Hizi ni nyakati za hatari sana hivyo wateule tuwe macho maana ni wakati wa kusimama kila mwamini katika zamu yake na kumlilia Mungu ili aepushe mauaji ya watu ya kila kukicha.
Polisi wanasema kuwa bomu hilo lililipuka wakati msafara
wa magari ya Umoja wa Mataifa mjini Mogadishuhuo ulipokuwa unaelekea karibu na barabara iliyoko karibu na uwanja wa ndege mjin humo.
Waokoaji katika harakati za kuzima moto.
Mlipuko wa pili iliripotiwa kulenga
vikosi vya muungano wa Afrika umbali wa kililomita 25 kutoka mjini humo ingawa
taarifa bado ni finyu.
Duru zimearifu kuwa mlipuko huo
huenda umesababishwa na mtu aliyejitolea muhanga aliyejilipua ndani ya gari.
Kundi la wapiganaji wa kiislamu la
Al- Shaabab mara kwa mara hutumia milipuko ya magari, lakini kufikia sasa
halijakiri kuhusika na mlipuko huo.
Maafisa wa usalama wa kigeni pia
walikuwepo katika eneo la shambulizi.
Kundi la Al-Shabab, ambalo
limehusishwa na wapiganaji wa al-Qaeda, limekuwa likifanya mashambulizi ya mara
kwa mara nchini Somalia na katika nchi jirani ya Kenya.
Mnamo siku ya Jumanne liliwaua watu
36 mjini Mandera karibu na mpaka na Somalia.
Hata hivyo bado halijatoa yamko
lolote kuhusu shambulizi lililofanywa mjini Mogadishu.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni