jimbo la Kinondoni na askofu Bruno Mwakibolwa wa jimbo la Temeke wakimsikiliza  mbunge wa Kigamboni kwa makinisa Mhe.Faustine ndugulile.

 Katibu wa PCT askofu David Mwasota akielezea hali ilivyojitokeza juu ya suala la uchomaji wa makanisa


waandishi wakichukua habari baada ya kikao cha maaskofu na wachungaji waliofika kutathmini hasara na jinsi ya kutafutia ufumbuzi tatizo hilo



Hizi ni baadhi ya CD ambazo ni vielelezo ambazo viongozi hao walisema kuwa wamepeleka kwa viongozi wa serikali jinsi walivyokuwa wajipanga kuangamiza ama kuaharibu makanisa.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni