Wabunge wa
Kenya wametofautiana vikali bungeni na
kuvuana mashati huku wakirushiana ngumi kufuatia mjadala kuhusu mswaada
tatanishi wa usalama ambao wabunge wa upinzani wanasema unakiuka uhuru wa
wakenya.
Bunge lililazimika kuahirisha vikao
vyake kwa dakika 30 badala ya kujadili mswada tatanishi kuhusu usalama wa nchi.
Kikao cha leo kilikuwa kikao maalum ambacho kilipaswa kupitisha mswada huo
ambao baadaye utaidhinishwa na Rais kuwa sheria.
Wabunge wa upinzani wlaipinga mswada
huo na kuanza kurusha karatasi sakafuni huku wakitatiza shughuli bungeni humo.
Seneta Muthama alijeruhiwa mguuni
Mwenyekiti wa kamati ya usalama wa
bunge, Bwana Asman Kamama, alijaribu kuyataja mabadiliko yaliyopendekezwa kufanyiwa
mswada huo lakini wabunge walianza kuimba na kumzomea spika wa bunge wakiukataa
mswada huo wakisema 'bado mapambano.'
Spika wa bunge Justin Muturi wakati
mmoja alimuru walinzi wa bunge kuwaondoa baadhi ya viongozi waliofika bungeni
humo kwa mjhadala ambao ulitarajiwa kuwa kaa moto, hasa kw aupande wa upinzani.
Mswada huo ambao umewasilishwa bunge
kufuatia matukio ya utovu wa usalama na mashambulizi nchini Kenya, unapendekeza
kuwa washukiwaw augaidi wanaweza kuzuiliwa kwa mwaka mmoja huku polisi wakifanya
uchunguzi.
Mapendekezo ya mswada huo ni kwamba
mshukiwa wa ugaidi anaweza kuzuiliwa kwa siku 360 kutoka siku 90 za awali.
Pia ikiwa mswada huo utapistihwa
kuwa sheria, mashirika ya habari yatatozwa faini ya hadili shilingi milioni 5
kwa kuchapisha taarifa au picha ambazo zinaleta hofu na kusababisha taharuki.
Mswada huu umetolewa kufuatia
mashambulizi yaliyofanywa na wapiganaji wa Al Shabaab wakilalamika na kutaka
wanajeshi wa Kenya kuondolewa Somalia
Rais Kenyatta amekuwa akikabiliwa na
shinikzo kuimarisha usalama wa tangu mashambulizi ya Septemba mwaka 2013 katika
jengo la maduka ya kifahari la Westgate mjini Nairobi ambapo watu 67 waliuawa.
Naibu spika wa bunge Joyce Laboso amwagiwa maji mara baada ya vurugu kuanza.Kikao cha adhuhuri cha wabunge nchini Kenya, kinaendelea kuzua hisia kali huku wabunge wakiendelea kuvurugana humo. Wabunge hao wanajadili mswada tatanishi wa usalama ambao upande wa upinzani unasema unakwenda kinyume na katiba na kuwanyima wakenya haki yao ya kujieleza.
Mmoja wa wabunge hao wa upinzani amemwagia soda naibu spika Joyce Laboso ambaye alikuwa anasimamia kikao hicho cha kufanyia mswada huo mabadiliko kabla ya kupitishwa.
Spika wa bunge hilo sasa amechukua usukani na kuamuru kutimuliwa kwa wabunge wawili waliokuwa wamezidi vurugu.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni