Wakati serikali ikijitahidi kukabiliana na vitendo vya uchomaji
moto makanisa nchini vinavyofanywa na baadhi ya wanaharakati wa Kiislamu,
imebainika kuwa Kanisa la Salvation
Ministry for all Nations (SMAN) lililoko Mbezi Juu Jijini Dar es Salaam, limechomwa moto zaidi ya mara
tatu.
Uongozi wa Kanisa hilo umelimbia Gazeti hili kuwa licha ya
matukio hayo ya hujuma wanazofanyiwa na waumini wa Kiislamu kutoka katika
msikiti wa Al Mubarak ulioko jirani na Kanisa hilo, usiku wa Jumapili iliyopita
ya Desemba 2, 2012 , waumini hao walilibomoa Kanisa hilo na kufanya jaribio
jingine tena la kulichoma moto.
Kwa mujibu wa Mchungaji kiongozi wa Kanisa hilo
la SMAN Freddy Mwamtembe na Msaidizi
wake Mch. Eliya Sudi, matukio matano ya hujuma mbaya dhidi yao yameripotiwa katika vituo vya polisi Mbezi
Juu na Kawe na kufunguliwa majalada yanayoeleza
jinsi hujuma hizo zilivyofanyika kwa muda na nyakati tofauti.
Hujuma ya kwanza ya uharibifu mali na uchomaji moto wa
Kanisa hilo iliripotiwa katika akituo cha polisi Kawe Februari 25, 2012 na kufunguliwa jalada nambari KW/RB/1743/2012
la kuchoma moto choo cha kanisa hilo,
ambapo jalada la pili la siku hiyo hiyo lilifunguliwa katika kituo cha Polisi
Mbezi Juu likiwa na nambari MBJ/RB/586/2012 likitaarifu juu ya tukio la
kuchomwa moto Kanisa hilo na kuharibu mali majira ya saa saba usiku.
Jalada jingine lilifunguliwa Machi 10, 2012 katika kituo cha
Polisi Mbezi juu na kupewa nambari
MBJ/RB/714/2012, likitoa taarifa juu ya hujuma ya kuchomwa moto kwa Kanisa hilo
la SMAN.
Hujuma nyingine lililofanyiwa kanisa hilo imo katika jalada
la kituo cha Polisi Kawe lenye nambari KW/RB/7974/2012 kama taarifa ya tukio lililofanywa Agosti 12, 2012 na waumini
28 wa msikiti wa Al Mubarak kwa kuvamia ibada,
kujeruhi waumini na kuharibu mali za Kanisa hilo, ambapo Mchungaji Msaidizi
Eliya Sudi alijeruhiwa akiwa madhabahuni.
Aidha uongozi wa Kanisa hilo ulilikabidha gazeti hili waraka
unaoelezea jinsi waumini wa msikiti huo wanavyoshirikiana na mama mmoja
kulifanyia fujo kwa kufukia msingi wa jengo lake na kisha mama huyo kuchimba
msingi na kuanza ujenzi wa nyuma yake katika kiwanja cha Kanisa hilo.
Uongozi huo wa Kanisa la SMAN ulisema ulilifikisha suala hilo katika ofisi
ya Serikali ya Mtaa wa Ndumbwi kupitia
mjumbe wa nyumba kumi shina namba 40 Mbezi
Juu Bwana Bonifasi Matiku kwa ajili ya
utatuzi, lakini hawakupatiwa msaada wowote, hadi ikabidi wamwandike barua Afisa
Mtendaji wa kata ya Mbezi Juu, kumtaarifu juu ya kiwanja cha kanisa lao kuvamia
na mama huyo ambaye kwa sasa jina lake limehifadhiwa.
Mjumbe huyo alidhibitisha juu ya kuwepo kwa hujuma dhidi ya
Kanisa hilo na
hatua alizochukua,ambapo liitaka serikali kutumia sheria ili kukabiliana nazo
na kuzikomesha.
“Nakumbuka siku nilipofika ofisini kwa Mtendaji wa Kata ya Mbezi Juu, niliishia kutukanwa na wajumbe niliowakuta
pale (majina tumeyahifadhi kwa sasa), wakinieleza mbele ya Mtendaji huyo kwamba
ni lazima mama huyo atajenga katika eneo
la kiwanja chetu cha Kanisa. Nilimtahadharisha Mtendaji juu ya matusi
niliyotukanwa lakini akanitaka niondoke akidai atashughulikia suala hilo. Mwandishi hadi leo hakuna kilichofanyika”, alisema
Mchungaji Mwamtembe.
Alisema tayari amelifikisha suala la hujuma za Waislamu dhidi ya Kanisa lake katika
ofisi za Kamanda wa Mkoa wa Kipolisi wa Kinondoni alikoahidiwa kushughulikiwa
haraka kwa mujibu wa sheria.
“Kwa kweli sisi Wakristo ni wavumilivu sana kwa vile tunapenda amani na utakatifu.
Tunaiomba sana
serikali iwashughulike watu hawa wachache wasiopenda amani na wanaochochea
vurugu za kidini. Ugomvi wa kidini ni mbaya sana. Tunaomba serikali iwe makini katika
hili”, alisema Mch. Mwamtembe.
Alisema waumini hao korofi wa Kiislamu wanaolihujumu Kanisa lake
kwa kulichoma moto, kuharibu mali na kujeruhi
washirika ni watu wanaofahamika wazi na hufanya hujuma hizo wazi wazi,
wakitamka wazi kuwa hawataki Kanisa
katika maeneo yao; jambo ambalo ni kinyume kabisa na Katiba ya nchi inayoruhusu uhuru wa kuabudu kwa kila mtu
Mmoja wa Mashehe wa Msikiti
wa Al Mubarak Mbezi Juu aliyetajwa kuwa mstari wa mbele kuhamasisha
waumini wake kulihujumu kanisa la SMAN, hakuweza kupatikana kutokana na
kutofika msikitini hapo kwa uwazi, akiogopa kukamatwa na Polisi wanaomsaka.
Aidha juhudi za kumpata mama aliyetajwa kushirikiana na
waumini wa msikiti wa Al Mubarak kulihujumu kanisa hilo hazikuzaa matunda, kutokana na makazi yake kutojulikana.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni