YESU NI JIBU

Alhamisi, 4 Oktoba 2012

Hatimaye ufumbuzi wa mafundi mitambo wa vitengo vya sauti umepatikana mara baada ya wakufunzi kutoka Afrika ya kusini kuwasili nchini na kuanza kuwafundisha ili kuweza kutafutia ufumbuzi tatizo hilo.

Wataalamu kutoka makanisa mbalimbali wamefika kujifunza jinsi ya kutatua tatizo hilo katika sehemu zao za kazi na wakufunzi hao wameletwa na HUDUMA VOICE OF HOPE MINISTRY.
Mafunzo hayo yalifanyika kwa muda wa siku mbili 28 na 29 septemba katika ukumbi  wa kanisa TAG Mwenge iliyopo Mwenge jijini Dar es saalam

 Mchungaji Gay kutoka Afrika ya kusini akiwa na mtafsiri wake ambaye alikuwa akifundisha somo katika semina ya siku mbili ya mafundi mitambo wa sauti na viongozi wa vikundi vya kusifu na kuabudu.

Mchungaji Gay akiwa na mke wake pamoja na mtaalamu wa sauti bwana Wesley ambaye yeye alikuwa akifundisha juu ya soun engineering kwa wataalamu mbalimbali waliofika katiak ukumbi wa kanisa la Mwenge kujifunza.

Mmoja wa wanafunzi waliofika kwenye Kongamano la mafundi mitambo akifuaatilia kwa makini akielekezwa na maalamu na pia ni mmoja wa waimbaji wa bendi ya Dar es saalam Goespel


Engineer Wesley akiwa na mtafsiri wake Mbuto wakati akitoa mafunzo juu ya vifaa vya sauti( sound system)

Waimbaji wa kikundi cha Messengers Band wakitumbuiza katika kongamano la mafundi mitambo.




Kiongozi wa Messengers Band ndugu Noel akiongoza katika kusifu na kuabudu katika kongamano.


Mmoja wa wapiga vyombo wa benbdi ya Messengers ndugu Waziri akionesha umahiri wake.




Ndug Gadrody Mng'anga mwenye shati blue pamoja na wanafunzi wenzake waliofika katika kongamano la mafundi mitambo.


Ni mafundi mitambo kutoka sehemu mbalimbali wakifuatilia kwa makini mafunzo ambaye yalitolewa na wataalamu kutoka Afrika ya Kusini.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni