Wito umetolewa kwa
vijana nchini kutumia fursa mbalimbali
zinazojitokeza katika jamii ili kujikomboa
kiuchumi na kuliinua taifa kwa
ujumla.
Wito huo umetolewa na
Makamu wa Rais wa Vicoba Bibi
Scholastica Kevela alipokuwa akitoa msaada kwa kikundi cha Jambo Africa Group kwa
malengo ya kuinua Vijana Jijini Dar es Salaam.
Aidha Bibi Kevela
amesema vijana ni muhimu kupewa
kipaumbele katika Nyanja mbalimbali ili kumiliki uchumi na kupunguza utegemezi katika jamii.
Naye Mwalimu wa Ujasiriamali wa Vicoba kitaifa, Bibi Flora Masalu amesema kuwa, vijana wanapaswa
kuachana na dhana ya kuajiriwa na kujiajiri kwa kufanya shughuli za ujasiriamali.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni