Mchungaji Florian Katunzi akimwombea mwanamke ambaye alifunjika mkono na haikupona kwa muda mrefu alipoombewa alianguka na ikamlazimu kumwombe.
Mchungaji Katunzi akimwombe mwanamke aliyefika ibadani na mwanaye kupata maombi na maombei katika ibada maalum ya utakaso.
Watoto nao hawakuwa nyuma ndani ya ibada ndani kanisa
zoezi la kufungullliwa ndiyo linaendeleaa hapa
Wakati wa maombi na maombezi ambayo yaliongozwa na mchungaji Katunzi
wengine walifika na picha za wapendwa wao kwa kuashiria imani ya kuombewa popote pale walipo
Huyu ndiye dada aliyefika kutoa ushuhuda na kutoa sadaka ya shukrani
Mchungaji Katunzi akifundisha neno kabla ya maombi na maombezi ndani ya ukumbi wa kanisa la EAGT City Center lilopo Mtoni Mtongani.
Wakati wa ushuhuda mchungaji Katunzi aliwaombea wadada waliofika kanisani na kushuhidia mateso waliyopitia kwa muda mrefu kiasi cha kupoteza watoto wake wawili na sasa anamshukuru Mungu maana alimfungua na kumweka huru mbali na mateso
hapa mchungaji hayupo pichani akitoa maelekezo kuwa kalia waliokukalia kuanzia sasa na wadada hawa walifika madhabahuni kutoa ushuhuda na na kuanza kufuata maelekezo ya mchungaji Katunzi
Mara baada ya usghuhuda aliwaombea wadada waliofika kutoa ushuhuda na kuanza kulipuka mapepo na kuanza kuombewa na mchungaji Katunzi madhabahuni ndani ya kanisa la EAGT City Center.
Mchungaji Racheal Katunzi kutoka kushoto akifuatilia neno la Mungu ambalo mchungaji Katunzi anafundisha madhabahuni.
Ni wakati wa maombi na maombezi inua mikono juu tumwombe Mungu.
Pilika pilika za maombi na maombbezi kamata madhabahu na ujiombee maana Mungu anakusikia ndivyo askofu alivyosikika akisema.
Mchungaji Rachael Katunzi ambaye ni mama mchungaji wa kanisa la EAGT City Center akimwombea mtoto kanisani hapo.
Mchungaji Katunznia akimwombea mtu ambaye miguu yake ilikuwa na shida na Mungu mtenda miujiza alimfungua na kumweka huru
Pita mbele ya madhabahu tumlilie Mungu atakufungua maana ni mwema sana
Waumini wametakiwa kusimamia utakatifu ambayo ndiyo njia pekee inayoweza kumasaidia
mwananadamu kumwona Mungu katika maisha yako ya kila siku na hakuna anayeweza kumwona Mungu pasipo utakatifu
Waumini wametakiwa kusimamia utakatifu ambayo ndiyo njia pekee inayoweza kumasaidia
mwananadamu kumwona Mungu katika maisha yako ya kila siku na hakuna anayeweza kumwona Mungu pasipo utakatifu
Hayo
yalisemwa na askofu wa kanisa la EAGT City Center iliyopo jijini Dar es salaam
askofu Florian Josephat Katunzi wakatui akifundisha somo la utakaso kanisani
hapo ambapo alisema kuwa utakaso ndiyo njia pekee ya kufanya mambo mema na
kumwona Mungu na ukuu wake katika maisha yako yako ya kila siku.
Aidha alisema
kuwa utakaso ni tendo la kiimani la kujitenga na vitu ambavyo ni viovu au
kilicho kiovu
jambo
linalokupelekea utengwe na dhambi na mauti na hata na biashara na maisha yako
yanakuwa salama na bora
"waumini
wakishatengwa na dhambi watakuwa wametengwa na matatizo na magonjwa maana
kupigwa kwake Yesu wanadamu wamewekwa huru na kufunguliwa maana wanadamu wengi
wamekuwa wakiteseka kateseka bila kufahamu kuwa kwa nini wanapitia katika
matesso hayo"alisema askofu Katunzi.
Aidha
alisema kuwa ni vyema waumini wakaaamu kuwa makini kuepuka kuwa sehemu ya kuhifadhia majini na mapepo bila
wewe kufahamu maana mwisho wake utakuwa ni mbaya kuliko hapo awali maana Mungu
akishamsamehe mtu dhambi kinafuata ni
kuondolewa magonjwa na matataizo zote zinazokuandama katijka maisha yako na
katika ukoo jamii na familia yako.
Akinukuu
kitabu cha Isaya 38:1-6 alisema kuwa Hezekia aligua,akawa katika hatari ya kufa
lakini Mungu alimtuma Samweli kupeleka ujumbe kwake kuwa atengeneze mambo ya
nyumba yake maaana anaenda kufa hakika.
AkitoA mfano
w akijana ambaye aliletwa na mama yake kanisani alisema kuwa mume wake alikufa
kwa ugonjw wa kuumwa kichwa na mtoto wake wa kiume pia alikufa kwa kuumwa
kichwa na alipougua na mwingine aliamua kumleta kanisani na kuanza kumwombea na
mwisha wake mama alidondoka na kuanza kupagwa na mapepo badala ya mgonjwa na kuanza
kusema kuwa tumeifunga familia hii.
Akielezea
juu ya suala la utakaso alisema kuwa kuna utakaso wa roho na wa nafsi hayo yote
mwamini lazima afunguliwe katika tatizo hilo na kuwekwa huru na hapo ndipo
mkambo yake yatakuwa salama maana
kupitia Damu ya Yesu ndiyo inayotakasa na kuweka huru kila mmoja ambaye
amemkubali Yesu kama Bwana na mwokozi wa maisha
yake.
"kila
mmoja ambaye anapitia katika mapito magumu ni vyema afunguliwe na kuwekwa huru
mbali na dhambi na magonjw a ambayo yamekuwa yakikitesa kwa muda mrefu.Ni vyema
akaamua kujiuliza maswali kuwa ni kwanini unakubali kiteseka na kupitia katika
mapito magumu huku Yesu amekuweka huru" alisema Askofu katunzi kwa
kusisitiza.
Aliongeza
kuwa Mungu aliye mweka huru ndugu Bonifasi asiliwe nyama na wachawi ndiye
ambaye anaenda kukuokoa na matatizo na masumbuko ya adui shetani na kukuweka
huru mbali na magonjwa na matatizo na taabu mbalimbali ambazo yamekuwa kikwazo
katika maisha yako ya kila siku ambayo imekupelekea kukata tamaa.
Uovu ulioko
ndani ya familia yako,jamii yako na hata katika ukoo wako wewe unaweza kuondoa
kwa kuomba na kufunga huku ukitolea sadaka na kukombolewa na upoenda kanisani
tarajia kukutana naMungu sio askofu Katunizi.
Askofu
katunzi pia alisema kuwa siku ya tarehe 26 April 2016 kutakuwepo na ibada
maalum ya familia ambayo itaanza kuanzia saa mbili asubuhi hadi saa saba kwa
lengo la kuomba kutengwa na uovu
Ambapo alinukuu
kitabu cha Ayubu 1:11 kwa muda mwingi ayubu alikuwa akimpendeza Mungu katika
misha yake hapo shetani akasema kuwa ni kwa vile kulikuwepo na ulinzi wa Mungu
juu yake na ndipo alisposema gusa mali yake naye atakuwacha.
"ibada
hii itakuwa wa kuowambea na kuwakomboa kwa kuwaombea na kuwatolea sadaka ya ukombozi
maana hata Ayubu hakuwaacha watoto wake nyuma ila aliwapeleka katika nyumba ya
ibada pamoja na kutolea sadaka na kuwaombea rehema maaana inawezekana kuwa
walitenda dhambi"alisema askofu katunzi.
Kuna
madhehebu ya dini ambayo hawaachi watoto wao nyuma wanaenda anao katika nyumba ya ibaada ila waumini wengine wanaacha watoto
wao manyumbani hata neno la Mungu hawafundishi ndani ya akili zao zimejaa
masomo ya dunia na mambo yaasiompendeza Mungu .
Hata hivyo
alisema kuwa Inatakiwa watoto wako wafundishwe neno la Mungu jumapili jioni na
jumamosi jioni ili watoto wafundishwe na kukumbushwa masuala ya Mungu ili aweze
kusimama katika nafasi yake wenyewe.
Nao wahudumu wa kanisa hilo hawakuwa nyuma kupita mbele mara baada ya huduma nao kupata maombi kwa mchungaji Katunzi
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni