YESU NI JIBU

Jumapili, 3 Januari 2016

KILA MTANZANIA ATAKIWA KULIOMBE TAIFA AMANI ILI AMANI NA USALAMA UENDELEE KUDUMU NA WANANCHI WAINULIWE KIUCHUMI.

Watanzania wametakiwa kuliombea taifa amani ili liendelee kudumu katika hali ya utulivu upendo na mshikamano na kuepukana na machafuko yanayoweza  kutokana na viongozi kushindwa kuongoza kwa haki na hivyo kujenga chuki miongoni mwa wananchi wake.
Akitoa salamu za mwaka mpya kwa waumini wa kanisa katoliki katika ibada ya uzinduzi wa parokia mpya ya mbarali askofu wa jimbo katoliki la Iringa ambaye pia ni rais wa baraza la maaskofu katoliki nchini TEC,Mhashamu askofu Tarcisius Ngalalekumtwa amesema watanzania wana kila sababu ya kumshukuru mungu  na kuendelea kuombea viongozi wa nchi kutenda haki kwa watu wote ili amani iendelee kuwepo nchini.
Awali akisoma risala ya waumini wa parokia ya mbarali katibu wa Parokia hiyo Bwana Francis Katuli amemshukuru askofu huyo wa jimbo la Iringa kukubali kuigawa Parokia ya Rujewa na kuzaa parokia ya pili ya mbarali kwa lengo la kurahisisha huduma za kiroho kwa waumini wake na kufanya jimbo la iringa kufikisha idadi ya Parokia 38.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni