YESU NI JIBU

Jumatano, 31 Oktoba 2012

MAOMBI YA KUHAMASISHA AMANI KATIKA TAIFA LA TANZANIA




MAOMBI YA KUHAMASISHA AMANI KATIKA TAIFA LA TANZANIA

Suala la amani na usalama ndani ya nchi ama taifa ni jukumu la kila mwananchi kuhakikisha kuwa unadumu sanjari na kumwomba Mungu juu ya jambo hilo.
Kauli hiyo ilitolewa jijini Dar es saalam na askofu Daktari Mgulu kilimba wa huduma ya christian mission Fellowship wakati wa ibada maalum yamaombi ya kuhamasisha amani nchini.
Aidha askofu DK Kilimba alisema neno la Mungu limetuagiza katika 1timotheo 2:1-2; kuwa kabla ya mambo yote nataka dua, sala, maombezi na shukurani vifanyike kwa watu wote; kwaajili ya Wafalme na wenye mamlaka, tuishi kwa utulivu na amani, katika utauwa wote na ustahivu ,tukiwa Kanisa la Mungu, tumechukua hatua hii ya kuanza kuliombea Taifa kwa kuugua mno ili Amani  tuliyopewa na Mungu na kuenziwa na waasisi wa Taifa hili iweze kudumishwa.
"ndugu zangu watanzania sote tufahamu kuwa, msimamo tuliyojiwekea katika katiba yetu ya jamhuri ya muungano wa tanzania, ni kupiga marufuku kila namna ya ubaguzi ukiwemo wa kijinsia, rangi na kidini. Katiba ya 1977 ibara 13(5) ambapo kwa upande wa madhehebu ya dini tanzania tuna dini kubwa tatu na nyingine ndogondogo dini kubwa ni ukristo, uislamu na dini za kijadi.toka mwanzo wakristo na waislamu tumekuwa tukishirikiana pamoja katika misiba, sherehe mbalimbali, kuoleana, kuishi katika nyumba moja  na kufanya shughuli za kijamii kwa pamoja bila kubaguana kabla na baada ya  miaka hamsini ya uhuru nchi yetu" alisema askofu dk kilimba .
Aliongeza kuwa wakristo na watanzania kwa ujumla ni vyema kufahamu kuwa, hakuna nchi  yeyote katika  bara la afrika yenye idadi kubwa ya wakristo na waislamu wanaoishi kwa amani na upendo  kama tanzania,ila kwa sasa watu wasioitakia amani nchi yetu wanataka kupenyeza chuki za kidini  ili isiwe nchi ya amani bali ya vurugu.
Kutokana na hayo hivi karibuni tumeshuhudia kuwepo kwa vitendo vinavyoashiria ubaguzi wa kidini kwa baadhi ya vikundi toka makundi ya dini kubwa kudai haki zao ambazo kimsingi wanaona wanastahili kuwa nazo sawa na dini nyingine, hali hii imefanya vikundi hivi vitumie vyombo vya habari hususani redio, magazeti na machapisho mbalimbali kueleza hisia zao kwa jamii, jambo ambalo limesababisha kuwepo kwa mgawanyiko katika jamii iliyokuwa imeshikamana na mgawanyiko huu unazidi kukua siku hadi siku na kusababisha hali ya chuki kwa mamlaka ya nchi na hatimaye dini moja na nyingine.
"Baada ya kufanya utafiti wa kina kwanini kuwepo na chuki baina ya makundi ya dini na serikali tumeona kuwa, makundi haya ya dini yanaiona serikali inawanyima haki zao na inapendelea  dini moja na hivyo kutumia mfumo wake katika utawala, ambapo  madai ya kundi hilo yanawapelekea kuwafanyia vurugu waumini wa kundi wanalosadiki kuwa linapendelewa na serikali, jambo ambalo linawafanya wanaofanyiwa vurugu wasitumie  uhuru wao wakufanya ibada ambayo kimsingi walipewa mungu na kuandikwa katika katiba ya nchi yetu", aliongeza.
Pamoja na hayo tukiwa kanisa la mungu, hali hii inatupelekea kuona kuwa bado serikali yetu haijawajibika ipasavyo katika kuelekeza sera na shughuli zake kwa lengo la kuhakikisha kuwa sheria za nchi zinalindwa na kutekelezwa, kimsingi haki na uhuru wa watu wengine au maslahi ya umma vinapaswa kutoathiriwa kabisa na  matumizi mabaya ya uhuru wa haki za watu binafsi.
Hivyo askofu Dk Kilimba aliongeza kusema kanisa baada ya kumlilia mungu kwa machozi na maombi mengi, tumeamua kuchukua mwelekeo wa uwajibikaji  usio wa maneno tu, kwani suala la  kutoa matamko ya kulaani limefanywa na dini na serikali kwa mkazo mkubwa. Na kwa upande wa serikali,  watawala wa nchi yetu wamekuwa wakilaani na kukemea, ubaguzi wa dini,  rushwa na ufisadi katika taifa hili bila mafanikio na hata leo tunawaona vijana wanatwangana hadharani kutokana na kushamili kwa rushwa ,hii yote ni kwa sababu  hayo ni vita ya kiroho na inapaswa kukemewa na viongozi wa dini na watawala wanapaswa kuchukua hatua. Kwa jinsi hii, kanisa limelitazama jambo hili kiroho zaidi kwa kutambua kuwa chuki na rushwa ni roho kamili inayotoka kwa shetani, hivyo watu wa kiroho tunalo jukumu la kuzipinga hila zote za shetani kwa dua, sala na maombi ili kuleta amani ya kudumu katika taifa letu, ambalo linasifika kuwa ndiyo kitovu cha amani afrika na duniani.
Akielezea kwa hisia alisema "Ndugu zangu wakristo na viongozi wa dini,  ikumbukwe na izingatiwe kuwa  nyumba za ibada ni sehemu ya kumwabudu mungu,  hivyo zitumike kuhubiri dini tuliyo amuriwa na mungu na sio siasa, na  pasiwe mahali  pa kuandaa na kuchochea vurugu na chuki miongoni mwetu kwani viongozi wa dini wanaaminiwa  sana na waumini wao na  lolote watakalo waambia waumini, huaminiwa kuwa limetoka kwa mungu".
Aidha aliongeza kuwa ikumbuke kuwa, tunafanya kila kitu vizuri zikiwemo ibada zetu kwasababu ya amani tuliyonayo, amani isipokuwepo hakuna kitu kinaweza kufanyika katika nchi iwe kwa waumini na wasio wauimini, iwe kwa maskini au matajiri. Amani ikishaondoka, matajiri au wenye pesa watakimbia na kuwa wakimbizi wa nchi zingine, huku masikini wakikosa mahali pa kwenda na kuishia kuuawa na kupoteza maisha. Kwa hiyo ni vema kuitunza amani yetu na kuilinda,kamwe tusiichezee amani tuliyonayo katika nchi yetu, hii ni tunu tuliyopewa na mungu na kuachiwa na waasisi wa nchi yetu ili tuienzi, hivyo kila mmoja wetu ni mdau wa amani. Mkulima anahitaji amani ili aweze kupata mazao shambani mwake; daktari anahitataji amani ili afanye kazi zake vema hospitalini, kadhalika mfanya biashara na mwanasiasa wote wanahitahi amani.
Pamoja na hayo yote askofu Dk Kilimba alisema kuwa kamanda Suleiman Kova wa kanda maalum ya dar es saalamkwa ameonesha juhudi  zake za kuifanya Dar-es-saalam iendelee kuwa bandari ya amani, ameonesha ushupavu na umadhubuti mkubwa katika kauli zake, kwani mchango wake umeleta heshima iliyotukuka katika vyombo vya dola nchini  na kwa watanzania wote.
Katika maombi hayo ya kuhamasisha amani nchini yalitanguliwa na maombi ya watu 12 waliowakilisha zaidi makabila 120 ya tanzania kwa kutumia lugha  za makabila hayo kama alama ya umoja na mshikamano.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni