Unaweza ukawa na maswali mengi katika maisha yako ila kumbuka maandiko yanavyosema juu ya siku za mwisho,kuwa watatokea manabii wa uongo,na watawadanganya wengi.
Ndugu msomaji wa blog hii hili sasa ni tukio la pili la mwanadamu kujiita mungu mara baada ya yule raia wa Kenya ambaye naye alijiita mungu na hatimaye akafariki baada ya kuugua ila waumini wake walikataa na kusema hajafariki wakati ni tukio la kweli kuwa amefariki.
Sasa hapa ni nchini Demokrasia ya Congo huyu naye anajiita mungu,ila ikumbukwe kuwa na hata Tanzania alishawahi kutokea mtu mwingine naye alijiita Adamu wa pili ila naye alifariki na waumini wake yaani wafuasi nao walidai kuwa amepaa kwenda mbinguni jambo ambalo lilionekana kuwa sio la kweli.
Source ITV,
MSOMAJI WA BLOG HII TUPE MAONI YAKO,
MSOMAJI WA BLOG HII TUPE MAONI YAKO,
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni