BARAZA la Sanaa la Taifa (Basata) limezidi kutoa wito kwa Waimbaji wa muziki wa Injili kujisajili katika baraza hilo ili stahiki zao zitambulike inavyotakiwa.
Mkurugenzi wa
ukuzaji Sanaa na Mtukio wa Basata, Maregesi Kwirujira Ng’oko alisema waimbaji
wengi wa muziki wa Injili wa Tanzania kuzingatia hilo.
Ng’oko
alisema kujisajili Basata kuna faida na fursa nyingi ambazo ni msaada ambao
utasaidia kupata haki zao kupitia kazi zao.
Ng’oko
alisema kwa kuwa wao ndio wasimamizi wa kazi za sanaa ni jukumu lao
kuwakumbusha mara kwa mara wasanii kujisajili.
Aidha Ng’oko
alisema wanatoa salamu hizo kwa wasanii pindi inapotokea mikinzano katika ufanikishaji
wa kazi zao.
Naye Makamu
Mwenyekiti wa Kamati ya maandalizi ya Tamasha la Pasaka, Abihudi Mang’era
alisema wanafikiria kuongeza msukumo kwa waimbaji wa muziki wa Injili kuhusu
kujisajili Basata katika baadhi ya matukio.
Mang’era
alisema wanafikiria kutoa elimu ya kujisajili Basata katika matamasha yao ama
kusaka namna ya kufanikisha utambuzi wa waimbaji katika baraza hilo.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni