YESU NI JIBU

Jumamosi, 23 Aprili 2016

UTAKASO NDIYO NJIA PEKEE YA KUMWOKOA MWANADAMU NA KUMWEKA MBALI NA DHAMBI NA MAGONJWA NA SHIDA MBALIMBALI -KWA MCHUNGAJI KATUNZI


Mchungaji Florian Katunzi akimwombea mwanamke ambaye alifunjika mkono na haikupona kwa muda mrefu alipoombewa alianguka na ikamlazimu kumwombe.

Mchungaji Katunzi akimwombe mwanamke aliyefika ibadani na mwanaye kupata maombi na maombei katika ibada maalum ya utakaso.

Watoto nao hawakuwa nyuma ndani ya ibada ndani kanisa


zoezi la kufungullliwa ndiyo linaendeleaa hapa







Wakati wa maombi na maombezi ambayo yaliongozwa na mchungaji Katunzi
wengine walifika na picha za wapendwa wao kwa kuashiria imani ya kuombewa popote pale walipo

Huyu ndiye dada aliyefika kutoa ushuhuda na kutoa sadaka ya shukrani
Mchungaji Katunzi akifundisha neno kabla ya maombi na maombezi ndani ya ukumbi wa kanisa la EAGT City Center lilopo Mtoni Mtongani.



Wakati wa ushuhuda mchungaji Katunzi aliwaombea wadada waliofika kanisani na kushuhidia mateso waliyopitia kwa muda mrefu kiasi cha kupoteza watoto wake wawili na sasa anamshukuru Mungu maana alimfungua na kumweka huru mbali na mateso
hapa mchungaji hayupo pichani akitoa maelekezo kuwa kalia waliokukalia kuanzia sasa na wadada hawa walifika madhabahuni kutoa ushuhuda na na kuanza kufuata maelekezo ya mchungaji Katunzi

Mara baada ya usghuhuda aliwaombea wadada waliofika kutoa ushuhuda na kuanza kulipuka mapepo na kuanza kuombewa na mchungaji Katunzi madhabahuni ndani ya kanisa la EAGT City Center.
Mchungaji Racheal Katunzi kutoka kushoto akifuatilia neno la Mungu ambalo mchungaji Katunzi anafundisha madhabahuni.

Ni wakati wa maombi na maombezi inua mikono juu tumwombe Mungu.

Pilika pilika za maombi na maombbezi kamata madhabahu na ujiombee maana Mungu anakusikia ndivyo askofu alivyosikika akisema.



Mchungaji Rachael Katunzi ambaye ni mama mchungaji wa kanisa la EAGT City Center akimwombea mtoto kanisani hapo.
Mchungaji Katunznia akimwombea mtu ambaye miguu yake ilikuwa na shida na Mungu mtenda miujiza alimfungua na kumweka huru
Pita mbele ya madhabahu tumlilie Mungu atakufungua maana ni mwema sana 
Waumini wametakiwa kusimamia utakatifu ambayo ndiyo njia pekee inayoweza kumasaidia 
mwananadamu kumwona Mungu katika maisha yako ya kila siku na hakuna anayeweza kumwona Mungu pasipo utakatifu
Hayo yalisemwa na askofu wa kanisa la EAGT City Center iliyopo jijini Dar es salaam askofu Florian Josephat Katunzi wakatui akifundisha somo la utakaso kanisani hapo ambapo alisema kuwa utakaso ndiyo njia pekee ya kufanya mambo mema na kumwona Mungu na ukuu wake katika maisha yako yako ya kila siku.
Aidha alisema kuwa utakaso ni tendo la kiimani la kujitenga na vitu ambavyo ni viovu au kilicho kiovu
jambo linalokupelekea utengwe na dhambi na mauti na hata na biashara na maisha yako yanakuwa salama na bora
"waumini wakishatengwa na dhambi watakuwa wametengwa na matatizo na magonjwa maana kupigwa kwake Yesu wanadamu wamewekwa huru na kufunguliwa maana wanadamu wengi wamekuwa wakiteseka kateseka bila kufahamu kuwa kwa nini wanapitia katika matesso hayo"alisema askofu Katunzi.
Aidha alisema kuwa ni vyema waumini wakaaamu kuwa makini kuepuka  kuwa sehemu ya kuhifadhia majini na mapepo bila wewe kufahamu maana mwisho wake utakuwa ni mbaya kuliko hapo awali maana Mungu akishamsamehe mtu  dhambi kinafuata ni kuondolewa magonjwa na matataizo zote zinazokuandama katijka maisha yako na katika ukoo jamii na familia yako.
Akinukuu kitabu cha Isaya 38:1-6 alisema kuwa Hezekia aligua,akawa katika hatari ya kufa lakini Mungu alimtuma Samweli kupeleka ujumbe kwake kuwa atengeneze mambo ya nyumba yake maaana anaenda kufa hakika.
AkitoA mfano w akijana ambaye aliletwa na mama yake kanisani alisema kuwa mume wake alikufa kwa ugonjw wa kuumwa kichwa na mtoto wake wa kiume pia alikufa kwa kuumwa kichwa na alipougua na mwingine aliamua kumleta kanisani na kuanza kumwombea na mwisha wake mama alidondoka na kuanza kupagwa na mapepo badala ya mgonjwa na kuanza kusema kuwa tumeifunga familia hii.
Akielezea juu ya suala la utakaso alisema kuwa kuna utakaso wa roho na wa nafsi hayo yote mwamini lazima afunguliwe katika tatizo hilo na kuwekwa huru na hapo ndipo mkambo yake yatakuwa salama  maana kupitia Damu ya Yesu ndiyo inayotakasa na kuweka huru kila mmoja ambaye amemkubali Yesu kama Bwana na mwokozi wa maisha  yake.
"kila mmoja ambaye anapitia katika mapito magumu ni vyema afunguliwe na kuwekwa huru mbali na dhambi na magonjw a ambayo yamekuwa yakikitesa kwa muda mrefu.Ni vyema akaamua kujiuliza maswali kuwa ni kwanini unakubali kiteseka na kupitia katika mapito magumu huku Yesu amekuweka huru" alisema Askofu katunzi kwa kusisitiza.
Aliongeza kuwa Mungu aliye mweka huru ndugu Bonifasi asiliwe nyama na wachawi ndiye ambaye anaenda kukuokoa na matatizo na masumbuko ya adui shetani na kukuweka huru mbali na magonjwa na matatizo na taabu mbalimbali ambazo yamekuwa kikwazo katika maisha yako ya kila siku ambayo imekupelekea kukata tamaa.
Uovu ulioko ndani ya familia yako,jamii yako na hata katika ukoo wako wewe unaweza kuondoa kwa kuomba na kufunga huku ukitolea sadaka na kukombolewa na upoenda kanisani tarajia kukutana naMungu sio askofu Katunizi.
Askofu katunzi pia alisema kuwa siku ya tarehe 26 April 2016 kutakuwepo na ibada maalum ya familia ambayo itaanza kuanzia saa mbili asubuhi hadi saa saba kwa lengo la kuomba kutengwa na uovu
Ambapo alinukuu kitabu cha Ayubu 1:11 kwa muda mwingi ayubu alikuwa akimpendeza Mungu katika misha yake hapo shetani akasema kuwa ni kwa vile kulikuwepo na ulinzi wa Mungu juu yake na ndipo alisposema gusa mali yake naye atakuwacha.
"ibada hii itakuwa wa kuowambea na kuwakomboa kwa kuwaombea na kuwatolea sadaka ya ukombozi maana hata Ayubu hakuwaacha watoto wake nyuma ila aliwapeleka katika nyumba ya ibada pamoja na kutolea sadaka na kuwaombea rehema maaana inawezekana kuwa walitenda dhambi"alisema askofu katunzi.
Kuna madhehebu ya dini ambayo hawaachi watoto wao nyuma wanaenda anao katika nyumba  ya ibaada ila waumini wengine wanaacha watoto wao manyumbani hata neno la Mungu hawafundishi ndani ya akili zao zimejaa masomo ya dunia na mambo yaasiompendeza Mungu .
Hata hivyo alisema kuwa Inatakiwa watoto wako wafundishwe neno la Mungu jumapili jioni na jumamosi jioni ili watoto wafundishwe na kukumbushwa masuala ya Mungu ili aweze kusimama katika nafasi yake wenyewe.
Nao wahudumu wa kanisa hilo hawakuwa nyuma kupita mbele mara baada ya huduma nao kupata maombi kwa mchungaji Katunzi

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni